Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 8/1 uku. 8
  • Subira na Uvumilivu Huleta Matokeo Mazuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Subira na Uvumilivu Huleta Matokeo Mazuri
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • “Dhihirisheni Subira”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kwa Nini Ninafurahia Kufanya Wanafunzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 8/1 uku. 8

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Subira na Uvumilivu Huleta Matokeo Mazuri

YESU KRISTO alitabiri kwamba katika siku za mwisho ‘upendo wa idadi iliyo kubwa zaidi ungepoa.’ Kwa sababu hiyo, katika sehemu nyingi za ulimwengu watu kwa ujumla hawapendezwi na habari njema za Ufalme. Wengine hata hudharau dini.—Mathayo 24:12, 14.

Licha ya hali hizo, watangazaji wa Ufalme wanafanikiwa kukabiliana na ugumu huo kwa sababu ya imani na uvumilivu wao, kama inavyoonyeshwa na jambo hili lililoonwa kutoka Jamhuri ya Cheki.

Mashahidi wawili walizungumza na mwanamke fulani akiwa amefunga mlango. Baada ya muda mfupi, mlango ulifunguliwa kidogo, na mkono ukanyooshwa kutoka ndani ukashika magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ambayo Mashahidi hao walimwonyesha. Walisikia sauti ikisema “asante,” kisha mlango ukafungwa. “Je, turudi?” Mashahidi hao wakajiuliza. Mmoja wao ambaye ni painia, au mhudumu wa wakati wote, aliamua kurudi lakini mambo yakawa kama yalivyokuwa hapo mwanzoni na hali hiyo ikaendelea kwa mwaka mmoja.

Baada ya kuamua kubadili utangulizi wake, painia huyo alisali kwa Yehova apate msaada. Kwenye ziara nyingine alipompelekea mwanamke huyo magazeti, alimwuliza hivi kwa urafiki: “Habari yako? Je, ulifurahia kusoma magazeti hayo?” Kwanza, mwanamke huyo hakujibu, lakini baada ya ziara nyingine kadhaa, akaanza kuwa mwenye urafiki. Wakati mmoja alifungua mlango wazi lakini mazungumzo yalikuwa mafupi.

Kwa sababu mwanamke huyo alisita kuongea naye mlangoni, yule painia aliamua kumwandikia barua ya kumweleza kwa nini amekuwa akimtembelea na jinsi ambavyo angeweza kujifunza Biblia nyumbani. Mwishowe, baada ya kujitahidi kwa uvumilivu kwa mwaka mmoja na nusu, painia huyo alifaulu kuanzisha funzo la Biblia na mwanamke huyo. Painia huyo alishangaa lakini akatiwa moyo wakati mwanamke huyo alipomwambia baadaye: “Nilianza kumwamini Mungu mlipoanza kuniletea magazeti haya.”

Kwa kweli, subira na uvumilivu zinaweza kuleta matokeo mazuri katika kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi.—Mathayo 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki