Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 7/1 kur. 30-31
  • Jinsi ya Kutafuta Marafiki Washikamanifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutafuta Marafiki Washikamanifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Uharibifu wa Sodoma na Gomora
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Yesu Anawaponya Watu Kimuujiza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Ashtakiwa kwa Uwongo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yesu Awashangaza Wasikilizaji Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 7/1 kur. 30-31

Kwa Ajili ya Vijana

Jinsi ya Kutafuta Marafiki Washikamanifu

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Yonathani, Daudi, na Sauli

Muhtasari: Yonathani anakuwa rafiki mkubwa wa Daudi baada ya Daudi kumwua Goliathi.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA 1 SAMWELI 17:57–18:11; 19:1; 20:1-17, 41, 42.

Unafikiri Sauli alikuwa na sura ya aina gani? (Dokezo: Ona 1 Samweli 10:20-23.)

․․․․․

Huenda Daudi alikuwa tineja alipokutana na Yonathani. Unafikiri alikuwa na sura ya aina gani? (Dokezo: Ona 1 Samweli 16:12, 13.)

․․․․․

Unafikiri sauti za Daudi na Yonathani zilikuwa na hisia gani walipokuwa wakiachana kama inavyoonyeshwa na sehemu ya mwisho ya 1 Samweli sura ya 20?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Simulizi hili linataja kuwa “nafsi ya Yonathani ikashikamana na nafsi ya Daudi.” (1 Samweli 18:1) Huenda Yonathani alivutiwa na sifa gani za Daudi? (Dokezo: Ona 1 Samweli 17:45, 46.)

․․․․․

Huenda Yonathani alimzidi Daudi kwa umri wa miaka 30 hivi. Unafikiri, ni nini kilichowasaidia kuwa “marafiki wazuri” ingawa walikuwa na tofauti kubwa hivyo katika umri wao?

․․․․․

Kulingana na simulizi hili, ni mambo gani yatakayokusaidia kujua marafiki wa kweli? (Dokezo: Ona Methali 17:17; 18:24.)

․․․․․

Kwa nini Yonathani alikuwa mshikamanifu kwa Daudi kuliko kwa baba yake?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Urafiki.

․․․․․

Ushikamanifu.

․․․․․

Urafiki na watu walio na umri mkubwa.

․․․․․

Unaweza kuwavutia marafiki wanaofaa kwa njia gani?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

SOMA HABARI ZAIDI ZA BIBLIA, KWENYE INTANETI www.watchtower.org

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki