HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 35-36
Tumepewa Uwezo wa Kufanya Kazi ya Yehova
Roho takatifu ya Yehova iliwawezesha Bezaleli na Oholiabu kufuata maagizo ya kujenga hema la ibada. (Ona picha kwenye jalada.) Leo, watumishi wa Yehova wanaweza pia kupata roho yake takatifu. Tunapaswa kufanya nini ili itunufaishe?
Tunapaswa kusali roho takatifu itusaidie kutumia ustadi wetu kwa njia nzuri zaidi tunapomtumikia Yehova
Tunapaswa kujifunza kwa ukawaida Neno la Mungu lililoongozwa na roho
Tunapaswa kufanya yote tuwezayo tunapopewa mgawo wowote ule
Yehova anaweza kukuwezesha kutimiza migawo gani?