Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 5 uku. 5
  • Je, Una Malaika Anayekulinda?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Una Malaika Anayekulinda?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Una Malaika Mlinzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 5 uku. 5

HABARI KUU | MALAIKA​—JE, WANAHUSIKA KATIKA MAISHA YAKO?

Je, Una Malaika Anayekulinda?

Biblia haifundishi kwamba kila mtu ana malaika wake anayemlinda. Ni kweli kwamba Yesu aliwahi kusema: “Angalieni msimdharau mmoja wa hawa wadogo [wanafunzi wa Kristo]; kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika zao mbinguni sikuzote huuona uso wa Baba yangu aliye mbinguni.” (Mathayo 18:10) Hata hivyo, badala ya kumaanisha kwamba kila mtu ana malaika anayemlinda, Yesu alimaanisha kuwa malaika wanamhangaikia kila mwanafunzi wake. Hivyo, waabudu wa kweli hawafanyi maamuzi yasiyo ya hekima au kujihatarisha, huku wakidhani kwamba malaika wa Mungu watawalinda.

Je, hilo linamaanisha kwamba malaika hawawasaidii wanadamu? Jibu ni hapana. (Zaburi 91:11) Baadhi ya watu wanaamini kabisa kwamba Mungu amewalinda na kuwaongoza kupitia malaika. Kenneth aliyetajwa katika makala ya kwanza, ni mmoja wa wale wanaoamini hivyo. Huenda yuko sahihi. Mara nyingi, Mashahidi wa Yehova wameona mambo yanayothibitisha kwamba malaika wanaunga mkono kazi yao ya kuhubiri. Hata hivyo, kwa kuwa malaika hawaonekani, hatuwezi kusema kwa usahihi Mungu anawatumia kwa kadiri gani kuwasaidia watu katika mambo mbalimbali. Lakini, si kosa kumshukuru Mweza Yote kwa kila msaada anaotuandalia.—Wakolosai 3:15; Yakobo 1:17, 18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki