Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/89 uku. 1
  • Je! Wewe Unathamini Thamani Yavyo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unathamini Thamani Yavyo?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KITABU KUISHI MILELE
  • KUTOA TOLEO
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Kusitawisha Kupendezwa na Ujumbe wa Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Je, Unazitumia Broshua Hizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Broshua Mpya Tutakayotoa!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 12/89 uku. 1

Je! Wewe Unathamini Thamani Yavyo?

1 Ilikuwa pindi yenye kusisimua wakati msemaji kwenye “Imani Ishindayo” Mkusanyiko wa Kimataifa wa 1978 alipolimbuka kifaa kipya cha kujifunza Biblia Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Uwezo wacho wa kufunza Biblia wachanga na wakubwa pia ulionekana upesi. Watu wazima walipendezwa kujua kwamba hadithi zenyewe zilifuatana kulingana na wakati wa matukio ya Biblia. Jambo hili limesaidia wengi wafahamiane na mfuatano wa matukio ya Biblia.

2 Mama mmoja ambaye mwanaye wa miaka mitatu alikuwa anakaza fikira kwa muda mfupi tu alipatwa na ghafula ya kupendeza kumwona ‘akijifunza’ kitabu hicho akiwa kimya kwa dakika 20. Muda si muda yakawa ni mazoea yake. Wenzi wawili wachanga walianza kufunza mwana wao kutoka kitabu cha Hadithi za Biblia muda mfupi baada ya kuanza kujifunza Biblia. Katika pindi moja, wakati jamaa hiyo ilipokuwa inakaribia kula chakula, mvulana huyo alikataa kula mpaka sala itolewe.

3 Tangu kitabu Hadithi za Biblia kilipolimbuliwa mara ya kwanza zaidi ya nakala milioni 23 zimechapwa katika lugha 66. Tunathamini thamani ya kifaa hiki kizuri cha kujifunza Biblia na tuko katika hali nzuri ya kukitoa kwa moyo kamili kwa wachanga na wakubwa pia katika Desemba.

KITABU KUISHI MILELE

4 Yehova alitupa hazina nyingine kwa namna ya kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Hiki kimekuwa kichapo bora kwa kuanzisha mafunzo na kuwasaidia wapya wajifunze kweli za msingi za Biblia. Katika shamba letu watu wengi, karibu wote, tayari wanaikubali Biblia kuwa Neno la Mungu. Hata hivyo sura ya 5 katika kitabu Kuishi Milele inatoa habari nzuri sana inayotia uhakika katika usahihi na ukweli wa Biblia. Kutumia sura hii kuhusiana na Kichwa cha Mazungumzo chetu cha wakati huu kutasaidia wengi waone thamani ya kujifunza Biblia.

KUTOA TOLEO

5 Unapofanyia kazi eneo lenu, huenda ukasema: “Tunazungumza na majirani wetu juu ya mahali tunapoweza kupata msaada unaofaa ili kukabiliana na matatizo ya maisha. Wakati uliopita, watu wengi walitafuta msaada katika Biblia. Lakini tunaishi wakati ambao mielekeo inabadilika. Ni kwa nini hasa sisi katika karne ya 20 tunapaswa kusoma na hata kujifunza Biblia? Leo, twaweza kuongea juu ya sababu mbili za msingi.” Halafu uendelee na utoaji kama ulivyotolewa muhtasari kwenye Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1989, ukurasa wa pili. Baada ya Yohana 17:3 waweza kusema hivi kwa kumalizia: “Hata watoto wanapaswa kufunzwa kanuni za msingi za Biblia. Wafunzwe na nani? Andiko lifuatalo katika Mithali 1:8 linakazia daraka la kimzazi katika kufundisha watoto juu ya Mungu. (Someni.) Hata hivyo, wazazi walio wengi tunaozungumza nao wangethamini kweli kweli msaada fulani katika kujua juu ya wanavyoweza kufunza watoto wao Neno la Mungu. Kwa kutambua uhitaji huo tunatangaza kwa chapa kifaa hiki cha kujifunza Biblia chenye kichwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Kama unavyoona haya ni mazungumzo yenye kufuatana kulingana na wakati wa matukio ya Biblia kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo katika lugha sahili, inayoeleweka kwa urahisi ambayo kwa kweli inatia moyo watoto wajifunze juu ya Mungu. Pia picha zinavuta fikira zao na ni misaada mizuri sana ya kufundisha. Kwa ajili ya faida yako na ya jamaa yako tungependa kukuachia nakala hii kwa mchango wa _________.”

6 Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu Hadithi za Biblia au ikiwa ingefaa zaidi kutoa kitabu Kuishi Milele, unaweza kutumia dokezo lililotolewa katika fungu 4. Au unaweza kuelekeza kwenye sura moja kwenye kitabu hicho unayosadiki ingempendeza mwenye nyumba. Kitabu Kuishi Milele hasa ni msaada katika kuanzisha mafunzo ya Biblia mapya. Kwa hiyo umwonyeshapo mwenye nyumba habari zilizozungumzwa, elekeza fikira pia kwenye maswali yaliyo chini ya ukurasa, maandiko yaliyotajwa, na maswali yanayotegemea Biblia kwenye mafungu. Huenda ukaweza kuanzisha funzo kwenye ziara ya kwanza.

7 Tunamshukuru Yehova kwa ajili ya Maandiko Matakatifu ambayo kwayo ‘mtu wa Mungu aweza kuwa na uwezo wa kutosha, aliye tayari kabisa kwa kila kazi njema.’ (2 Tim. 3:17, NW) Pia tunashukuru kwa ajili ya vichapo kama vile kitabu Hadithi za Biblia na kitabu Kuishi Milele. Tunathamini thamani yavyo na tunafurahi kwamba tunaweza kuvitoa kwa wengine katika mwezi wa Desemba.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki