Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/94 uku. 2
  • Wachanga Wahitaji Kielelezo Chema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachanga Wahitaji Kielelezo Chema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • “Mambo Hayo Uwakabidhi Watu Waaminifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Thamini Nguvu za Vijana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Wathamini Ndugu na Dada Zetu Waaminifu Wenye Umri Mkubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Kuwatendea Vijana Yaliyo Mema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 7/94 uku. 2

Wachanga Wahitaji Kielelezo Chema

1 Twashangilia kuwa pamoja na idadi inayokua ya vijana ‘wanaolisifu jina la BWANA [“Yehova,” NW].’ (Zab. 148:12, 13) Wengi wao bado ni wachanga kwa umri. Maendeleo yao yanategemea sana mafundisho na kielelezo wanachopewa na wazazi wao na wengine wakubwa katika kutaniko. Hata hivyo, jambo lisilopaswa kupuuzwa, ni uvutano unaofanywa na vijana wengine, hasa matineja wakubwa na watu wazima wachanga. Ikiwa u katika rika hili, maelezo haya yaweza kukufaidi wewe.

2 Vijana wanaokaribia utineja huelekea kuiga matineja wakubwa. Kwa asili wana tamaa ya kuwa kama rafiki zao wa karibu wanaowapenda. Huelekea kutamani vijana wengine ambao ni wakubwa hivi na wenye kuonekana kuwa wenye ujuzi na maendeleo zaidi. Likiwa tokeo, huenda wakaiga msemo na mwenendo wako na pia uthamini wako wa mambo ya kiroho na kushiriki kwako utendaji wa kutaniko.

3 Ukiwa tineja mkubwa, una pendeleo pamoja na daraka zito. Hivi sasa, kielelezo chako yaelekea chavutia washiriki wako wachanga. Jiulize mwenyewe, ‘Ni uvutano wa aina gani ninaotolea wachanga? Je! mimi hufikiri kwa uzito, nikiepuka ujinga na “tamaa za ujanani”? Je! naonyesha utii na heshima kwa wazazi wangu, wazee na watu wengine wakubwa?’ (2 Tim. 2:22; Kol. 3:20) Unalosema na kufanya laweza kuwa jambo kuu katika maendeleo ya kiroho ya wachanga wale wengine wanaoangalia matendo yako.

4 Kuhubiri ujumbe wa Ufalme ndio kazi ya msingi ya kutaniko. Utayari na kushiriki kwako kikawaida kwaweza kutia moyo washirika wako wawe watendaji zaidi. Ukiweza kuchukua utumishi wa painia, rafiki zako watachochewa katika njia hiyohiyo. Kutoa maelezo mikutanoni na kujitolea kusaidia kufanya wajibu wa lazima katika Jumba la Ufalme kwaweza pia kutoa kielelezo chema.

5 Ijapokuwa Timotheo hakuwa katika miaka yake ya utineja Paulo alipompa ushauri ufuatao, nyinyi matineja mwaweza kuutumia: “Uwe kielelezo kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, katika usafi wa kiadili.” (1 Tim. 4:12, NW) Idili yako na kushiriki kwako kwa nafsi yote katika utumishi wa Yehova kwaweza kuwachochea washirika wako na watazamaji wachanga kwa njia chanya, kukiwasaidia wafanye maendeleo kuelekea kuwa watu wakomavu kiroho. (Efe. 4:13) Matineja walio sehemu ya familia ambazo zimeanza tu kujifunza wanaweza kuvutiwa kwenye kweli na yale wanayoona kwako.

6 Hata lililo la maana zaidi, juhudi yako ya kuonyesha sifa za kimungu zinaleta heshima kwa Yehova na tengenezo lake. (Mit. 27:11) Watazamaji wenye mioyo minyoofu watastaajabia tofauti kubwa sana kati yako na vijana wengine wa ulimwengu. Kwa hiyo una fursa isiyo na kifani ya kusaidia wachanga ilhali unachangia sifa ya thamani kwa Yehova.—Zab. 71:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki