Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 10/1 uku. 3
  • Kwa Nini Watu Husali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Watu Husali?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Kumkaribia Mungu Katika Sala
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Yesu Anatufundisha Kusali
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 10/1 uku. 3

HABARI KUU | JE, KUNA FAIDA YOYOTE TUNAPOSALI?

Kwa Nini Watu Husali?

“Nilipenda sana kucheza kamari. Nilikuwa na kawaida ya kusali ili nishinde. Lakini sikuwahi kushinda.”—Samuel,a Kenya.

“Tulipokuwa shuleni tulikariri na kusali sala tulizofundishwa.”—Teresa, Ufilipino.

“Mimi husali ninapopata matatizo. Ninasali ili kuomba msamaha wa dhambi na ili kuwa Mkristo anayefaa.”—Magdalene, Ghana.

1. Mwanamume akisali katika meza ya kuchezea kamari; 2. Msichana akisali shuleni; 3. Mwanamke akisali

Maelezo yaliyotolewa na Samuel, Teresa, na Magdalene yanaonyesha kwamba watu husali wakiwa na malengo mbalimbali, mazuri au mabaya. Baadhi ya watu husali kutoka moyoni; na wengine hawasali kutoka moyoni. Hata hivyo, iwe wanasali ili kufaulu mitihani shuleni, timu wanayoipenda ishinde, Mungu asaidie familia zao, au kwa sababu zozote zile, watu wengi huona kuna uhitaji wa kusali. Kwa kweli, utafiti mwingi uliofanywa unaonyesha kwamba hata baadhi ya watu wasio na dini husali kwa ukawaida.

Je, wewe husali? Ikiwa ndiyo, basi unasali kwa ajili ya nini? Iwe una kawaida ya kusali au la, huenda ukajiuliza: ‘Je, kuna faida yoyote tunaposali? Je, kuna yeyote anayesikiliza sala?’ Mwandishi mmoja alisema sala ni “aina mojawapo ya matibabu . . . sawa na kuzungumza na samaki unayemfuga.” Wataalamu wa tiba wana maoni hayo pia, nao husema kwamba sala ni aina mojawapo ya “tiba mbadala.” Je, watu wanaotoa sala hupata faida yoyote nyingine?

Tofauti na maoni ya watu wengi, Biblia inataja kwamba sala ina faida nyingi zaidi ya kuwa tiba. Inasema kwamba kuna mtu anayesikiliza sala zinazotolewa kwa njia inayofaa na kwa mambo yanayofaa. Je, jambo hilo ni la kweli? Acheni tuone uthibitisho.

a Baadhi ya majina yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki