Je, Wakumbuka?
Je, umeona matoleo ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi kuwa yenye msaada kwako? Basi kwa nini usitahini kumbukumbu lako kwa maswali yafuatayo?
◻ Ni nini tofauti kati ya “siku ya Bwana” na “siku ya Yehova”? (Ufunuo 1:10; Yoeli 2:11)
“Siku ya Bwana” yatia ndani utimizo wa yale maono 16 yafafanuliwayo katika Ufunuo sura ya 1 hadi ya 22 na matukio ya msingi aliyotabiri Yesu kwa kujibu swali la mitume wake juu ya ishara ya kuwapo kwake. Ukiwa upeo wa siku ya Bwana, siku yenye kutia hofu ya Yehova itafyatuka atekelezapo hukumu dhidi ya ulimwengu wa Shetani wenye ufisadi. (Mathayo 24:3-14; Luka 21:11)—12/15, ukurasa wa 11.
◻ Ni yapi baadhi ya mambo yenye kutokeza ya Biblia ya Makarios?
Jina Yehova laonekana zaidi ya mara 3,500 katika Biblia ya Makarios. Msomi mmoja wa fasihi ya kidini ya Kirusi, alisema hivi: “[Hiyo] tafsiri yashikamana sana na maandishi ya Kiebrania, na lugha ya hiyo tafsiri ni safi na yaifaa hiyo habari.”—12/15, ukurasa wa 27.
◻ Ni “kweli” gani ambayo Yesu alisema ingetuweka huru? (Yohana 8:32)
Alipotaja “kweli,” Yesu alimaanisha habari iliyopuliziwa kimungu—hasa habari kuhusu mapenzi ya Mungu—ambayo imehifadhiwa katika Biblia.—1/1, ukurasa wa 3.
◻ Yehu na Yehonadabu wa kisasa ni nani?
Yehu hufananisha Yesu Kristo ambaye awakilishwa duniani na “Israeli wa Mungu,” Wakristo watiwa-mafuta. (Wagalatia 6:16; Ufunuo 12:17) Kama vile Yehonadabu alivyotoka kwenda kumlaki Yehu, “umati mkubwa” kutoka katika mataifa umetoka ili kuwaunga mkono wawakilishi wa Yesu wa kidunia. (Ufunuo 7:9, 10; 2 Wafalme 10:15)—1/1, ukurasa wa 13.
◻ ‘Kutembea na Mungu’ kwamaanisha nini? (Mwanzo 5:24; 6:9)
Kwamaanisha kwamba watu wenye kufanya hivyo, kama vile Enoki na Noa, walijiongoza katika njia iliyotoa uthibitisho wa imani yenye nguvu katika Mungu. Walifanya yale ambayo Yehova aliwaamuru na walipatanisha maisha zao na yale waliyojua juu yake kutokana na shughuli zake na mwanadamu.—1/15, ukurasa wa 13.
◻ Kwa nini mtu apaswa apange kimbele kwa ajili ya uwezekano wa kifo chake?
Katika maana fulani, kufanya mipango ya namna hiyo ni zawadi kwa familia yako. Kwaonyesha upendo. Kwathibitisha tamaa ya ‘kuwaandalia kitu washiriki wa nyumba yako’ hata wakati ambapo hauko nao tena. (1 Timotheo 5:8)—1/15, ukurasa wa 22.
◻ “Agano la zamani” lilitimiza nini? (2 Wakorintho 3:14)
Liliandaa mimweko ya kimbele juu ya agano jipya na, kwa dhabihu zake za kurudiwa-rudiwa, lilionyesha uhitaji mkubwa wa mwanadamu wa kukombolewa katika dhambi na kifo. Lilikuwa ‘mfunzi likiongoza kwa Kristo.’ (Wagalatia 3:24)—2/1, ukurasa wa 14.
◻ Agano jipya ni lenye kudumu milele katika njia zipi? (Waebrania 13:20)
Kwanza, tofauti na agano la Sheria, hakuna jingine litakalochukua mahali pake. Pili, matokeo ya utendaji-kazi wake ni yenye kudumu. Na tatu, raia wa kidunia wa Ufalme wa Mungu wataendelea kunufaika na mpango wa agano jipya katika Milenia.—2/1, ukurasa wa 22.
◻ Ni manufaa gani zitokanazo na kuwa mwenye shukrani?
Ule uchangamshi ambao mtu hupata kwa sababu ya kuwa mwenye shukrani moyoni huchangia furaha yake na amani. (Linganisha Mithali 15:13, 15.) Na ikiwa sifa ijengayo, shukrani humlinda mmoja asiwe na hisia zisizojenga kama hasira, wivu, na uchungu.—2/15, ukurasa wa 4.
◻ Wazaliwa kwa roho wametiwa katika maagano gani?
Agano jipya, ambalo Yehova hufanya pamoja na washiriki wa Israeli wa kiroho, na agano kwa ajili ya Ufalme, ambalo Yesu hufanya na wafuasi wa hatua zake watiwa-mafuta. (Luka 22:20, 28-30)—2/15, ukurasa wa 16.
◻ Ni misherehekeo gani mitatu mikubwa ambayo Waisraeli waliamriwa kuhudhuria?
Msherehekeo wa Keki Zisizotiwa Chachu, uliofuata mara tu baada ya Sikukuu ya Kupitwa ya Nisani 14; Msherehekeo wa Majuma, siku ya 50 kuanzia Nisani 16; na Msherehekeo wa Kukusanya, au Msherehekeo wa Vibanda, katika mwezi wa saba. (Kumbukumbu la Torati 16:1-15)—3/1, ukurasa wa 8, 9.
◻ Kwa nini ni pendeleo kuhudhuria makusanyiko ya Kikristo?
Yesu alisema hivi: “Palipo na wawili au watatu wakiwa wamekusanyika pamoja katika jina langu, hapo mimi nipo katikati yao.” (Mathayo 18:20; 28:20) Pia, njia ya maana ambayo kulishwa kiroho hufanywa ni kupitia mikutano ya kutaniko na vilevile makusanyiko yaliyo makubwa zaidi. (Mathayo 24:45)—3/1, ukurasa wa 14.
◻ Ni nini iliyo asili ya jina Nimrodi?
Wasomi kadhaa wana maoni yaliyo sawa kwamba jina Nimrodi halikuwa jina alilopewa wakati wa kuzaliwa. Badala ya hivyo, wao huliona kuwa jina ambalo alipewa baadaye ili lifaane na sifa yake ya kuasi baada ya hiyo sifa kuwa dhahiri.—3/15, ukurasa wa 25.
◻ Familia ni yenye umaana jinsi gani kwa jamii ya kibinadamu?
Binadamu wanahitaji familia. Historia yaonyesha kwamba mpango wa familia umomonyokapo, nguvu ya jumuiya mbalimbali na ya mataifa hudhoofika. Kwa hiyo ina tokeo la moja kwa moja juu ya uthabiti wa jamii na hali njema ya watoto na vizazi vya wakati ujao.—4/1, ukurasa wa 6.
◻ Kuna ithibati gani tatu kwamba Biblia ni Neno la Mungu?
(1) Ni sahihi kisayansi; (2) ina kanuni zenye kudumu ambazo ni zenye kutumika katika maisha ya kisasa; (3) ina unabii mahususi ambao umetimizwa, kama ithibitishwavyo na mambo ya hakika ya kihistoria.—4/1, ukurasa wa 15.