Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 8/1 kur. 4-11
  • Kukusanyika kwa Kusudi la Kuendeleza Imani Ishindayo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukusanyika kwa Kusudi la Kuendeleza Imani Ishindayo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • IMANI INAPATA NJIA
  • WALISHINDA KWA IMANI
  • JAMAA ZENYE FURAHA NA ZENYE IMANI ISHINDAYO
  • IMANI ISHINDAYO KATI YA VIJANA
  • TAYARI FAIDA ZINAONEKANA WAZI
  • IMANI ISHINDAYO INAENDELEZA UDUGU
  • “TANGAZO LA IMANI YETU”
  • IMANI ISHINDAYO INATAKA MATENDO!
  • WANAENDELEA KUJENGA IMANI ISHINDAYO
  • Namna Imani Ishindayo Inavyoweza Kukuhusu Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Endeleeni ‘Kusimama Imara Katika Imani’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 8/1 kur. 4-11

Kukusanyika kwa Kusudi la Kuendeleza Imani Ishindayo

KUNA Wakristo hodari zaidi wa 2,000,000 ambao wamesimama imara katikati ya matatizo (magumu) yanayopata ulimwengu wa leo. Tena, uhakika wa kwamba mfuatano wa makusanyiko yao ya mataifa yote zaidi ya 100 ambayo yataleta pamoja zaidi ya watu 2,000,000 unafanya watu hawa kuwa tamasha mbele ya mataifa na watu mmoja mmoja. Nacho kichwa cha makusanyiko haya ya Kikristo “Imani Ishindayo” kinasisimua kweli kweli.

Katika siku ya kwanza ya kusanyiko, hotuba ya kufungua imekuwa ikikaza fikira juu ya maneno haya: “Huku ndiko kushinda kushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.” (1 Yohana 5:4) Msemaji aliuliza, “Ushindi huu kwa imani ni ushindi wa namna gani,” kisha akajibu hivi: “Basi, kuwa na imani maana yake ni kusadiki kabisa kabisa mambo yasiyoonekana bado au mambo ya wakati ujao hata mambo hayo yanakuwa hakika kwa anayeamini. Imani ya kweli ya Kikristo ambayo imejengwa juu ya msingi hakika wa Yesu Kristo, ni tofauti kabisa na imani isiyo na msingi iliyojengwa juu ya maono ya moyoni yanayobadilika au ushirikina. Kama vile ‘dhahabu, fedha na mawe ya thamani’ [imani ya kweli] haiwezi kuharibika.” (1 Kor. 3:11-14) Lakini imani hii inajidhihirishaje?

IMANI INAPATA NJIA

Kwa wengine, kuhudhuria tu mojawapo ya haya makusanyiko kulileta jaribu la imani. Kwa mfano: Roho ya imani ishindayo ilikuwa ndani ya maelezo haya ya mwanamke mmoja wa kutoka United States aliyehudhuria kusanyiko katika Montreal, Quebec, Canada. Yeye huhitaji uaguzi wa kuchuja (kusafisha) umaji-maji wa figo zake baada ya kila siku moja. Kwa kuwa hana chombo kinachoweza kubebwa, (cha kufanya kazi hiyo) ingemlazimu yeye kwenda hospitalini katika mji huo kwa kila uaguzi. Je! hii ingemzuia? Hapana! Yeye alisema: “Sitaacha kajambo kadogo kama hako kanizuie!” Na hakakumzuia.

Vilevile imani ishindayo ilionyeshwa wakati jamaa kubwa kutoka sehemu ya kaskazini ya United States ilipohudhuria kusanyiko la Montreal, Canada. Moto ulikuwa umeteketeza nyumba yao, na walikuwa wamekuwa wakiishi katika bas la shule lililogeuzwa kuwa mahali pa kulala. Mama wa jamaa hiyo, Mkristo aliyebatizwa karibuni, alikuwa na nia hii “Yehova atatoa msaada.” Sehemu kubwa ya akiba ndogo ya jamaa hii ilitumiwa kutengenezesha gari ili liweze kusafiri, lakini mtambo wake uliharibika karibu na Montreal wakalazimika kulipa gharama kubwa gari lilipokokotwa mpaka Mji wa kusanyiko wa magari yaliyokokotwa nyuma ya magari mengine. Mashahidi wenzao walijitolea kulipa nusu ya gharama ya kukokotwa kwa gari hilo, na walipofahamu kwamba mtambo wa gari lao usingeweza kutengenezwa upya, walifanyia jamaa hiyo mpango wa kusafiri kurudi nyumbani kwao pamoja na rafiki wengine. Vilevile wakaaji wa Mji wa magari yaliyokokotwa nyuma ya mengine walitoa mchango wa kutosha kuwezesha jamaa hiyo kununua gari jingine kama hilo wakirudi kwao. Baba mwenyewe, akiwa hajabatizwa bado, alishangazwa sana na ukarimu huu wa kujitolea hata akalia, akisema kwamba kwa kweli alikuwa akijionea upendo aliokuwa amesoma juu yake katika vitabu vya Mashahidi wa Yehova.​—⁠Yohana 13:34, 35.

Kati ya maelfu ya waliohudhuria “Imani Ishindayo” Makusanyiko ya Mataifa Yote katika New Orleans (U.S.A.) alikuwako dada mmoja aliyeolewa ambaye alikuwa huko “peke yake” pamoja na mtoto wake wa miaka minne na kitoto cha miezi sita. “Katika jamaa yangu hakuna mtu aliyemo katika kweli,” ndivyo anavyoandika, “na nilipokuwa huko Superdome nilijisikia kama kwamba nilikuwa katika mahali palipo na chemchemi. Nilijua kwamba ningalilifurahai na nilitazamia liwe lenye kupendeza, lakini sikujua furaha iliyoningojea kwa kuwa pamoja na ndugu na dada hao wote.” Vilevile muziki uliorekodiwa kipekee ulivutia sana. “Wimbo wa kwanza ulipoimbwa,” anasema, “Sikuweza kuuimba wote kwa kuwa nilikuwa ninalia kwa furaha.”

WALISHINDA KWA IMANI

Hao wasikilizaji wengi wa makusanyiko hayo wanatia ndani watu wengi waliokuwa wameshinda kwa imani hivi karibuni tu. Namna gani? Kwa kuacha njia za kilimwengu, kuweka maisha zao wakf kwa Yehova Mungu kupitia kwa Yesu Kristo, na kubatizwa katika maji. Kati ya watu 785,051 waliohudhuria yale makusanyiko 20 ya mataifa yote katika United States, watu 5,539 walibatizwa. Kwa msaada wa roho takatifu ya Mungu, wengine wao walikuwa wamefanya mabadiliko makubwa ya utu.​—⁠Kol. 3:8-10.

Kwa mfano, mwanamume mmoja na mkewe walikuwa wakitumia dawa za kulevya wakati mwanamke huyo alipoanza kujifunza Biblia katika mwaka 1974. Wakati huku mumewe akiendelea na huo mwenendo wa maisha, ‘mke alichagua njia ya Yehova.’ Katika mwaka 1976 mwanamume huyu alipewa na serikali ruhusa ya kufanya talaka, lakini katika mwaka 1977 yeye alipoteza mali zake zote za kidunia. Ndipo alipokumbuka yale ambayo mkewe alikuwa amesema juu ya “siku za mwisho.” (2 Tim. 3:1-5) Baada ya kushirikiana na dini nyingi za Jumuiya ya Wakristo, yeye alipata uhakika kwamba hawakuwa wakifundisha kweli ya Biblia. Basi mwanamume huyo alimwomba Mungu amwonyeshe dini ya kweli na amwezeshe kupata amani ya akili. Siku moja alipata anwani ya Jumba la Ufalme la mahali hapo naye anakumbuka hivi:

“Nilikwenda hapo usiku huo na kupata Biblia bure kutoka kwa ndugu mmoja, ijapokuwa nilijitolea niilipie. Sura yangu ilikuwa imemhakikishia kwamba nilihitaji Biblia, kwa kuwa nywele zangu zilifika mpaka kiunoni mwangu. Nilianza kuisoma usiku huo na baada ya muda mfupi, nilifahamu kwamba sikuifahamu. Kwa hiyo nikarudi tena kwa msaada zaidi, nikapata kitabu Kweli [Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele], nikaambiwa kwamba ndugu fulani angejifunza pamoja nami. Nilikubali kwa furaha.

“Tangu wakati huo, mimi na mke wangu wa zamani tumeona tena (Julai 1, 1978) na tukawa na pendeleo la kuhudhuria Kusanyiko la “Imani Ishindayo” pamoja na wana wangu, wenye umri wa miaka 16 na 14, ambapo nilibatizwa [Julai 22].”

JAMAA ZENYE FURAHA NA ZENYE IMANI ISHINDAYO

Hii si imani isiyotenda​—⁠kuamini tu kitu fulani cha kiroho​—⁠kinachounganisha tena wenzi wa ndoa waliotengana. Kinachohitajiwa ni imani yenye nguvu​—⁠ndiyo, imani ishindayo. Katika siku ambazo ndoa zinavunjika na jamaa kutengana, imani hiyo inashinda. Inatokeza maisha yenye furaha ya jamaa.

Sehemu kubwa ya wahudhuriaji wanaokusanyika katika “Imani Ishindayo” Makusanyiko ya Mataifa Yote ni washiriki wa jamaa za Kikristo zinazoongozwa na Neno la Mungu, Biblia. Jambo la kuvutia ni kwamba katika mojawapo ya miji ya makusanyiko naibu wa meya (mkuu wa mji) alisema hivi: “Jambo linalostahili kuangaliwa ni vile mnavyojali sana maisha ya jamaa na njia yenu ya maisha iongozayo kwenye haki. Hili ni jambo ninalopendezwa nalo nami nafurahi kuona mkitenda jambo fulani kuhusiana nalo.”

Kwa kufaa, siku ya nne ya makusanyiko haya ya mataifa yote ina kichwa “Uwe na Imani ya Kuokoa Nyumba Yako.” (Ebr. 11:7) Hotuba yenye kichwa “Kupambana na Matatizo ya Ndoa Katika Ulimwengu Huu wa Kisasa” inaonyesha waziwazi kwamba mara nyingi uchoyo wa mtu binafsi ndio chanzo cha magumu ya ndoa. Hata hivyo, kwa kusitawisha sifa za Kikristo inawezekana waume wawe wanaume wa Mungu na wake wawe wanawake wa Mungu. Mambo mbalimbali yaliyoko kwenye programu yanaonyesha pasipo shaka kwamba​—⁠kwa kutumia imani ishindayo​—⁠inawezekana kufanya maisha ya jamaa yako yawe yenye furaha.

Hata hivyo, ili kupata furaha katika ndoa huenda marekebisho fulani yakatakiwa. Kwa mfano, katika masimulizi ya jambo lililoonwa katika kusanyiko la mataifa yote katika Winnipeg, Manitoba, Canada, mwanamume mmoja alikubali hivi: “Nami vilevile niliona vigumu kukubali ukichwa, kwa kuwa ilikuwa rahisi zaidi kwa [mke wangu] kuchukua uongozi, Walakini hii imewezekana baada ya muda fulani.”​—⁠Efe. 5:21-23, 33.

Lo! namna ilivyo furaha kuona jamaa nzima zikionyesha waziwazi imani ishindayo katika ulimwengu wa leo! Kwa kweli inafaa kuangalia jamaa kubwa sana iliyohudhuria kusanyiko la mataifa yote la lugha ya Kispania katika Los Angeles, California (U.S.A.). Jamaa hiyo ilianza kupata kweli ya Biblia katika mwaka 1917 babu yao alipoanza kusoma vitabu vya watu wa Mungu. Miaka mingi baadaye nyanya yao mjane alihamia nchi ya Mexico na kuanza kujifunza Biblia pamoja na watangazaji wa Ufalme wa wakati wote katika nchi hiyo. Watoto wake 12 wa kiume na wa kike walitakiwa kushiriki kwa kusoma kitabu na kutoa maelezo juu yake. Leo kuna zaidi ya washiriki wa jamaa hiyo 150 wanaoonyesha imani ishindayo, kati yao kuna wazee, watumishi wa huduma na mapainia (watangazaji wa “habari njema” wa wakati wote). Kwa kweli, washiriki 106 wa jamaa hiyo walihudhuria kusanyiko la lugha ya Kispania katika Los Angeles.

IMANI ISHINDAYO KATI YA VIJANA

Ikiwa maisha ya jamaa yenye furaha yatapatikana lazima watoto na vijana wafikiriwe. Kwa kufaa, basi, siku nzima kabisa ya kusanyiko imewekwa kwa ajili ya kichwa “Enyi Vijana, Mwe Vielelezo katika Imani.” (l Tim. 4:12) Katika programu ya siku hii kuna mchezo wa kuigiza unaotia imani nguvu “Vijana​—⁠Mradi Wenu Maishani ni Nini?” Unahusu imani na utumishi wa kimungu usio na choyo wa mwamume kijana Timotheo, mwenzi wa mtume Mkristo Paulo.

Ndugu watatu wa kimwili walikuwa kati ya waliokuwa wakishiriki katika mchezo huu kuigiza katika Kusanyiko la Mataifa Yote la “Imani Ishindayo” huko Milwaukee, Wisconsin, (U.S.A.). Wote walikubali kwamba wakati wa kujaribu zaidi na kutia imani yao nguvu uliletwa na kifo cha baba yao baada ya kupatwa na ugonjwa wa ghafula.” Ni kitu gani kilichosaidia vijana hawa wawe na imani ishindayo? Mmoja wao, Lawrence, alijibu hivi: “Imani imetuweka pamoja kama jamaa. Baba yetu alipokuwa hai, alikuwa mwangalifu sana kwetu. Alikuwa akitukusanya pamoja sisi vijana na kutuambia mambo juu ya maisha.” “Na wakati wote yeye alitutia moyo tuendelee kusonga mbele,” akaongezea Lester, mwenye umri wa miaka 17. Vilevile alisema hivi: “Mama aliendelea tu katika nyayo za [baba] akaongoza jamaa iendelee mbele katika imani.” Leon, mwenye umri wa miaka 20, aliyecheza sehemu ya Timotheo katika mchezo huo wa kuigiza, alisema hivi: “Wazee [wa kundi], walioshirikiana nasi na kutualika katika utimishi wa shambani, walitusaidia kudumisha imani yetu yenye nguvu.” Ndiyo, vijana Wakristo wana imani inayoshinda katika ulimwengu wa leo.

TAYARI FAIDA ZINAONEKANA WAZI

Makusanyiko haya ya mataifa yote yametayarishwa kwa kusudi la kuendeleza imani ishindayo. Mpaka sasa, wale wanaolifuata Neno la Mungu tayari wanatoa ushuhuda kwamba wamefaidika kutokana na mashauri yake. Mtu mmoja mwenye hoteli kandokando ya barabara katika eneo la San Fransisco, California, (U.S.A.) alisema hivi: “Nilifurahi kuwa na Mashahidi wa Yehova wakikaa mahali pangu na kupajaza. Nataka kusema, watoto wenu wana tabia njema sana. Wao hawachezi na mashine za barafu, kucheza-cheza na mashine za kupandisha watu au kukimbia-kimbia mapitoni ya jumba kama wafanyavyo watoto kila mara.”

San Juan, Peurto Rico, vilevile ulikuwa mji ambamo Mashahidi wa Yehova walikutanika kwa makusanyiko ya mataifa yote. Huko msimamizi mmoja wa hoteli alisema: “Sana sana nimefurahishwa na watoto wenu. Sisi hatusumbuliwi nao hata kidogo na wanajiendesha vizuri sana. Ijapokuwa kweli kwamba kuna zaidi ya Mashahidi wa Yehova 200 wakiwa wageni katika hoteli hii, kuna kimya sana. Ningetaka kwamba [wote] wanaokaa hapa wawe Mashahidi wa Yehova. Sijawahi kuona jambo kama hilo tena kwamba watoto wengi hivyo na watu wazima wangeweza kuwa na umoja na unyenyekevu hivyo.”

Mwanamume mmoja ambaye amekuwa mlinzi wa usalama kwa miaka tita katika uwanja mmoja ambao hutumiwa na Mashahidi wa Yehova katika San Juan, alisema hivi: “Mimi huona kwamba matayarisho yenyewe ni ya ajabu sana. . . mimi siwi na wasiwasi. Sitatizwi nanyi. Tazama, mimi hata sibebi fimbo. Lakini katika yale makusanyiko mengine ya kidini sivyo ilivyo. Ninyi huniheshimu sana. . . . Hata watoto wananitii! Jambo hilo halitukii kamwe!”

IMANI ISHINDAYO INAENDELEZA UDUGU

Makusanyiko haya ya Mashahidi wa Yehova yamevuta sana fikira. Jambo moja lililowezesha hilo ni roho iliyoonekana pote ya udugu na umoja. Kwa mfano, akiandika katika gazeti The Times​—⁠Picayune, Wesley Jackson aliwaeleza Mashahidi kuwa “watu wema, wenye maisha yenye adili za juu sana ambayo huwawezesha kufikiria sana hali ya jamaa.” Vilevile alisema hivi: “Maelfu wengi ya Mashahidi hapa juma hili, wakiwa wa kadiri mbalimbali za ukubwa na umbo, rangi na mataifa tofauti, kwa msingi wao ni Wakristo waliojitoa sana. Ambao imani yao ya kidini inatofautiana na ile ya jamii nyingine yote ya Kikristo. Kwamba wao wana ushirikia wa karibu sana inaonyeshwa wazi na wengi sana ambao wamekutana katika mji huu kwa mkutano wa kwanza wa mikutano miwili ya mataifa yote inayofanyiwa hapa New Orleans, [U.S.A.].”

Vilevile roho ya udugu na umoja inayoonekana waziwazi kati ya Mashahidi wa Yehova ilitajwa katika habari ya mhariri iliyoandikwa katika gazeti Washington Afro-American la Juni 24, 1978. Ilisema hivi:

“Ingawa maendeleo mengi yamefanywa katika kuendeleza uhusiano wa mataifa yote, wachunguzi wengine wameona sababu za kuvunja moyo hivi karibuni. Kadirio lao: [Kuna] weusi na weupe wachache sana wanaokaa pamoja kanisani.

“Wakati wa vipindi vya ‘Imani Ishindayo’ Kusanyiko la Mataifa Yote la Mashahidi wa Yehova inaonekana wazi kwamba hakuna mgawanyiko kama huo. Wahudhuriaji 48,000 wa mkutano unaoendelea katika R.F.K. Stadium wanakula, kaubudu, na kushirikiana pamoja pasipo tofauti za kijamii.”

Wakitambua kwamba Mungu “alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika [mtu] mmoja,” Mashahidi wa Yehova wana umoja ulimwenguni pote. (Matendo 17:26) Kama vile mtume Petro, wao wanafahamu kwamba “Mungu hana upendeleo, bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34, 35) Kwa hiyo, migawanyiko ya kijamii, kitaifa na mingineyo inapoendelea kuvunja jamii ya kibinadamu, “Imani Ishindayo” Makusanyiko ya Mataifa Yote yanashuhudia kwamba kuna watu wenye umoja wanaoonyesha imani isiyoshindika.

“TANGAZO LA IMANI YETU”

Bila shaka, imani ishindayo imekaziwa katika haya makusanyiko ya mataifa yote. Kwa mfano, hotuba ya watu wote ilikazia imani iongezwe katika Yehova Mungu na Mfalme wake wa Kimasihi. Hotuba hiyo, yenye kichwa “Yesu Kristo​—⁠Mfalme Mshindi Atakayepambana na Mataifa,” ilionyesha waziwazi kwamba Mwana wa Mungu ni mfalme mpiga-vita ambaye lazima apande farasi apiganie kweli, unyenyekevu na haki na kupigana kwa ajili ya kusimamishwa kwa taratibu mpya juu ya dunia yote.​—⁠Zab. 45:3-5; Isa. 26:9.

Hivyo, makusanyiko ya mataifa yote yalipokuwa yakiendelea duniani pote, Lo! namna ilivyofaa kwamba Mashahidi wa Yehova wapaswa watoe “Tangazo la Imani” Yao! Wamekuwa wakifanya hivyo katika kila kusanyiko. Wakristo hawa wenye imani ishindayo wanaonyesha furaha yao kwa kuwa sehemu ya udugu wa pekee wa kweli wa mataifa yote duniani pote. Wao wanaonyesha nia yao ya kutaka kusonga mbele katika utumishi wa Mungu Aliye Juu Zaidi, Yehova, na kutoa tangazo la ujumbe wa Ufalme mpaka mwisho wa taratibu ya mambo. Tena, wana nia ya kutokumwacha kamwe Yule ambaye amewafanyia mengi sana na kuwapa kusudi maishani.

IMANI ISHINDAYO INATAKA MATENDO!

Walakini, itikio la imani ni jambo moja. Kuionyesha katika matendo ni jambo jingine. (Yak. 2:18-20) Asubuhi ya Ijumaa ya “Imani Ishindayo” Kusanyiko la Mataifa Yote imetolewa kwa ajili ya utendaji wa shambani. Wakiwa na vitabu vinavyobebewa katika mifuko maridadi inayolitangaza kusanyiko, wahudhuriaji wanatoa ushuhuda nyumba kwa nyumba, sehemu za biashara, barabarani kuu za mjini na kwingineko. Kwa mfano, zaidi ya Mashahidi 20,000 walishiriki utendaji huu katika Philadelphia, Pennsylvania, (U.S.A.) na katika ujirani wake. Huko New Orleans, Louisiana, (U.S.A.) zaidi ya wahudhuriaji 30,000 waliishiriki kazi hiyo.

Katika sehemu mbalimbali, wafanya kazi wa television au wa njia nyinginezo za kueneza habari wamefuatana na Mashahidi katika utendaji wao wa shambani Ijumaa asubuhi. Cheryl Ernst, mwandikaji wa gazeti Everett Herald, aliandika katika gazeti hilo la jambo la Washington hivi: “Wao walisafiri kwa miguu kutoka Kingdome [Seattle] watu 40,000, kama vile jeshi [la kivita] la Yoshua . . . Imani ilikuwa ndiyo wazi lao la kivita, Biblia ndiyo silaha na maneno yao ndiyo risasi zao.”

Utendaji huu wa pekee ulileta matokeo gani? Katika St. Louis, Missouri, (U.S.A.), mwanamume mmoja alimjia Shahidi akifanya kazi katika barabara kuu za mji na kusema: “Mimi nitasema jambo moja juu ya Mashahidi wa Yehova: Wanawake wenu wanavalia kama wanawake waungwana.” Donna Balkan, mwandishi wa gazeti la Ottawa, Ontario, Citizen, aliandika hivi: “Hata wasioamini walio washupavu sana wanavutwa na mwenendo wa kirafiki, na wenye kupendeza wa wahudhuriaji. Majaribio ya kubishana nao yalishindwa kwa maneno ya upole​—⁠ingawaje, si rahisi kubishana na watu wanaozungumza wakati wote juu ya upendo, amani, na ‘hali bora ya maisha’ ambayo Ufalme wa Mungu utaletea jamii ya kibinadamu.”‏

WANAENDELEA KUJENGA IMANI ISHINDAYO

Mashahidi wa Yehova wanangojea kwa uhakika “hali bora ya maisha” na baraka nyingine ambazo ufalme wa Mungu utaletea wanadamu. Hata hivyo, tayari ibada ya Yehova Mungu na utumishi wa kujitoa kwake umewapa kusudi maishani linalowathawabisha. Vilevile, kwa sababu ya kutumia kanuni za Maandiko, sasa wao wanafurahia maisha ya jamaa yenye furaha na wanapata uradhi utokezwao na mabadiliko ya utu ambayo hupatana na mapenzi ya Mungu. Nao Wakristo hawa wanafurahi kwamba udugu na umoja wa kweli unawafungamanisha pamoja katika ulimwengu huu uliogawanyika.

Ndiyo, Mashahidi wa Yehova wanatoa uthibitisho kwamba imani yaweza kushinda katika ulimwengu wa leo. Hata hivyo, wao wanafahamu kwamba kuendelea kujenga imani ni jambo la maana sana, nayo makusanyiko yao ya wakati huu yanawafaidi na kuwasaidia kufanya hivyo. Jamaa moja ya wale waliohudhuria ililisema vizuri jambo hilo kwa kuandika hivi: “Akina ndugu, kila mtu alitoka katika kusanyiko hili akiwa anaweza kupambana vizuri zaidi na magumu mengi tunayopata sote katika maisha ya kila siku. Asanteni kwa kazi yote mliyoifanya, na yote kwa utukuzo wa Yehova.” Kwa kweli, makusanyiko haya ya mataifa yote yanaiendeleza imani.

[Picha katika ukurasa wa 8, 9]

“Imani Ishindayo”

NI YENYE MATENDO​​—⁠kama inavyoonyeshwa na kikundi hiki chenye furaha cha watangazaji wa Ufalme pamoja na jamaa yenye umoja wanaoshiriki utendaji wa kutoa ushuhuda katika kusanyiko

Mtume Paulo amtia moyo kijana Timotheo. Michezo ya kuigiza ya Biblia yenye kufundisha inaonyeshwa katika makusanyiko yote

Waargentina wakutana na Waafrika. Katika ulimwengu huu uliogawanyika, Mashahidi wa Yehova wa mataifa yote ni washiriki wa udugu mmoja wa mataifa yote

Watu hawa wawili waliooana ambao wamebatizwa sasa hivi wameonyesha sasa hivi kwamba sasa wanaushiriki ushindi kwa imani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki