Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 11/1 uku. 4
  • Uwongo Unaomfanya Mungu Asiwe na Jina

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwongo Unaomfanya Mungu Asiwe na Jina
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu na Lako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Mungu Anaitwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 11/1 uku. 4

HABARI KUU | UWONGO UNAOFANYA WATU WASIMPENDE MUNGU

Uwongo Unaomfanya Mungu Asiwe na Jina

MAONI YA WATU WENGI

“Hatujafikia muafaka ikiwa Mungu ana jina, na ikiwa analo, hatulijui.”​—Profesa David Cunningham, Theological Studies.

UKWELI WA BIBLIA

Mungu alisema: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.” (Isaya 42:8) Yehova ni jina la Kiebrania linalomaanisha “Yeye Husababisha Kuwa.”​—Mwanzo 2:4.

Yehova anataka tutumie jina lake. “Liitieni jina lake,” Biblia inasema. “Tangazeni matendo yake kati ya vikundi vya watu. Semeni kwamba jina lake limeinuliwa juu.”​—Isaya 12:4.

Yesu alilitumia jina la Mungu. Yesu alisali hivi kwa Yehova: “Nimewajulisha [wanafunzi wa Yesu] jina lako nami nitalijulisha.” Kwa nini Yesu aliwajulisha wanafunzi wake jina la Mungu? Aliendelea kusema hivi: “Ili upendo ulionipenda nao upate kuwa ndani yao nami katika muungano pamoja nao.”​—Yohana 17:26.

KWA NINI NI MUHIMU?

Mwanatheolojia Walter Lowrie aliandika hivi: “Mtu asiyelijua jina la Mungu hawezi kumwona Mungu kuwa mtu halisi na pia hawezi kumpenda ikiwa anafikiri Mungu ni nguvu isiyo na utu.”

Mwanamume mmoja anayeitwa Victor alienda kanisani kila juma, lakini hakuhisi kwamba anamjua Mungu vizuri. Anasema: “Kisha nilijifunza kwamba Mungu anaitwa Yehova, na hivyo nikamjua rasmi. Nilihisi kama hatimaye nimekutana na Mtu niliyemsikia kwa muda mrefu. Nilianza kumuona kama Mtu halisi na kuanzisha urafiki pamoja naye.”

Yehova huwakaribia wale wanaotumia jina lake. Mungu anawaahidi “wale wanaolifikiria jina lake” hivi: “Nitawaonyesha huruma, kama vile mwanamume anavyomwonyesha huruma mwana wake ambaye anamtumikia.” (Malaki 3:16, 17) Pia, Mungu huwathawabisha wale wanaoliitia jina lake. Biblia inasema hivi: “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”​—Waroma 10:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki