Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 5/1 kur. 5-7
  • Yehova Ni Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Ni Nani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Umaana wa Jina Lake
  • Sifa Zenye Nguvu za Yehova
  • Mungu wa Mataifa Yote
  • Manufaa za Kumjua Yehova
  • Yehova—Yeye Ni Nani?
    Yehova—Yeye Ni Nani?
  • Kumjua Mungu
    Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha
  • Mungu wa Kweli Ni Nani?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Jina Lililo Kuu Kupita Majina Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 5/1 kur. 5-7

Yehova Ni Nani?

YEHOVA alimwambia mmoja wa waabudu wake waaminifu hivi: “Mwanadamu hataniona akaishi.” (Kutoka 33:20) “Mungu ni roho,” nao wanadamu hawawezi kumwona kwa macho yao ya kimwili. (Yohana 4:24) Kama vile ambavyo kuangalia jua moja kwa moja wakati wa mchana kungeharibu macho yetu, pia lingekuwa jambo lenye kutuangamiza ikiwa tungeona Chanzo cha nishati iliyoumba si jua letu jangavu tu, bali pia mianga mingine mingi sana katika ulimwengu wote mzima.

Kwa furaha, hatuhitaji kumwona Mungu ili tumjue. Biblia humtambulisha Yule aliyetutayarishia kifurushi kizuri ajabu, yaani dunia, nayo hufunua utu wake. Kwa hiyo yafaa tuiangalie Biblia tupate kumjua Baba aliyetupatia uhai na kutuandalia makao yenye kupendeza tuwezamo kufurahia maisha.

Umaana wa Jina Lake

Majina yote yana maana, hata ingawa huenda wengi wasizijue maana hizo leo. Kwa kielelezo, jina lijulikanalo sana la Kiingereza, David, hutokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Mpendwa.” Jina la Muumba, Yehova, pia lina maana. Gani hiyo? Katika lugha ya awali ya Biblia, Kiebrania, jina la Mungu limeandikwa kwa herufi nne, YHWH, nalo laonekana karibu mara 7,000 katika sehemu ya Kiebrania ya Biblia. Jina la Mungu laeleweka kumaanisha “Yeye Husababisha Iwe.” Hilo hudokeza kwamba Yehova hujifanya kwa hekima awe chochote kile atakacho kuwa ili kutimiza makusudi yake. Yeye ni Muumba, Hakimu, Mwokozi, Mwendelezaji wa Uhai, na kwa hiyo aweza kutimiza ahadi zake. Na zaidi, katika Kiebrania, jina Yehova ni namna ya kitenzi ambacho hudokeza tendo fulani lililo katika hali ya kutimizwa. Naam, Yehova bado hujisababisha awe mtimizaji wa makusudi yake. Yeye ni Mungu aishiye!

Sifa Zenye Nguvu za Yehova

Biblia humfafanua Muumba kuwa “Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema [“fadhili-upendo,” NW] na kweli; mwenye kuwaonea huruma [“fadhili-upendo,” NW] watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi.” (Kutoka 34:6, 7) Usemi “fadhili-upendo” hufasili neno la maana sana la Kiebrania. Lamaanisha fadhili ambayo hujiambatisha yenyewe kwa upendo kwenye kitu fulani mpaka kusudi lake kuelekea hicho kitu litimizwe. Pia laweza kutafsiriwa kuwa “upendo mwaminifu-mshikamanifu.” Fadhili ya Yehova hujiambatisha kwa upendo kwa viumbe vyake na hutimiza kusudi lake lililo zuri ajabu. Je, usingethamini sana upendo huo kutoka kwa Yule ambaye amekupatia uhai?

Yehova si mwepesi wa hasira na ni wa haraka kusamehe makosa yetu. Inachangamsha kuwa na uhusiano wa karibu na mtu wa aina hiyo. Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba yeye huruhusu makosa. Yeye alitangaza hivi: “Mimi, BWANA [“Yehova,” NW], naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu.” (Isaya 61:8) Akiwa Mungu wa haki, hatavumilia milele watenda-dhambi wajasiri ambao hudumu katika uovu wao. Hivyo, twaweza kuwa na hakika kwamba kwa wakati wake mwenyewe, Yehova atasahihisha ukosefu wa haki ulioko ulimwenguni. Hatapuuza wenye kutaabishwa.

Si rahisi kudumisha usawaziko mkamilifu kati ya upendo na haki. Ikiwa wewe ni mzazi, je, wewe huona ikiwa vigumu kuamua wakati, jinsi, na kadiri ambayo wapaswa kurekebisha watoto wako wanapokosea? Ili kusawazisha haki na upendo wenye wororo, hekima ya kiwango cha juu yahitajiwa. Yehova huonyesha sifa hiyo kwa wingi anaposhughulika na wanadamu. (Waroma 11:33-36) Kwa kweli, hekima ya Muumba yaweza kuonekana kila mahali, kwa kielelezo katika ajabu za uumbaji unaotuzunguka.—Zaburi 104:24; Mithali 3:19.

Hata hivyo, kuwa na hekima hakutoshi. Ili kutimiza mapenzi yake, Muumba lazima pia awe na nguvu, na Biblia hufunua kwamba yeye ni mwenye nguvu sana: “Inueni macho yenu juu, mkaone; ni nani aliyeziumba hizi; aletaye nje jeshi lao kwa hesabu; aziita zote kwa majina; kwa ukuu wa uweza wake, na kwa kuwa yeye ni hodari kwa nguvu zake; hapana moja isiyokuwapo mahali pake.” (Isaya 40:26) Yehova hufanya vitu kwa “ukuu wa uweza wake.” Je, sifa kama hiyo isikuvutie kwake?

Mungu wa Mataifa Yote

‘Lakini je, Yehova si Mungu wa “Agano la Kale,” Mungu wa Israeli ya kale?’ huenda ukauliza. Ni kweli kwamba Yehova alijitambulisha mwenyewe kwa Waisraeli. Ingawa hivyo, kwa msingi wa kuwa aliwaumba wanadamu wawili wa kwanza, Yehova ni Mungu “ambaye kwake kila familia . . . duniani hupata jina layo.” (Waefeso 3:15) Ikiwa waamini kwamba ni vizuri kustahi wazazi wako wa kale waliokufa, je, haingefaa kumsujudu Yule aliyempa mwanadamu wa kwanza uhai, mzazi wetu mmoja wa kale, ambaye ni chanzo cha nasaba zote zilizoko duniani leo?

Muumba wa wanadamu si mtu aliye na mawazo finyu. Ni kweli kwamba, wakati mmoja alikuwa na uhusiano wa pekee na taifa la Israeli. Lakini hata wakati huo, aliwapokea kwa moyo wote wale walioitia jina lake. Mfalme mwenye hekima wa Israeli alisali hivi kwa Yehova: “Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako . . . , usikie huko mbinguni, . . . ukatende kwa kadiri ya yote atakayokuomba mgeni huyo; ili watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako.” (1 Wafalme 8:41-43) Hadi siku hii, watu wa mataifa yote wanaweza kumjua Yehova na wawe na uhusiano mzuri naye. Lakini jambo hilo lakuathirije?

Manufaa za Kumjua Yehova

Kwa kurudia kile kielezi kilicho katika makala iliyotangulia, ikiwa ungepokea kifurushi kilichofungwa vizuri, bila shaka ungetaka kujua zawadi hiyo ilikuwa ya nini. Yapasa kutumiwaje na kutunzwaje? Vivyo hivyo, twataka kujua kile ambacho Mungu alikusudia alipotutayarishia dunia. Biblia husema kwamba “hakuiumba ukiwa,” bali “aliiumba ili ikaliwe na watu,” yaani, na wanadamu.—Isaya 45:18.

Ingawa hivyo, wanadamu wengi zaidi, hawajatunza zawadi ya Muumba. Wamo katika hatua ya kuiharibu dunia, wakimchukiza Yehova sana. Lakini, kulingana na linalomaanishwa na jina lake, Yehova ameazimia kutimiza kusudi lake la awali kuelekea mwanadamu na dunia. (Zaburi 115:16; Ufunuo 11:18) Atarekebisha dunia na kuwapa iwe urithi wale walio tayari kuishi wakiwa watoto wake watiifu.—Mathayo 5:5.

Kitabu cha mwisho cha Biblia hufafanua jinsi mambo yatakavyokuwa jambo hilo litukiapo: “Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa vikundi vya watu wake. . . . Naye atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” (Ufunuo 21:3, 4) Wakati huo hakuna mtu atakayetoa machozi ya huzuni au kuomboleza kwa sababu ya kumpoteza mpendwa. Hakuna atakayelia akitaka msaada kwa sababu ya kukata tamaa au kuumizwa na maradhi yenye kufisha. Hata “kifo kitafanywa kuwa si kitu.” (1 Wakorintho 15:26; Isaya 25:8; 33:24) Hilo hufafanua aina ya maisha ambayo Yehova alitaka sisi tufurahie awali alipoumba wazazi wetu wa kale waliokufa.

Kwa kweli, unaweza kuwa na mwono wa kimbele wa hali hizo za kiparadiso ambazo sasa zimo miongoni mwa waabudu wa Yehova. Yeye huwaambia hivi: “Mimi ni BWANA [“Yehova,” NW], Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.” (Isaya 48:17) Yehova ni Baba mwenye fadhili ambaye hutufundisha sisi watoto wake, njia bora ya kuishi. Miongozo yake kwa wanadamu, huandaa ulinzi wenye upendo, si kizuizi kisichofaa. Kuifuata kutatokeza uhuru na furaha ya kweli, kama tu ilivyoandikwa: “Sasa Yehova ndiye Roho; na iliko roho ya Yehova, kuna uhuru.” (2 Wakorintho 3:17) Kwa kufuata miongozo iliyowekwa katika Biblia, wale wanaokubali utawala wake sasa wanapata amani ya akili ambayo siku moja itaenea katika ulimwengu wote wa wanadamu.—Wafilipi 4:7.

Yehova ni Baba mkarimu kama nini! Je, uko tayari kujifunza mengi zaidi kuhusu Yule aliyezibuni ajabu zote za uumbaji? Kwa wale walio tayari, manufaa ni nyingi sana hata sasa. Na wakati ujao baraka zitakuwa za milele.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Jina la Mungu likiwa limeandikwa katika zile herufi nne za Kiebrania laweza kuonekana kwenye kuta za makanisa mengi ya zamani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki