Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w06 4/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kutoka Mchirizi wa Maziwa Hadi Kijiko cha Maziwa ya Unga
    Amkeni!—1999
  • Maziwa ya Mama
    Je, Ni Kazi ya Ubuni?
  • “Sheria ya Bwana Ni Kamilifu”
    Mkaribie Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
w06 4/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Tunaweza kujifunza nini kutokana na amri hii katika kitabu cha Kutoka 23:19: “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake”?

Amri hiyo katika Sheria ya Musa, ambayo inapatikana mara tatu katika Biblia, inaweza kutusaidia kuelewa maoni ya Yehova kuhusu mambo yanayofaa, huruma zake, na fadhili zake. Pia, amri hiyo inakazia jinsi anavyochukia ibada ya uwongo.—Kutoka 34:26; Kumbukumbu la Torati 14:21.

Kumtokosa mbuzi mchanga au mnyama yeyote mchanga katika maziwa ya mama yake kungepingana na mpango wa Yehova. Mungu aliandaa maziwa ya mama ili kumlisha mtoto na kumsaidia kukua. Kulingana na msomi fulani, kumpika mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake kungemaanisha “kutoheshimu uhusiano uliopo kati ya mzazi na mtoto ambao Mungu ameuweka na kuutakasa.”

Isitoshe, watu wengine hudokeza kwamba huenda desturi ya kumtokosa mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake ilikuwa desturi ya kipagani iliyofanywa ili kutokeza mvua. Ikiwa ilikuwa desturi ya kipagani, basi amri hiyo iliwalinda Waisraeli kutokana na desturi za kidini zisizo na maana na za kikatili zilizofanywa na mataifa jirani. Sheria ya Musa iliwakataza Waisraeli wasitembee katika sheria za mataifa hayo.—Mambo ya Walawi 20:23.

Mwishowe, sheria hiyo inaonyesha huruma nyororo za Yehova. Kwa kweli, Sheria ilikuwa na amri nyingi zilizokataza kuwatendea wanyama kikatili na kufanya mambo yanayopingana na sheria za asili. Kwa mfano, Sheria ilitia ndani amri zilizokataza kumtoa dhabihu mnyama ambaye hakuwa amekaa na mama yake kwa angalau siku saba, kumchinja mnyama na mtoto wake siku ileile, na kumchukua ndege pamoja na mayai au vifaranga wake kutoka katika kiota chake.—Mambo ya Walawi 22:27, 28; Kumbukumbu la Torati 22:6, 7.

Bila shaka, Sheria haikuwa na amri na vizuizi vigumu. Faida moja ya Sheria ni kanuni zake ambazo hutusaidia kudumisha maadili mazuri yanayoonyesha sifa bora za Yehova.—Zaburi 19:7-11.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]

© Timothy O’Keefe/Index Stock Imagery

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki