Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 4 uku. 13
  • Usadikisho Mkubwa Kutoka Kwenye Herufi Ndogo Zaidi ya Kiebrania

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usadikisho Mkubwa Kutoka Kwenye Herufi Ndogo Zaidi ya Kiebrania
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Mahubiri ya Mlimani—Sikuja Kutangua Bali Kutimiliza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Jina la Mungu Lilipatwa na Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 4 uku. 13
Tetragramatoni, herufi ndogo zaidi ikiwa imetiwa rangi

Tetragramatoni, jina takatifu la Mungu, Yehova, katika herufi za Kiebrania, ambazo husomwa kutoka kulia kwenda kushoto

Usadikisho Mkubwa Kutoka Kwenye Herufi Ndogo Zaidi ya Kiebrania

Je, kweli tunaweza kuwa na uhakika kwamba ahadi zote za Mungu zitatimia? Yesu aliamini kabisa jambo hilo, na mafundisho yake yalijenga imani ya wale waliomsikiliza. Hebu fikiria mfano huu aliotoa kwenye Mahubiri yake ya Mlimani, unaopatikana katika andiko la Mathayo 5:​18: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba mbingu na dunia zingepitilia mbali upesi zaidi kuliko herufi moja ndogo zaidi au nukta moja ya herufi kupitilia mbali kutoka katika Sheria na mambo yote yasitukie.”

Herufi ndogo zaidi katika alfabeti ya Kiebrania ni י (yod), ambayo ni herufi ya kwanza ya Tetragramatoni, jina takatifu la Mungu, Yehova.a Waandishi na Mafarisayo waliona kila “nukta moja ya herufi” kuwa muhimu sana kama vile tu walivyoona maneno na herufi nyingine za Sheria ya Mungu.

Yesu alikuwa akisema kwamba ni rahisi zaidi kwa mbingu na dunia kupitilia mbali kuliko sehemu ndogo zaidi ya Sheria kukosa kutimia. Hata hivyo, Maandiko yanatuhakikishia kwamba mbingu na dunia halisi zitadumu milele. (Zaburi 78:69) Kwa hiyo, maneno hayo ya Yesu yalionyesha kuwa hakuna hata sehemu ndogo ya Sheria ambayo haingetimizwa.

Je, Yehova Mungu anachukulia kwa uzito hata mambo madogo kabisa? Bila shaka. Fikiria jambo hili: Waisraeli wa kale waliambiwa wasivunje mfupa wowote wa kondoo wa Pasaka. (Kutoka 12:46) Huenda hilo likaonekana kuwa jambo dogo. Je, walielewa kwa nini hawakupaswa kuvunja mfupa wowote? Labda hawakuelewa. Lakini Yehova Mungu alijua kwamba jambo hilo lingekuwa na utimizo wa kinabii kuhusiana na Masihi. Hakuna mfupa wake hata mmoja ambao ungevunjwa katika kifo chake kwenye mti wa mateso.​—⁠Zaburi 34:20; Yohana 19:​31-​33, 36.

Maneno ya Yesu yanatufundisha nini? Sisi pia tunaweza kuwa na uhakika kabisa kwamba ahadi zote za Yehova zitatimia kikamili. Kwa kweli huo ni usadikisho mkubwa kutoka kwenye herufi ndogo zaidi ya Kiebrania!

a Herufi ndogo zaidi katika alfabeti ya Kigiriki ni iota na inafanana tu na ile ya Kiebrania י (yod). Kwa sababu Sheria ya Musa iliandikwa na kupitishwa kwa vizazi vingine katika Kiebrania, inaelekea Yesu alikuwa akirejelea herufi ya Kiebrania.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki