Roho Takatifu Yatenda Kazi juu ya Watu wa Zamani
(Funzo la Kitabu)
1. Biblia pake yake kama kitabu inakanushaje wale wanaokataa kwamba hakuna kitu kama roho takatifu?
NI KAZI bure kwa watu wenye kuamini vionekanavyo tu leo kubisha kwamba hakuna kitu kama roho takatifu. Kifaa kilichotokezwa kwa utendaji wake juu ya wanadamu wa zamani tungali nacho, ulimwenguni pote. Kifaa iiicho jtiuieokoka ingawa wanadamu na mataifa wamejitahidi sana wakihafibu. Ni kifaa gani? Ni kitabu lisichoweza kuharibiwa kinachoitwa Biblia Takatifu. Ingawa wanadamu na mashetani wamefanya npinzani m’kali sana, Kitabu hicho kitakatifu ndicho kinachoenezwa zaidi kuliko vitabu vilivyoandikwa na wanadamu. Wako wanaume na wanawake wanaotumia Kitabu hicho watetee maisha zao zenyewe.
2. Kwa sababu gani Biblia si tofauti na vitabu vingine kwa habari ya mikono iliyotumiwa kuiandika?
2 Biblia Takatifu ni tofauti na vitabu vingine vyote. Kwa sababu gani? Si kwa sababu iliandikwa na wanadamu dhaifu. Hakuna mtu anayedai kwamba Biblia iliandikwa na mikono isiyo ya wanadamu dhaifu. Lakini ni watu wa namna gani walioiandika? Je! waliyoandika yalikuwa ya kujitungia? Hilo ni jambo la maana kujua tufanye uamuzi.
3-5. (a) Biblia yatuambia iliandikwaje? (b) Petro ahakikishaje hilo katika 2 Petro 1:15-21?
3 Biblia yenyewe yatuambia kwamba vitabu 66 vidogo zaidi vilivyomo viliandikwa na wanadamu. Biblia yenyewe yatuambia waandikaji wake walikuwa watu wa namna gani. Inaonyesha pia nguvu isiyoonekana iliyoongoza watu hao waandike. Kulikuwa na roho yenye kuwaongoza walipokuwa wakiandika. Roho hiyo haikuwa ya Shetani Ibilisi, kwa maana wakati wote huo amekuwa akijikaza kudanganya dunia yote inayokaliwa na watu. Roho iliyoongoza kuandikwa kwa Biblia haikuwa roho inayoendesha taratibu ya rnambo ya zamani iliyopo. Lakini kwa habari ya namna ya watu walioandika na roho iliyowaongoza kuandika, acheni tuangalie usemi mfupi wa mtume Petro, aliyefia Ukristo wa kweli:
4 “Walakini nitajitahidi, kwamba kila baada ya kufariki kwangu [kuuawa kwa ajili ya imani] mpate kuyakumbuka mambo hayo. Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Na sauti hiyo sisi tulisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.
5 “Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing’aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na [roho takatifu].”—2 Pet. 1:15-21.
6. Petro anapotaja kugeuka kwa Kristo huo unakuwa ushuhuda wa nini, na ni nini kilichofanya barua zake mbili ziwe zimeongozwa na Mungu?
6 Petro mwenyewe akawa mmoja wa watu hao walioandika na kunena yaliyotoka kwa Mungu ‘wakiongozwa na roho takatifu.’ Kwa sababu hiyo, Petro alitoa ushuhuda mwaminifu juu ya mambo ambayo yeye na mitume Yakobo na Yohana waliona na kusikia wao wenyewe wakati Yesu Kristo alipogeuka mbele yao wakiwa juu ya mlima mrefu Palestina. Wanafunzi wengine watatu wa Kristo wanaandika habari za kugeuka huko kwa Yesu Kristo miezi kadha kabla hajauawa kwa jeuri nje ya kuta za Yerusalemu. (Mt. 17:1-9; Marko 9:2-9; Luka 9:28-36) Kwa hiyo ushuhuda wa Petro unaungwa mkono na watu wenye kutumainika. Katika Biblia barua mbili zenye jina lake ziliandikwa naye, mwanadamu; lakini hiyo haikufanya barua hizo zake ziwe maandiko ya kutungwa na mwanadamu tu. Barua za Petro ziliongozwa. na roho takatifu. Kwa hiyo ziliongozwa na Yehova Mungu. Chanzo cha roho takatifu.
7. Katika 2 Petro 3:15, 16, Petro alionyeshaje kwamba alihesabu maandiko ya Paulo kuwa sehemu ya Biblia iliyoongozwa na Mungu?
7 Katika barua yake ya pili Petro aonyesha maandiko ya mtume Paulo ni sehemu ya maandiko ya Biblia yaliyoongozwa na Mungu. Petro alisema: “Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.” (1 Pet. 3:15, 16) Leo wako wenye lawama wanaobisha kwamba mwanadamu dhaifu (Paulo) aliandika barua hizo, kwa hiyo wanabisha kwamba zimetungwa na mwanadamu. Wenye lawama hao wanapotoa Maandiko, “kwa uvunjifu wao wenyewe.”
8. Kwa habari ya Maandiko yaliyoandikwa na watu walionena na kuandika yaliyotoka kwa Mungu, Paulo alisema nini katika 2 Timotheo 3:16, 17?
8 Kwa habari ya Maandiko Matakatifu yaliyoandikwa na wanadamu walioandika na kunena yaliyotoka kwa Mungu, mtume Paulo alisema haya: “Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu [kwa halisi, Mungu alipulizia pumzi (the opneustos)], na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; ili mutu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo jema.”—2 Tim. 3:16, 17, ZSB; Kingdom Interlinear.
9. Kwa kutaja-taja maneno ya Maandiko hayo, Paulo aliweza kuhakikisha msingi wa Ukristo ni msingi gani?
9 Paulo mwenyewe alikuwa namna hiyo ya “mutu wa Mungu” aliye hodari. Aliyafahamu sana Maandiko ya Kiebrania ya kale. Kwa kutaja taja yaliyoandikwa katika Maandiko hayo yaliyoongozwa na Mungu Paulo aliweza kuhakikisha Ukristo wa kweli ulipewa na Mungu.—Matendo 17:3.
10. Kwa sababu gani unabii mbalimbali wa Biblia umeendelea kutimia mpaka sasa, ingawa wanadamu hawakujua namna Mungu angeutimiza?
10 Kuna sababu ya kuendelea kutimia kwa unabii mbalimbali uliomo katika Biblia, hata katika karne yetu ya 20. Sababu ni kwamba unabii huo si matabiri ya wanadamu dhaifu wanaojaribu kufanya tafsiri zao wenyewe juu ya namna mambo ya ulimwengu yatavyokuwa. Bali, kanuni za Biblia zimetoka kwa Mungu, naye alizitoa kupitia kwa wanadamu waliokuwa wamejitoa Kwake. Mungu hutimiza unabii wake ingawa wanadamu hawajui hasa namna Mungu anavyofanya hivyo. Jambo hilo lilikaziwa na Petro, wakati alipoambia kundi la Wayahudi katika, hekalu katika Yerusalemu hivi: “Mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo . . . ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu.” (Matendo 3:18-21) Biblia imeandika unabii wa Mungu asiyesema uongo, ingawa alinena kupitia kwa manabii.
11. Alipokuwa akihutubia kundi la wanafunzi 120 katika Yerusalemu, Petro alikaziaje kwamba unabii mbalimbali wa Mungu ulipaswa kutimia?
11 Kwa sababu unabii wa Biblia unatokana na Mungu kupitia kwa roho takatifu yake umetimia. Petro aliendelea kutaja jambo hilo alipoliambia kundi la karibu wanafunzi 120 wa Kristo katika Yerusalemu hivi: “Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, [ililolinena roho takatifu] zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda, aliyewaongoza wao waliokamata Yesu.”—Matendo 1:15, 16.
12. Petro na wanafunzi wengine waliunganaje katika sala wakaonyesha Zaburi 2:1 iliyoandikwa na’ Daudi ilipaswa kutimia?
12 Baadaye, Petro alijiunga na wanafunzi wenzake katika sala iliyokazia namna unabii, mwingine uliotolewa na Daudi ulivyotimia. Matendo 4:24, 25 lasema: “Wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; nawe ulinena kwa [roho takatifu] kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona, mataifa wamefanya ghasia, na makabila wametafakari ubatili?” (Zab. 2:1) Hivyo Wakristo hao wa karne ya kwanza walijua kwamba Maandiko ya Kiebrania yaliyo matakatifu yaliandikwa kwa uongozi wa roho takatifu ya Mungu iliyotenda kazi juu ya watu wa zamani.
13. (a) Kulingana na 2 Samweli 23:1-3, ni nani alive-paswa kusifiwa kwa sababu ya sehemu za Maandiko ya Kiebrania zilizotungwa na Daudi aliyetiwa mafuta? (b) Ni mambo gani yaliyofanya unabii mbalimbali uliotolewa kupitia kwa Daudi utimie?
13 Kwa kuwa mtunga zaburi Daudi hapa atajwa jina waziwazi, twaweza kuuliza: Alijisikiaje akisema na kuandika mambo yaliyofanywa kuwa sehemu ya Maandiko ya Kiebrania yaliyo matakatifu? Hajisifu kwa maandiko yake, ambayo yamehifadhiwa kuwa yenye ubora mwingi sana hata kwetu leo. Kuhakikisha hilo, haya ni maandishi yanayohusu mfalme huyo aliyetiwa mafuta wa Israeli wote, yaliyohifadhiwa kwa ajili yetu katika 2 Samweli 23:1-3 “Basi haya ndiyo maneno ya mwisho ya Daudi. Daudi, mwana wa Yese, anena, Anena huyo mtu aliyeinuliwa jua yeye, masihi wake Mungu wa Yakobo, mtungaji wa nyimbo za Israeli mwenye kupendeza; Roho ya [Yehova] ilinena ndani yangu, na neno lake likawa ulimini mwangu. Mungu wa Israeli alisema, Mwamba wa Israeli aliniambia.” Kwa hiyo yaliyofanya unabii mbalimbali kupitia kwa Daudi utimie hayakuwa busara yake ya kuona yasiyotokea wala haukuweza uwezo wake kufanya tafsiri yake mwenyewe juu ya mambo. Roho ya Mungu iliyokuwa ikitenda kazi juu ya Daudi na maongozi ya Mungu ndiyo yaliyotimiza hayo.
14. Zaidi ya Daudi, Isaya na Yeremia walionyeshaje kwamba sehemu zao zilizoandikwa katika Maandiko hawakuzitunga wao wenyewe?
14 Daudi siye peke yake anayekubali kwamba sehemu zake zilizoandikwa katika Biblia Takatifu hayakutungwa naye mwenyewe. Manabii wengine, ambao vitabu vyao vilivyoongozwa na Mungu vimehifadhiwa katika Biblia, wanakubali kwa unyofu kwamba neno la Yehova Mungu ndilo lililowajia. Kwa, mfano, Isaya afungua kitabu chake kikubwa cha unabii kwa kusema: “Haya ni maono ya Isaya, mwana wa Amozi, aliyoyaona katika habari za Yuda na Yerusalemu, siku za Uzia na Yothamu na Hezekia, wafalme wa Yuda. Sikieni, enyi mbingu, tega sikio, Ee nchi, kwa maana [Yehova] amenena.” (Isa. 1:1, 2) Yeremia aanza kitabu chake kikubwa cha unabii, akisema: “Maneno ya Yeremia, mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani waliokuwa katika Anathothi, katika nchi ya Benjamini; ambaye neno la [Yehova] lilimjia katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa kumiliki kwake.”—Yer. 1:1, 2.
—Kutoka Holy Spirit—the Force Behind the Coming New Order sura ya 4.