Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/91 uku. 4
  • Kuwatendea Vijana Yaliyo Mema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwatendea Vijana Yaliyo Mema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • “Mambo Hayo Uwakabidhi Watu Waaminifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Thamini Nguvu za Vijana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Wachanga Wahitaji Kielelezo Chema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Wathamini Ndugu na Dada Zetu Waaminifu Wenye Umri Mkubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 12/91 uku. 4

Kuwatendea Vijana Yaliyo Mema

1 Sikuzote Yehova amehangaikia wale wanaoonewa. (Zab. 146:7-9) Katika nyakati za kale alifanya mipango ya pekee kuhakikisha kwamba hata vijana wasiofanikiwa wanaangaliwa. Sheria yake aliyowapa Israeli ilitaja waziwazi “yatima.” (Kut. 22:22-24) Ingawa leo hatuko chini ya sheria hiyo ya kale, je! kanuni ya sheria hiyo si inatupa wajibu kama Wakristo?

2 Katika makundi mengine ya Mashahidi wa Yehova, kuna wale ambao twaweza kuwaita vijana “yatima.” Hiyo ni kwa sababu wazazi wao hawaamini. Vijana wengine wanao wazazi waamini ambao huenda wakahitaji msaada katika kutoa msaada wa kiroho kwa watoto wao. Huenda ikawa kwamba wazazi hao ni wapya sana katika kweli na hawako katika hali ya kuweza kusaidia watoto wao kwa matokeo, kama ambavyo wangependa. Kwa ajili ya mikazo ya namna zote kuleta mambo mengi yenye kuongezeka, huenda wengine wakawa na ugumu wa kupanga wakati wa kutosha wa kujifunza na watoto wao au kufanya nao kazi katika utumishi wa shambani, na kadhalika. Wazazi wengine, ingawa wana tamaa ya kutoa msaada unaohitajiwa, wanajikuta wakiwa na uhitaji wa kusaidiwa kuingiza sana kweli za Neno la Mungu ndani ya akili na mioyo ya watoto wao.

3 Unaweza Kufanya Nini?: Swali ambalo wote katika kundi wanaweza kufikiria kwa uzito ni hili: “Naweza kutoaje msaada na kitiamoyo kinachohitajiwa?” Wale wenye migawo katika mikutano wanaweza kutia ndani vijana pindi kwa pindi. Je! vijana wengi tofautitofauti walio mfano mzuri kundini wanaweza kutumiwa katika sehemu za mkutano? (Mdo. 16:1, 2) Ingawa wengine huenda wasiwe na kipawa cha kujieleza kama wengine, kuwapa mapendeleo ya pindi kwa pindi kutawatia moyo hata na wengine. Huenda ikachukua wakati kusaidia wengine, lakini mazoezi, mambo yaliyoonwa na uangalifu huu, yataleta faida nyingi kwa kadiri vijana wetu waaminifu wanavyokua katika kweli.

4 Wazazi wana wajibu waliopewa na Mungu wa kusaidia watoto wao. Lakini je! hiyo inamaanisha kwamba wengine hawawezi kusaidia? Sivyo kabisa! Na hilo linakuwa hivyo hasa wakati wazazi fulani wanapopatwa na magumu hayo ambayo yamekwisha kutajwa. Watoto wanaohitaji msaada wa ziada wanaweza kualikwa wajiunge na familia yako katika funzo, utumishi wa shambani na pengine tafrija zinazofaa. Je! kitia-moyo cha mtume juu ya ‘kukunjuka’ si kinahusu habari hii?—2 Kor. 6:11-13.

5 Hata wale ambao si wazazi wanaweza ‘kukunjuka’ kwa shauku ambayo wanawaonyesha vijana kwa kutumia wakati pamoja nao. Kujitoa kwao kutasaidia kutia moyo na kutia nguvu vijana.

6 Huenda ukaweza kutumia nafasi zinazopatikana kabla na baada ya mikutano upate kuzungumza na vijana. Hiyo yapaswa kuwa zaidi ya kusema “Jambo” na “u hali gani?” Mzee mmoja alimwuliza kivulana mmoja juu ya hali yake, lakini kabla ya kivulana huyo kujibu, akageuka azungumze na ndugu mwingine mzee zaidi ambaye alikuwa anataka kumwona. Baadaye kivulana huyo alikuja na kumwuliza mzee huyo: “Je! kweli kweli unataka kujua namna nilivyo?” Mzee huyo akakubali kwamba alikuwa amejifunza kutokana na jambo hilo aliloliona.

7 Vijana wanaitikia kwa utayari zaidi wanapojulikana kwa majina. Naam, wao pia ni sehemu ya kundi nao walio wazee zaidi wanapaswa kusitawisha masikilizano pamoja na washiriki hao vijana. Vijana wanapokuja kukuona kama “rafiki” yao kunakuwako utayari zaidi wa kuitikia shauri na uongozi, ama sivyo?

8 Matokeo Yenye Kudumu: Bila shaka wengi wenu mnaweza kuangalia nyuma na kukumbuka pendeleo dogo mlilopewa mlipokuwa wachanga sana. Lilikuwa lenye kutia moyo nalo lilithaminiwa, ama sivyo? Ni jambo gani lililokuvutia? Je! ilikuwa sehemu ndogo katika wonyesho? Maneno fulani ya fadhili ya kushauri au sifa iliyotolewa na mzee? Pengine jambo lililoonwa pamoja shambani wakati wa kufanya kazi na ndugu au dada mzee? Kwa kuwaona wote kundini kuwa sehemu ya “familia” kubwa iliyo kundi, kutakuwako baraka nyingi kwa vijana na kwa wazee pia. Tunapojitahidi kuiga mfano wa Yehova katika kuonyesha kupendezwa na shauku kwa ainabinadamu yote, ebu tuendelee kuwafanyia mema vijana wetu.—Imechapishwa tena kutoka km-SW 9/80.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki