Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 11/1 kur. 6-7
  • Swali la 2: Ni Nini Kitakachonipata Nitakapokufa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Swali la 2: Ni Nini Kitakachonipata Nitakapokufa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Wafu Wako Wapi?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Tukifa tunaenda wapi?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • “Kifo Kimemezwa Milele”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?
    Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 11/1 kur. 6-7

SWALI LA 2: Ni Nini Kitakachonipata Nitakapokufa?

ROMAN alipokuwa mvulana, rafiki yake wa karibu alikufa katika aksidenti ya gari. Alisema hivi: “Kifo cha rafiki yangu kilinishtua sana. Miaka mingi baada ya aksidenti hiyo, nilijiuliza nini hutupata tunapokufa.”

Kwa nini tuulize swali hilo?

Kifo cha binadamu ni jambo lisilo la kawaida. Hata tuwe na umri gani, sote hatupendi kufa. Wengi huogopa jambo linalotukia baada ya kifo.

Watu fulani wanafikiri jibu ni nini?

Wengi wanaamini kwamba mtu anapokufa sehemu fulani ya mtu huyo huendelea kuishi. Wanaamini kwamba watu wazuri watathawabishwa kwa kwenda mbinguni, huku wale waliokuwa wabaya wakiadhibiwa milele kwa sababu ya dhambi zao. Wengine wanafikiri kwamba mtu anapokufa haendi popote na mwishowe anasahaulika kabisa.

Majibu hayo yanamaanisha nini?

Jibu la kwanza linaonyesha kwamba wakati wa kifo mtu hafi kabisa. Jibu la pili linaonyesha kwamba maisha hayana kusudi. Wale wanaofikiri kwamba mtu anapokufa haendi popote, huenda wakawa na mtazamo huu hatari: “Na tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.”—1 Wakorintho 15:32.

Biblia inafundisha nini?

Biblia haifundishi kwamba baada ya kufa sehemu fulani ya mtu huendelea kuishi. Mungu alimwongoza Mfalme Sulemani kuandika hivi: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5) Wale ‘wasiojua lolote’ hawajui kinachoendelea. Hawawezi kuhisi wala kutenda. Hivyo, watu waliokufa hawawezi kuwasaidia wala kuwadhuru walio hai.

Kinyume na jinsi watu wengi wanavyoamini, Mungu hakukusudia wanadamu wafe. Alimuumba mwanadamu wa kwanza, Adamu, akiwa na tarajio la kuishi milele duniani. Mungu alitaja kifo alipomwambia Adamu kuhusu adhabu ya kutotii. Alimkataza Adamu asile tunda la mti fulani kisha akamwonya kwamba ikiwa angekula tunda hilo ‘angekufa hakika.’ (Mwanzo 2:17) Ikiwa Adamu na Hawa wangeendelea kuwa watiifu wao pamoja na wazao wao ambao wangekuwa washikamanifu kwa Mungu, wangeishi milele duniani.

Adamu aliamua kupuuza onyo la Mungu. Alifanya dhambi alipokosa kumtii Mungu, hivyo akafa. (Waroma 6:23) Hakuna sehemu ya mwili wa Adamu iliyoendelea kuishi baada ya kufa. Badala yake, Adamu alipokufa hakuwepo. Mungu alimwambia Adamu hivi: “Kwa jasho la uso wako utakula mkate mpaka utakaporudi katika udongo, kwa kuwa ulitolewa katika huo. Kwa maana wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.” (Mwanzo 3:19) Kwa kuwa wanadamu wote ni wazao wa Adamu, tumerithi dhambi na kifo kutoka kwake.—Waroma 5:12.

Ingawa Adamu alifanya uamuzi mbaya, Mungu atatimiza ahadi yake ya kujaza dunia na wazao wa Adamu. (Mwanzo 1:28; Isaya 55:11) Hivi karibuni, Yehova atawafufua watu wengi waliokufa. Akizungumza kuhusu wakati huo mtume Paulo alisema: “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15.

Roman, aliyetajwa mapema alijifunza Biblia na akatambua mambo inayofundisha kuhusu kifo na kumhusu Yehova Mungu. Mambo aliyojifunza yalimchochea sana. Soma simulizi lake katika ukurasa wa 11 wa gazeti hili.

Ili upate habari zaidi kuhusu jambo linalotukia baada ya kifo, ona sura ya 6 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Unaweza kukipakua kwenye Tovuti ya www.jw.org/sw

Yesu Alisema Nini Kuhusu Kifo?

Yesu hakukubaliana na viongozi wa kidini wa siku zake waliosema kwamba hakutakuwa na ufufuo wa wafu. (Luka 20:27) Wala hakufundisha kwamba sehemu fulani ya mwanadamu huendelea kuishi baada ya kifo. Badala yake, Yesu alifundisha mambo yafuatayo.

Kifo ni kama usingizi. Rafiki yake, Lazaro, alipokufa, Yesu alisema: “Lazaro rafiki yetu anapumzika, lakini ninafunga safari kwenda huko ili kumwamsha kutoka usingizini.” Wanafunzi wa Yesu hawakuelewa alichomaanisha. Walimjibu: “Bwana, ikiwa anapumzika, atapona.” Simulizi hilo la Biblia linaeleza hivi: “Yesu alikuwa amesema juu ya kifo chake. Lakini walifikiri alikuwa akisema juu ya kupumzika katika usingizi. Kwa hiyo, wakati huo, Yesu akawaambia waziwazi: ‘Lazaro amekufa.’”—Yohana 11:11-14.

Wafu watafufuliwa. Yesu alipofika katika mji wa nyumbani wa Lazaro, alimfariji Martha, dada ya Lazaro, kwa kumwambia: “Ndugu yako atafufuka.” Kisha, Yesu akatoa ahadi hii muhimu sana: “Mimi ndiye ufufuo na uzima. Yule anayeniamini, hata akifa, atarudi kwenye uzima.” Ahadi ya Yesu haikuwa maneno matupu tu. Mbele ya mashahidi wengi, Yesu alimfufua Lazaro, ingawa alikuwa amekufa kwa siku nne.—Yohana 11:23, 25, 38-45.

Katika ufunuo aliompa mtume Yohana, Yesu aliahidi tena kwamba wafu watafufuliwa. Alieleza kuhusu wakati ujao ambapo watu watawekwa huru kwa njia ya mfano kutokana na utumwa wa kifo.—Ufunuo 20:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki