Sanduku la Swali-2
● Kwa nini mtu ajipatie maktaba ya kibinafsi?
Sababu moja ya msingi ni kwamba funzo la kibinafsi ni la muhimu kwa Mashahidi wa Yehova. (Yn. 17:3) Ni jambo linalofaa kuwa na maktaba nyumbani ili kufanya utafiti, kujibu maswali, na kutayarisha kwa ajili ya mikutano ya Kikristo. Hatupaswi kupuuza thamani ya kupata kwa urahisi habari zenye kutegemeka za Maandiko.
Sababu nyingine ya kuwa na maktaba ya nyumbani inahusiana na uhakika wa kwamba lazima kila Mkristo ‘alichukue furushi lake mwenyewe’ la daraka. (Gal. 6:5) Maswali yanapotokea, ni vizuri kuwa na tabia ya kufanya utafiti wetu wenyewe kwanza halafu kuuliza maswali ya wengine inapohitajiwa tu. Tunaweza kukuza nguvu zetu za utambuzi na ufahamu kwa kuwa wanafunzi wenye juhudi wa Neno la Mungu na kutumia vizuri maktaba ya nyumbani.—Ebr. 5:11-14.
Watoto fulani wamesaidiwa na wazazi wao kuweka maktaba yao ya kibinafsi, kwa kufikiria mahitaji ya sasa na ya wakati ujao. Hakuna shaka kuhusu jambo hilo, maktaba nzuri ya kibinafsi ni miliki yenye thamani katika nyumba ya Kikristo.