Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 5 kur. 4-5
  • Ukweli Kuwahusu Malaika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ukweli Kuwahusu Malaika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 5 kur. 4-5
Malaika mkuu akiwa na makumi ya maelfu ya malaika wengine

HABARI KUU | MALAIKA​—JE, WANAHUSIKA KATIKA MAISHA YAKO?

Ukweli Kuwahusu Malaika

Je, ungependa kujua ukweli kuwahusu malaika—wao ni nani, walitoka wapi, na wanafanya nini? Hakuna mahali pengine tunapoweza kupata majibu sahihi ya maswali hayo isipokuwa, katika Biblia, Neno la Mungu lililoongozwa na roho Yake. (2 Timotheo 3:16) Maandiko yanasema nini kuwahusu malaika?

  • Kama ambavyo Mungu ni Roho, malaika pia ni viumbe wa roho wasioonekana, nao hawana “nyama na mifupa.” Malaika washikamanifu wanaishi mbinguni nao wanatumikia mbele za Mungu.—Luka 24:39; Mathayo 18:10; Yohana 4:24.

  • Nyakati fulani malaika walikuja duniani wakiwa wamejivika miili ya kibinadamu ili kutimiza migawo waliyopewa na Mungu, na kurudia miili yao baada ya kumaliza migawo hiyo.—Waamuzi 6:11-23; 13:15-20.

  • Ingawa katika Biblia malaika wanatajwa wakiwa wa kiume na mara zote walikuja duniani na miili ya kiume, ukweli ni kwamba wao hawana jinsia ya kiume wala ya kike. Hawaoani wala kuzaliana. Kwa kuongezea, malaika hawakuwa wanadamu zamani, wakiwa watoto au watu wazima. Wao waliumbwa na Yehova; ndio sababu Biblia inawaita “wana wa Mungu wa kweli.”—Ayubu 1:6; Zaburi 148:2, 5.

  • Biblia inataja kuhusu “lugha za wanadamu na za malaika,” ikionyesha kwamba viumbe wa roho wana njia ya mawasiliano na lugha. Ingawa Mungu amewatumia malaika kuwasiliana na wanadamu, hataki tusali kwao wala kuwaabudu.—1 Wakorintho 13:1; Ufunuo 22:8, 9.

  • Kuna makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu ya malaika, na hivyo huenda wakafikia mabilioni.a—Danieli 7:10; Ufunuo 5:11.

  • Malaika wana “nguvu nyingi,” zinazopita za wanadamu, na pia wana uwezo mkubwa zaidi wa akili. Kwa kweli malaika wanaweza kusafiri kwa kasi sana, kuliko tunavyoweza kuwazia.—Zaburi 103:20, Verbum Bible; Danieli 9:20-23.

  • Licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa akili na nguvu nyingi, malaika wana mipaka, na kuna mambo ambayo hawajui.—Mathayo 24:36; 1 Petro 1:12.

  • Malaika waliumbwa wakiwa na utu tofauti-tofauti, sifa kama za Mungu, na uhuru wa kuchagua. Hivyo, kama vile wanadamu, wanaweza kuchagua kufanya mema au mabaya. Kwa kusikitisha, baadhi ya malaika waliamua kumwasi Mungu.—Yuda 6.

a Makumi ya elfu ni 10,000. Na elfu kumi mara elfu kumi ni sawa na milioni 100. Hata hivyo, kitabu cha Ufunuo kinataja kuhusu, “makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu” ya malaika. Hiyo ni sawa na mamia ya mamilioni, au hata mabilioni ya viumbe hao wa roho!

Malaika Wa Mungu Wamepangwa Jinsi Gani?

Malaika Mkuu, Mikaeli, ni mkuu katika nguvu na mamlaka. Maandiko yanaonyesha wazi kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo.—1 Wathesalonike 4:16; Yuda 9.

Maserafi ni malaika wenye daraja la juu katika mapendeleo na heshima kuliko malaika wengine, nao wanatumikia kuzunguka kiti cha ufalme cha Mungu.—Isaya 6:1-3.

Makerubi pia wana cheo cha juu, nao hushughulikia majukumu ya pekee yanayohusu ukuu wa Mungu Mweza Yote. Mara nyingi wanatajwa wakiwa wanamtumikia Mungu moja kwa moja.—Mwanzo 3:24; Ezekieli 9:3; 11:22.

Makumi ya maelfu ya malaika wengine hutumikia wakiwa wajumbe na wawakilishi wa Mwenye Enzi Kuu katika kufanya mapenzi yake.b —Waebrania 1:7, 14.

b Ili upate habari zaidi kuhusu malaika, soma sura ya 10 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? na vilevile nyongeza yenye kichwa “Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?” kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Pia, kinapatikana kwenye www.jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki