Je! Imani Inaweza Kushinda katika Ulimwengu wa Leo?
KUSUDI linalothawabisha maishani. Kijana huyu mwanamume hakuwa nalo. Kama vile alivyokubali mwenyewe, yeye alikuwa “mfanya matata tangu alipokuwa na umri wa miaka 12,” Kwa sababu ya kutumia sana dawa za kulevya hakuweza kushindana na matatizo (magumu) “ya ulimwengu yasiyotatulika,” anakubali hivi: “Niligeukia ulaji wa kujilazimisha. Katika Januari wa mwaka 1977 nilitaka kujiua. Nilikataa kuendelea kuishi namna hii. Kila nukta iliumiza.”
Miezi michache baadaye, kijana huyu huyu mwanamume alipata furaha na kusudi maishani linalothawabisha. Kwa sababu gani? Ni kitu gani kilicholeta badiliko hili? Imani!
Bila shaka maisha ya jamaa yenye furaha hayakufurahiwa na mwanamume mmoja na mkewe pamoja na watoto wao aliyekuwa akifanya kazi ya kibarua ya shambani, walioishi katika nchi ya mashariki (Asia). Baba huyo hakutoa riziki ya kutosha naye alitumia sehemu kubwa ya fedha zake kununua tumbako, vileo na popoo. Yeye na jamaa yake waliishi katika hali yenye kusikitisha, hawakuvikwa vya kutosha na mara nyingi waliona njaa.
Walakini mwanamume huyo alianza kubadilika. Yeye akaacha kulewa, akabadilisha tabia zake kazini akapata malipo bora. Kwa muda wa miezi michache tu alisafisha nyumba yake akaleta maendeleo. Kisha jamaa yake ililishwa na kuvikwa, hiyo ikatokeza furaha.
Ni kitu gani kilicholeta maisha yenye furaha ya jamaa? Ni imani mpya liliyopatikana!
Badiliko la utu kuwa mwema lilihitajiwa sana na msichana mmoja wa miaka 16 wa nchi ya Amerika ya Kusini. Katika maneno yake mwenyewe, yeye aliasi kila kitu ‘kilichohusiana na mamlaka.’ Msichana huyu hata alishiriki katika usafirishaji ulio marufuku wa bidhaa kutoka na kuingia nchini mwao. Kama vile yeye mwenyewe alivyosema, ‘Nilikuwa mwasi asiye na sababu.’
Hata hivyo, msichana huyu aliweza kufanya badiliko la utu, na kuacha matendo yake ya uasi wa sheria. Hii iliwezekanaje? Yeye alikuwa amepata imani yenye msingi wa Biblia.
Udugu na umoja si mambo ya kawaida katika ulimwengu wa leo. Sana sana vita vimeharibu sana roho hii. Walakini yafikirie maono ya wanaume wanne—mabaharia watatu Wakanada na Mjeremani mmoja afisa mpiga mizinga katika meli ya kivita. Pindi moja wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Wakandada hao walijaribu kuzamisha meli ya afisa huyo. Miaka thelathini na minne baadaye Wakanada hao ambao hapo zamani walikuwa mabaharia waliungana. Wazia mshangao wao walipofahamu kwamba wakati fulani katika muda huo wa miaka thelathini na minne, adui yao ya wakati wa vita alikuwa amekuwa ndugu yao wa kiroho, na hata akambatiza mmoja wao kuwa Mkristo!
Kwa hiyo, basi, je! imani inaweza kushinda katika ulimwengu wa leo? Inashinda. Wengi waliokosa tumaini wakati mmoja, sasa wana kusudi maishani linalowathawabisha. Mababa, akina mama na watoto waliokosa furaha hapo kwanza wanafurahia maisha ya jamaa yenye furaha wakati huu. Watu wengi waliopata kuona kwamba nia na mwenendo wao ulikuwa mbaya wakati mmoja wamefanya mabadiliko ya utu ukawa mwema. Nao waliopata kuwa maadui hapo zamani wamefungamanishwa pamoja katika vifungo visivyovunjika vya udugu na umoja.
Sana sana ni kitu gani ambacho kimeleta matukio haya mema? Ni imani ishindayo! Kwa kweli, mambo hayo yaliyoonwa yalisimuliwa katika “Imani Ishindayo” Makusanyiko ya Mataifa Yote ya Mashahidi wa Yehova yaliyofanywa hivi karibuni katika sehemu mbalimbali. Mengine ya makusanyiko haya yamesimuliwa katika habari ifuatayo.