Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w08 3/1 uku. 12
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Maisha Katika Nyakati za Biblia—Pesa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Sauli—Chombo-Kichaguliwa kwa Bwana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Ametumbukiza Zaidi ya Wote
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Jinsi Ambavyo Jina la Mungu Limejulishwa
    Amkeni!—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
w08 3/1 uku. 12

Je, Wajua?

Sarafu mbili za yule mjane zilikuwa na thamani gani?

Katika karne ya kwanza W.K., Wayahudi walilipa kodi ya hekalu ya kila mwaka ya “drakma mbili,” ambayo ililingana na mshahara wa kazi ya siku mbili. (Mathayo 17:24) Tofauti na hilo, Yesu alisema kwamba shomoro wawili waliuzwa kwa “sarafu ya thamani ndogo,” ambayo inalingana na mshahara wa kazi ya dakika 45. Pia, shomoro watano wangeweza kununuliwa kwa bei iliyokuwa mara mbili ya hiyo, au iliyolingana na mshahara wa kazi ya dakika 90.—Mathayo 10:29; Luka 12:6.

Mchango wa hekalu uliotolewa na yule mjane ambaye Yesu aliona ulikuwa wenye thamani ndogo kuliko bei ya shomoro watano. Sarafu hizo mbili, au lepta mbili, ndizo zilizokuwa sarafu ndogo zaidi za shaba ambazo zilitumiwa wakati huo katika Israeli. Thamani yake ilikuwa sawa na sehemu moja ya 64 tu ya mshahara wa siku moja, au tukipiga hesabu kwa siku moja ya kazi ambayo kwa wastani ilikuwa na saa 12, basi thamani yake ilikuwa sawa na mshahara wa kazi iliyofanywa kwa muda usiozidi dakika 12.

Yesu Kristo alisema kwamba zawadi ya mjane huyo ilikuwa na thamani kubwa zaidi kuliko zile za wote waliotoa zaidi “kutokana na ziada yao.” Kwa nini? Simulizi hilo linasema kwamba mjane huyo alikuwa na “sarafu ndogo mbili,” kwa hiyo angeweza kutoa moja na kubaki na moja. Hata hivyo, alitoa “vyote alivyokuwa navyo, riziki yake yote.”—Marko 12:41-44; Luka 21:2-4.

Ni wakati gani ambapo Sauli alianza kuitwa Paulo?

Mtume Paulo alizaliwa akiwa Mwebrania mwenye uraia wa Roma. (Matendo 22:27, 28; Wafilipi 3:5) Kwa hiyo, inaelekea kwamba tangu alipokuwa mtoto, alipewa jina la Kiebrania Sauli na jina la Kiroma Paulo. Hata watu fulani wa ukoo wa Paulo walikuwa na majina ya Kiroma na ya Kigiriki. (Waroma 16:7, 21) Zaidi ya hilo, ilikuwa kawaida kwa Wayahudi wa wakati huo, hasa wale walioishi nje ya Israeli, kuwa na majina mawili.—Matendo 12:12; 13:1.

Zaidi ya miaka kumi baada ya kuwa Mkristo, inaonekana kwamba bado wengi walimjua mtume huyo kwa jina lake la Kiebrania, Sauli. (Matendo 13:1, 2) Hata hivyo, wakati wa safari yake ya kwanza ya umishonari, mwaka wa 47/48 hivi W.K., inaonekana alipendelea kutumia jina lake la Kiroma, Paulo. Aliagizwa ahubiri habari njema kwa wasio Wayahudi, na huenda aliona kwamba jina lake la Kiroma lingekubaliwa kwa urahisi. (Matendo 9:15; 13:9; Wagalatia 2:7, 8) Pia, huenda alitumia jina Paulo kwa sababu matamshi ya Kigiriki ya jina lake la Kiebrania, Sauli, yanafanana sana na neno fulani la Kigiriki lenye maana mbaya. Hata sababu ya kubadili jina lake iwe nini, Paulo alionyesha kwamba alikuwa tayari ‘kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote, ili kwa vyovyote awaokoe wengine.’—1 Wakorintho 9:22.

[Picha katika ukurasa wa 12]

Lepta, ukubwa halisi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki