Endeleeni ‘Kusimama Imara Katika Imani’
“Kesheni, simameni imara katika imani.”—1 Kor. 16:13.
1. (a) Makusanyiko ya “Imani Ishindayo” yanawapelekea watu ujumbe gani? (b) Yesu alitetea imani ya namna gani?
IMANI ishindayo inasitawi duniani! Huo ndio ujumbe unaotolewa na “Imani Ishindayo” Kusanyiko la Mataifa Yote la Mashahidi wa Yehova lililofanywa ulimwenguni pote katika mwaka uliopita. Kwa mashahidi wa Yehova imani si kitu wanachodai kuwa nacho tu. Badala yake, lazima iwe hai, ikiambatana na matendo. Yesu alieleza matunda ya imani kama hiyo katika Mahubiri yake ya Mlimani: “Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.” Na katika usiku wa mwisho na wenye maana sana pamoja na wenzi wake wasiri Yesu alimwaambia hivi: “Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.”—Mt. 5:16; Yohane 15:8, Habari Njema kwa Watu Wote.
2. Ni kitu gani kinachoonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ‘wana’ imani?
2 Ni kweli katika nyakati hizi zenye magumu kwamba “si wote walio na imani.” (2 The. 3:2) Walakini mashahidi Wakristo wa Yehova ni wenye imani sana. Imani yetu yenye matendo ndiyo inayotuongoza tuendelee kutangaza “habari njema” waziwazi katika utumishi wa shambani. Lo! ushuhuda mzuri kama nini uliotolewa katika njia hii katika siku ya tatu ya makusanyiko haya ya mataifa yote! Imani iyo hiyo ndiyo inayotupa nguvu ya kuendelea kutoa ushuhuda, hata katika maeneo yenye magumu sana, na kusimama imara tukutanapo na majaribu na mateso makali sana. Hata inatuwezesha kufurahi katika nyakati za majaribu, tunapotazama mbele kwa hamu kubwa sana kwenye ufunuo wa Yesu Kristo katika utukufu wa Ufalme.—1 Pet. 4:12, 13.
3. (a) Sababu gani inaweza kusemwa kwamba imani yetu ni halisi? (b) Imani inapaswa kuongozaje’ wale wa zamani na wale wapya?
3 Imani yetu ni jambo halisi. Msingi wake imara ni Bwana Yesu Kristo, Kichwa cha kundi la Kikristo, ambalo washiriki wake wanatumikia wakishirikiana naye. Mtume Paulo anawaonya hawa kwa upole hivi: “Basi kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye shina na wenye kujengwa katika yeye; mmefanywa imara kwa imani, kama mlivyofundishwa; mkizidi kutoa shukrani.” (Kol. 2:6, 7) Na kama vile wale walio wa zamani katika kweli wanavyoendelea kutembea katika hii imani ishindayo, vivyo hivyo maombi yetu ni kwamba, hata na wapya, kutia na wale waliobatizwa hivi karibuni, wataimarishwa katika imani, ndiyo, wazidiwe sana na imani. Imani ndiyo inayotuchochea sisi sote ‘tukiri kwa vinywa vyetu kwa wokovu,’ na kuwaambia wengine habari njema.—Rum. 10:10.
4. (a) Imani ina uhusiano gani na mwenendo?. (b) Ni kitu gani kilichotokeza msemo “Mwenendo wenu ndio mahubiri yenu makuu”? .
4 Vilevile imani hii inawaongoza Wakristo wawe na mwenendo mwema, ambao huleta sifa kwa jina lenye themani kuu la Yehova Mungu wetu. (1 Pet. 2:12) Katika wakati wa “Imani Ishindayo” Kusanyiko, gazeti la Montreal La Presse la Julai 8 lilitaja maneno haya yanayofaa kuhusu Mashahidi wa Yehova:
“Wao wana kanuni bora sana za adili, . . . katika hali, ya mtu binafsi, wakiendeleza kanuni za jamaa, na kupinga talaka na utoaji wa mimba. Wanahangaikia sana mafundisho ya kidini ya watoto wao.”a
Mwenendo mzuri sana, ambao msingi wake ni kuthamini huku kwa kanuni za adili ulionekana waziwazi sana katika makusanyiko haya. Mtaalam mmoja kutoka Urusi, ambaye ni mleta habari za magazeti, alisikika akisema hivi katika kusanyiko la Mashahidi wa Yehova la Munich: “Mwenendo wenu ndio mahubiri yenu makuu.” Na katika mji uo huo gazeti liitwalo Munchner Merkur la Julai 25, 1978, lilisema:
“Katika Jamhuri ya Mwungano [ya Ujeremani] wao ndio walipa kodi walio waaminifu zaidi na wanaolipa bila kuchelewa. Utii wao kwa sheria unaweza kuonekana katika njia wanayoendesha magari; yao nayo na vilevile katika tarakimu za uvunjaji wa sheria. . . . Wanawatii walio na mamlaka (wazazi, waalimu, serikali). . . . Biblia iliyo msingi wa matendo yao yote, ndiyo tegemezo lao. . . . Walakini hakuna anayepaswa kuwaza kwamba Mashahidi wa Yehova ni wavivu wanaojikalia kitako na kuwaza mambo yasivyo au kwamba wao ni watu wanaojifanya watawa sana na watakatifu. Katika kazi kubwa sana ya kusafisha waliweza kusafisha viti vyote na vyoo katika [Olympic] stadium katika muda wa saa tatu tu. Uwanja huo ulionekana kana kwamba ulikuwa “umelambwa na kuwa safi.” Wao ni watendaji wanaopambana na kila hali kwa kujitolea—kwa kuwa ndivyo inavyotaka Biblia.’
5. Mathayo 7:16 limetumikaje juu ya Mashahidi wa Yehova katika kusanyiko?
5 Maneno yanayofanana na hayo yamesikiwa kuzunguka ulimwengu wote. Gazeti liitwalo Corriere della Sera la, Milan Italia, hata lilisema juu ya tofauti katika toleo lake la Agosti 7, 1978:
“Wanaungwa mkono na tengenezo lililo kamilifu sana, hata matengenezo mengine yananalionea wivu. . . . Ni jambo gani jingine linaloweza kusemwa juu ya hawa Mashahidi wa Yehova? Wamejionyesha kuwa raia wenye adabu sana, hivi kwamba mwenendo wao karibu unaonekana kuwa karipio kwa kutotenda kunakoonyeshwa mara nyingine na vikundi vingine vya Wakatoliki.”
Je! Yesu hakusema: “Mtawatambua kwa matunda yao”?—Mt. 7:16.
6. Katika miezi ya karibuni, Mashahidi wamekuwaje mfano wenye kutokeza wa Ukristo wa kweli?
6 Ni kwa sababu ya hudhurio kubwa katika makusanyiko haya kwamba mwenendo wa Mashahidi umevuta sana fikira za ulimwengu. Katika nchi tatu ambazo zimetajwa hapo’ juu, jumla ya 140,590 walikusanyika katika Montreal, Winnipeg, Vancouver na Edmonton, Canada, na 108, 901 katika Munich na Dusseldorf, Ujeremani, na 111,320 katika Milan na Rumi, Italia. Katika makusanyiko yote 68 yaliyokuwa yamemalizika kufikia Septemba, 1978, jumla hudhurio ilizidi 1,700,000. Utu wa Kikristo wa watumishi hawa wa Yehova umeonyeshwa duniani pote hivi kwamba umewafanya kuwa mfano wenye kutokeza sana wa Ukristo wa kweli.
WAKATI WA ‘KUSIMAMA IMARA’
7. Ni kwa sababu gani majaribu ya imani lazima yaongezeke katika wakati ujao?
7 Majaribu ya imani yetu yataongezeka bila shaka katika siku zilizo. mbele yetu. Kwa sababu gani? Kwa sababu, tangu kuzaliwa “ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake” katika mwaka 1914 W.K., Ibilisi “akatupwa hata nchi.” Naye anajua kwamba “ana wakati mctu.” Hivyo, ghadhabu yake juu ya watumishi wa Yehova walioko duniani inaongezeka, wale “wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu” akiwa Mfalme mwenye nguvu aketiye juu ya kiti cha enzi ambaye sasa anajitayarisha kushuhudia milele enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova. (Ufu. 12:9-12, 17) Adui mkubwa huchochea taabu na wasiwasi ulimwenguni, sana sana kwa ki la kuzuia au hata kukomesha hii ‘kazi ya kutoa ushuhuda.’ Tukiwa mashahidi wa Mungu na Kritso tunayo vita kwli kweli mikononi mwetu—ya kupigana na adui wasioonekana ambao wamejikaza waharibu imani na kazi yetu.
8. Tunawezaje kusimama imara katika imani yetu sasa?
8 Huu sio wakati wa kuwa wasiotenda au kutojali. Mtume Paulo anaonya kwa upole hivi: “Vaeni silaha kamili kutoka kwa Mungu mpate kuweza kusimama imara kushindana na hila za Ibilisi. . . .Kwa sababu hiyo vaeni silaha kamili kutoka kwa Mungu, ili mweze . . . kusimama imara. Kwa hiyo, simameni imara . . . . Na zaidi ya yote, twaeni ngao kubwa ya imani, ambayo katika hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.” (Efe. 6:11-16, NW) Mashambulio ya Ibilisi yaweza kuja wakati wo wote, yakitoka katika pande nyingi mbalimbali. Ni zipi nyingine za hila zake?
PIGO LA UASHERAT!
9. (a) Ni maongozi gani yenye kuharibu ambayo Ibilisi ametumia katika muda wote wa historia? (a) Kwa hiyo, Yuda anawashaurije Wakristo?
9 Tangu siku za mwanzo-mwanzo wa historia ya wanadamu, Ibilisi ametumia uasherati kama njia ya kuwapotoza wanadamu. (Mwa. 6:2-5; 18:20; Hes. 25:1-3) Namna ya ngono zilizopotoka ilenea pote katika siku za mwanzo-mwanzo wa Ukristo, hata ikawa hatari kubwa kwa usafi wa kundi. Kwa hiyo, Yuda, ndugu mzazi mmoja na Yesu, ijapokuwa alitamani kuwaandikia Wakristo wenzake brua yenye kutia moyo juu ya wokovu uliokuwa wao wote, alilazimika badala yake kuwatia moyo “[waishindanie] imani waliokabidhiwa watakatifu mara moja tu.” Watu wasiomwogopa Mungu, walikuwa wameingia katika kundi, pamoja na mwenendo wao mpotovu. Hawa walikuwa kama wale malaika waliokuwa metenda dhambi kabla ya siku za Gharika, na kama wakaaji wachafu wa Sodoma na Gomora na kama Waisraeli waliopotozwa na mabinti waasherati wa Moabu na Midiani. Walikuwa wakichafua mwili na kuingiza maongozi ya kinyama katika watu wa Mungu. Kwa hiyo Yuda aliwashauri Wakristo wenye akili safi hivi: “Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika [roho takatifu], jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele.”—Yuda 3-7,19-21.
10, 11. (a) Ni Kwa sababu gani onyo la upole lililo katika Waefeso 5:3-5 ni la maana sasa kwa Wakristo? (b) Ni onyo gani tunalopaswa kutii kuhusu “yule mwanamke Yezebeli,” na kwa sababu gani?
10 Tunaweza kutazamia kuendelea kukaa bila kuchafuliwa na “uchafu” wa ulimwengu ikiwa tu tutaendelea ‘kuishindania imani’ hii. (Efe. 5:3-5) Katika ujumbe wake kwa kundi la Thiatira, Yesu “Mwana wa Mungu” alisema hivi: “Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako, tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza. Lakini nina neno hili juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu. Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake.”—Ufu. 2:19-21.
11 Yezebeli, mke wa Mfalme Ahabu wa Israeli wa nyakati zilizotangulia Ukristo, aliyekuwa mwabudu wa sanamu, alikuwa. na sifa mbaya sana kwa sababu ya matendo yake ya uasherati. Wakati mwanawe Yoramu alipomwuliza Mfalme Yehu aliyetiwa mafuta kama nyumba ya Ahabu ilikuwa na amani, yeye alijibu hivi: “Amani gani, maadamu uzinzi wa mama yako Yezebeli na uchawi wake ni mwingi?” Na baada ya kuwaua Wafalme Yoramu na Ahazia (wa Yuda), Yehu aliendelea kumwua Yezebeli, pamoja na wana 70 wa Ahabu na wale wengine wote waliosalia wa nyumba yake, pamoja na wote waliozoea ibada ya uasherati ya dini ya Baali. (2 Fal. 9:22-10:28) . Acheni’ sisi leo tulitii onyo hili la mfano, tusije tukatoka katika njia ya haki na kuzichunguza “fumbo za Shetani.”—Ufu. 2:24.
UKIMBIE ‘UFUATIAJI WA MALI’
12. “Kupenda fedha” ni nini na kwa sababu gani kunapaswa kuepukwa?
12 Kuna mikazo mingine ambayo Ibilisi huleta juu ya watumishi waaminifu wa Yehova, yote ikikusudiwa ituondoe katika ufalme wa Mungu na haki yake.(Mt. 6:33) Mtume Paulo alionya juu ya maongozi ya werevu ya “kupenda fedha” ambayo yanaweza kumwongoza mtu aiache imani. “Kupenda” huku kunaweza kutia ndani mambo mengi mbalimbali, si fedha peke yake, bali utajiri wote wa mambo ya kimwili, anasa pamoja na shughuli zinazoweza kunuliwa na fedha. Huku “kupenda fedha” kunaweza kuchukua wakati mwingi sana na kufanya maisha ya kila siku yawe magumu na yenye kuharibu imani ya Kikristo. Na kama matokeo, mtu anaweza “kujichoma kwa maumivu mengi.”—1 Tim. 6:10.
13. Wazee na hata vijana wanaweza kufauluje katika ‘kuvipiga vile vita vizuri vya imani’?
13 Mtume Paulo alimshauri kijana Timotheo kwamba, mahali pa kufuatia utajiri, anapaswa ‘kuweka macho yake’ kwenye mradi utakaomthawabisha kiroho maishani: “Bali wewe, mtu wa Mungu, uyakimbie mambo hayo, ukafuate haki, utauwa, imani, upendo, saburi, upole. piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi.” (1 Tim. 6:11, 12) Kwa kumtegemea Yehova, enyi vijana wa leo mnaweza kufaulu vivyo hivyo katika ‘kuvipiga vita hivyo vizuri vya imani.’ Na vilevile na ninyi mlio wazee!
14. (a) Ni mambo gani mawili ambayo lazima ‘tupigane nayo kwa ajili ya imani’? (b) Waebrania 13:4-6 huonyeshaje hivyo?
14 Inapaswa kuangaliwa kwamba Maandiko yanatushauri tupigane vita hivi vya imani kuhusiana na uasherati na kupenda fedha. Katika kila jambo, imani yenye nguvu, pamoja na kusimama imara katika imani yetu ndiko kutakaotuwezesha tufaulu kuyapinga majaribu ya Ibilisi. Paulo anatushauri vivyo hivyo katika Waebrania 13:4-6: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na. malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu. Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kataisa. Hata twathubutu kusema [Yehova] ndiye anisaidiaye, sitaogopa, mwanadamu atanitenda nini?” Tukiutumaini kabisa msaada wa Yehova, acheni tuazimie kabisa kuvipiga vita vya imani mpaka mwisho wa taratibu hii mbovu!
KUSHINDANA NA MAGUMU
15, 16. Kichocheo gani ambacho kimetolewa na makusanyiko? (b) Ni kitia moyo gani tunachopaswa kupata kutoka katika Wagalatia 6:9, 10, sana sana kwa sababu ya hudhurio la Ukumbusho la mwaka jana?
15 “Imani Ishindayo” Makusanyiko ya Mataifa Yote ya Mashahidi wa Yehova yamekuwa hatua kubwa katika mwendo wa watu wa Mungu wa duniani. Yalitoa kichocheo kilichohitajiwa sana. Miaka michache iliyopita imekuwa wakati wa kutengenezwa upya. Wengi wetu tulikuwa tumetumaini kwamba kufikia sasa tungekuwa tumeona mwisho wa taratibu hii mbovu ya mambo. Ni kweli, tumeona kutengenezwa upya kuliko kukubwa zaidi ambako kumepata kutoka katika usimamizi wa tengenezo la Mashahidi wa Yehova, walakini “taratibu mbovu ya mambo” haijaisha bado. Kwa wazi, bado Yehova ana kazi ya kufanywa na sisi. “[Kwa hiyo,] tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozima roho. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.”—Gal. 6:9, 10.
16 Wazee wa kundi, vichwa vya jamaa pamoja na wengine wanaendelea kujitahidi katika njia yenye kusifika katika ‘kutendea mema wale wa jamaa ya waaminio,’ nayo matunda mema ya hili yanaonekana katika kifungo cha upendo na mapendano ambacho kinawaunganisha watu wa Yehova kwa nguvu sana duniani pote. Kwa huo wanatambuliwa kuwa wanafunzi wa Yesu. (Yohana 13:34, 35) Umoja huu mkuu katika imani ni jambo lisiloweza kukadiriwa kwa hesabu katika ripoti. Walakini hudhurio lenye kutokeza sana la 5,095,831 katika ukumbusho wa Chakula cha Bwana cha Jioni Machi 23, 1978 duniani pote laonyesha kwamba kuna watu milioni nyingi, ambao bado kujiweka wakf kwa Yehova, wanaopenda sana kushirikiana na watu wa Mungu. Hawa wote nao, na wasaidiwe kuwa washindi kwa imani!
17. Hagai 2:7 na Zekaria 8:23 yanaendeleaje kutimizwa?
17 Kwamba wapya hawa, “vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote,” wanaendelea kuingia ndani inaonyeshwa na jambo la kwamba 18,754 wao walibatizwa katika “Imani Ishindayo” makusanyiko yaliyokwisha fanywa mpaka sasa. (Hag. 2:7) Vilevile, katika orodha iliyo katika ukurasa 10 mpaka 13 inaonyesha kwamba Mashahidi wapya 95,052 walibatizwa duniani pote katika kupindi cha miezi 12 iliyomalizikia Agosti, 1978. Tunafurahi kwamba wenye thamani hawa kutoka “lugha zote za mataifa” wanajiunga pamoja na mabaki ya watiwa mafuta katika utumishi wa Yehova, “wakisema, Tutakwenda pamoja nanyi [enyi watu], kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.”—Zek. 8:23.
18. (a) Ibadi kubwa inaendeleaje kuonyesha imani? (b) Kama orodha inavyoonyesha. ni maonyo gani ya Maandiko yaliyo ya muhimu?
18 Hata hivyo, orodha hii inaonyesha jambo jingine: Kwamba wengine wa watumishi wa Mungu waliobatizwa wamekuwa walegevu. Idadi kubwa wanaendelea kuonyesha imani ishindayo. Nchi kadha zinapata ongezeko la wanaojiandikisha katika kazi ya wakati wote ya painia, tena kuna zaidi ya watu milioni mbili wanaofanya utumishi wa shambani kikiwa kilele. Lakini inaokekana kwamba hesabu fulani kwa mia wamejiachilia washindwe na mikazo inayoletwa kwao na Ibilisi na taratibu yake. Uasherati wa ulimwengu, ufuatiliaji wa anasa na wa udanganyifu wa mali, pamoja na kushindwa kuendelea kukesha juu ya haraka ya nyakati —mambo haya yameleta madhara yake yajapokuwako maonyo ya Maandiko juu ya hatari kama hizo. (Luka 17:26-30; 1 Yohana 2:15-17) Kwa kweli huu ndio wakati wa maana sana kwetu ‘kukesha, kusimama imara katika imani.’—1 Kor. 16:13.
[Maelezo ya Chini]
a Kutoka L’Eglise de Montreal, gazeti la kila juma la Jimbo la Askofu Mkuu la Kikatoliki la Montreal, Canada.
[Picha katika ukurasa wa 5]
Uasherati pamoja na “kupenda fedha’” ndizo hila mbili kuu anazofumia Ibilisi kuvunja imana ya Kikristo katika hizi siku za mwisho