Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 7/15 kur. 20-21
  • Je, Ni Lazima Wengine Watambue Kazi Yako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ni Lazima Wengine Watambue Kazi Yako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KAZI ZENYE KUVUTIA ZILIZOONWA NA WATU WACHACHE
  • KURIDHIKA BILA KUSIFIWA NA WENGI
  • Tumepewa Uwezo wa Kufanya Kazi ya Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Waaminifu wa Zamani Waliongozwa na Roho ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mapendekezo ya Kuanzisha Mazungumzo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Roho Takatifu Yatenda Kazi juu ya Watu wa Zamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 7/15 kur. 20-21
Bezaleli na Oholiabu wakitengeneza makerubi wa dhahabu

Je, Ni Lazima Wengine Watambue Kazi Yako?

BEZALELI na Oholiabu walifahamu kazi ya ujenzi. Hawangependa kukumbuka kazi kubwa waliyofanya ya kutengeneza matofali mengi walipokuwa watumwa huko Misri. Lakini mambo hayo yalikuwa yamepita. Sasa wangekuwa wasanii stadi baada ya kupewa mgawo wa kuongoza katika kazi ya kujenga maskani. (Kut. 31:1-11) Hata hivyo, watu wachache sana wangeona kazi maridadi walizofanya. Je, jambo hilo liliwavunja moyo? Je, ilikuwa lazima wengine watambue kazi yao? Je, ni lazima wengine watambue kazi yako?

KAZI ZENYE KUVUTIA ZILIZOONWA NA WATU WACHACHE

Baadhi ya vyombo vya maskani vilikuwa vya pekee sana. Kwa mfano, fikiria makerubi wa dhahabu waliokuwa juu ya sanduku la agano. Mtume Paulo alisema kuwa ni “wenye utukufu.” (Ebr. 9:5) Hebu wazia uzuri wa maumbo hayo yaliyotengenezwa kwa dhahabu safi!—Kut. 37:7-9.

Ikiwa vifaa ambavyo Bezaleli na Oholiabu walitengeneza vingekuwapo leo, basi vingewekwa kwenye majumba maarufu ya makumbusho na kuwavutia watu wengi sana. Lakini wakati vilipotengenezwa, ni watu wangapi walioona uzuri wake? Makerubi waliwekwa katika Patakatifu Zaidi; hivyo wangeonwa na kuhani mkuu tu alipoingia mara moja kwa mwaka, katika Siku ya Upatanisho. (Ebr. 9:6, 7) Kwa hiyo, ni wanadamu wachache sana waliowaona makerubi hao.

KURIDHIKA BILA KUSIFIWA NA WENGI

Ikiwa ungekuwa Bezaleli au Oholiabu na umefanya kazi kubwa ya kutengeneza vyombo hivyo bora, ungehisije baada ya kujua kwamba vilionwa na watu wachache sana? Leo watu huridhika wanaposifiwa na kuheshimiwa kwa sababu ya kazi zao. Wanahisi kwamba hicho ni kipimo cha kuwasaidia wajue thamani ya kazi zao. Lakini watumishi wa Yehova wako tofauti. Kama Bezaleli na Oholiabu, tunaridhika kwa kufanya mapenzi ya Yehova na kupata kibali chake.

Katika siku za Yesu, ilikuwa kawaida kwa viongozi wa kidini kutoa sala ili kuwapendeza watu. Hata hivyo, Yesu alipendekeza njia nyingine: Sali kwa unyofu bila kutaka kusifiwa na wanaokutazama. Matokeo yatakuwa nini? “Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.” (Mt. 6:5, 6) Hivyo, jambo la muhimu ni maoni ya Yehova kuhusu sala zetu, na si maoni ya watu. Maoni yake hufanya sala zetu ziwe zenye thamani sana. Inafaa tuwe na maoni kama hayo kuhusu jambo lolote tunalotimiza katika utumishi wetu mtakatifu. Kazi yetu ni muhimu kwa sababu inampendeza Yehova, “anayetazama akiwa mahali pa siri,” na si kwa sababu tunasifiwa na watu.

Maskani ilipokamilika, wingu “likaanza kufunika hema la mkutano, na utukufu wa Yehova ukaijaza maskani.” (Kut. 40:34) Huo ulikuwa uthibitisho ulio wazi wa kibali cha Yehova! Unafikiri Bezaleli na Oholiabu walihisije wakati huo? Ingawa majina yao hayakuandikwa kwenye vyombo walivyotengeneza, waliridhika sana kwa kujua kwamba Mungu alibariki jitihada zao zote. (Met. 10:22) Katika miaka iliyofuata, walifurahi sana kuona vitu walivyotengeneza vikiendelea kutumiwa katika utumishi wa Yehova. Watakapofufuliwa katika ulimwengu mpya, bila shaka Bezaleli na Oholiabu watafurahi sana kujua kwamba maskani ilitumiwa kwa ajili ya ibada ya kweli kwa miaka 500 hivi!

Ndugu na dada wakifanya kazi mbalimbali kwa unyenyekevu na utayari

Hata ikiwa hakuna mwanadamu anayeona utumishi wako unaofanya kwa unyenyekevu na utayari, Yehova anaona!

Leo katika tengenezo la Yehova, wale wanaotengeneza vibonzo, wachoraji, wanamuziki, wapiga picha, watafsiri, na waandishi hawajulikani kwa majina katika kazi wanazofanya. Kwa njia hiyo, hakuna mtu “anayeona” kile wanachofanya. Ndivyo ilivyo pia kuhusu kazi nyingi zinazofanywa katika makutaniko zaidi ya 110,000 ulimwenguni pote. Ni nani anayeona mtumishi wa hesabu anapojaza fomu za hesabu kila mwezi? Ni nani anayeona mwandishi anapotayarisha ripoti ya utumishi wa shambani ya kutaniko? Ni nani anayeona ndugu au dada anapofanya marekebisho muhimu katika Jumba la Ufalme?

Katika maisha yao, Bezaleli na Oholiabu hawakupata vikombe, medali, au tuzo kutokana na ubunifu wa hali ya juu na ubora wa kazi walizofanya. Lakini walipata kitu chenye thamani zaidi, yaani, kibali cha Yehova. Tuna uhakika kwamba Yehova alitambua kazi zao. Acheni tuige unyenyekevu na utayari walioonyesha katika utumishi wao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki