Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 8/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Je! Mungu Anasikiliza Sala Zako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 8/1 uku. 16
[Picha katika ukurasa wa 16]

Majibu ya Maswali ya Biblia

Je, Mungu husikiliza sala zote?

Mungu husikiliza watu wa mataifa yote. (Zaburi 145:18, 19) Neno lake, Biblia, hutuhimiza tumweleze jambo lolote linalotuhangaisha. (Wafilipi 4:6, 7) Hata hivyo, si sala zote zinazompendeza Mungu. Kwa mfano, hapendezwi na sala zenye maneno yanayorudiwa-rudiwa.​—Soma Mathayo 6:7.

Pia, Yehova hapendezwi na sala za watu wanaovunja sheria zake kimakusudi. (Methali 28:9) Kwa mfano, katika nyakati za Biblia, Mungu alikataa kuwasikiliza Waisraeli waliokuwa na hatia ya kuua. Kwa kweli, ni lazima tutimize mambo fulani ili Mungu atusikilize.​—Soma Isaya 1:15.

Tunapaswa kufanya nini ili Mungu atusikilize?

Ili Mungu atusikilize tunapaswa kusali tukiwa na imani. (Yakobo 1:5, 6) Ni lazima tuwe na hakika kwamba yupo na anatujali. Tunaweza kuimarisha imani yetu kwa kujifunza Biblia kwa sababu imani ya kweli hutegemea uthibitisho na uhakika unaopatikana katika Neno la Mungu.​—Soma Waebrania 11:1, 6.

Tunapaswa kusali kwa unyoofu na kwa unyenyekevu. Hata Yesu, Mwana wa Mungu, alisali kwa unyenyekevu. (Luka 22:41, 42) Hivyo, badala ya kumwambia Mungu jambo la kufanya, tunapaswa kujitahidi kuelewa sheria zake kwa kusoma Biblia. Na hivyo tunaweza kusali kupatana na mapenzi ya Mungu.​—Soma 1 Yohana 5:14.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 17 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kupakua kitabu hiki kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki