Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 5 uku. 3
  • Malaika​—Je, Wanahusika Katika Maisha Yako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaika​—Je, Wanahusika Katika Maisha Yako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Una Malaika Anayekulinda?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 5 uku. 3
Wenzi wa ndoa wakimfariji mwanamke kwa kutumia Biblia

HABARI KUU | MALAIKA​—JE, WANAHUSIKA KATIKA MAISHA YAKO?

Malaika​—Je, Wanahusika Katika Maisha Yako?

Jumapili moja alasiri, Kenneth na Filomena, wanaoishi Curaçao, walienda kuwatembelea wenzi fulani wa ndoa ambao walikuwa wanajifunza nao Biblia.

Kenneth anasimulia hivi: “Tulipofika, nyumba ilikuwa imefungwa na gari halikuwepo. Lakini kitu fulani kilinisukuma nimpigie simu mke wake.”

Mwanamke huyo alipokea simu na kusema kwamba mume wake yuko kazini. Hata hivyo, alipojua kwamba Kenneth na Filomena walikuwa mlangoni, alifungua mlango na kuwakaribisha ndani.

Mara moja wakagundua kwamba alikuwa analia. Kenneth alipokuwa akitoa sala ili waanze kujifunza Biblia, mwanamke huyo alianza tena kulia. Hivyo, kwa fadhili Kenneth na Filomena walimuuliza alikuwa na tatizo gani.

Mwanamke huyo aliwaeleza kuwa alikuwa amepanga kujiua alasiri hiyo, na kwamba alikuwa anaandika ujumbe wa kumuaga mume wake wakati Kenneth alipompigia simu. Aliwaeleza kuwa anasumbuliwa na tatizo la kushuka moyo, kwa hiyo wakamfariji kwa kutumia Biblia. Kitia moyo chao kiliokoa maisha yake.

Kenneth anasema hivi: “Tunamshukuru Yehova kwa kutuwezesha kumsaidia mwanamke huyo aliyekuwa ameshuka moyo, hasa kwa jinsi alivyotuongoza, labda kupitia malaika au roho Yake takatifu, na kutusukuma tumpigie simu!”a

Je, Kenneth na Filomena walikuwa na sababu za kuamini kwamba Mungu aliingilia kati, iwe ni kupitia malaika au roho Yake takatifu, yaani nguvu Yake ya utendaji? Au je, inawezekana tu kwamba kwa tukio zuri Kenneth alipiga simu muda unaofaa?

Hatuwezi kusema kwa hakika kuhusu hilo. Lakini kile tunachojua ni kwamba Mungu huwatumia malaika zake kuwasaidia watu kiroho. Kwa mfano, Biblia inasema kwamba Mungu alimtumia malaika kumwelekeza Filipo, mweneza injili Mkristo, amsaidie ofisa Mwethiopia ambaye alikuwa anatafuta msaada wa kiroho.—Matendo 8:26-31.

Dini mbalimbali zinaamini kwamba kuna viumbe wa roho wenye nguvu nyingi, na baadhi yao hutumiwa na Mungu kutimiza mapenzi yake au kumlinda mwanadamu mmoja mmoja. Zaidi ya kuamini kwamba kuna malaika, watu wengi wanaamini kuwa viumbe hao wa roho wanahusika kwa kiasi kikubwa katika maisha yao. Hata hivyo, kuna wengine wengi ambao hawaamini kabisa kwamba kuna malaika.

Je, malaika ni viumbe halisi? Ikiwa jibu ni ndio, basi walitoka wapi? Biblia inasema nini kuwahusu malaika? Je, wanahusika katika maisha yako? Acheni tuchunguze ukweli wa mambo.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyoonyeshwa katika Biblia.—Zaburi 83:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki