Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/88 uku. 4
  • Kutangaza Habari Njema—Nyumba kwa Nyumba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema—Nyumba kwa Nyumba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KILE AMBACHO KAZI YA NYUMBA KWA NYUMBA INATIMIZA
  • KUSHINDA VIZUIZI
  • Kwa Nini Huduma ya Nyumba kwa Nyumba Ni ya Maana Sasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Kuhubiri Nyumba kwa Nyumba
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Kuhubiri Katika Ulimwengu Wenye Uasi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Fundisha Peupe Na Kutoka Nyumba Kwa Nyumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 6/88 uku. 4

Kutangaza Habari Njema—Nyumba kwa Nyumba

1 Kazi yetu ya kuhubiri habari njema za ufalme imeamrishwa na mamlaka iliyo kuu zaidi katika ulimwengu wote mzima, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova na Mwana wake aliyemilikishwa, Yesu Kristo.—Mt. 28:18; Ufu. 14:6, 7.

2 Yesu aliweka kigezo kwa “kusafiri kutoka jiji kwa jiji na kutoka kijiji kwa kijiji, akihubiri na kutangaza habari njema za ufalme wa Mungu.” (Luka 8:1, NW) Wanafunzi wake hawakukosa somo alilofundisha kupitia kwa neno na kwa kielelezo. (Mt. 13:51, 52) Wao walithamini umaana wa kazi ya kuhubiri waziwazi. Hata baada ya kupigwa kwa sababu ya kusema kwao waziwazi, wao hawakuacha lakini waliendelea kila siku katika hekalu na nyumba kwa nyumba “kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Mdo. 5:41, 42, NW; 20:20) Katika nyakati za ki-siku-hizi kazi hii inatimizwa na Mashahidi wa Yehova peke yao, ambao walitumia zaidi ya saa milioni 739 katika utendaji wa kuhubiri mwaka uliopita, nyingi zazo zikiwa zilitia ndani kazi ya nyumba kwa nyumba.—Hag. 2:7; Isa. 60:22.

KILE AMBACHO KAZI YA NYUMBA KWA NYUMBA INATIMIZA

3 Kama inavyoonyeshwa katika Ezekieli 33:33 na 38:23, utendaji wetu wa nyumba kwa nyumba unatimiza sehemu ya maana katika kutakaswa kwa jina la Yehova. Habari njema za Ufalme zinawekwa mbele ya wenye nyumba mmoja mmoja, zikiwapa nafasi ya kuonyesha wanaposimama. (2 The. 1:8-10) Kwa tumaini, watasukumwa kuchukua msimamo wao upande wa Yehova na kupokea uhai.—Mt. 24:14; Yoh. 17:3.

4 Pia kazi ya nyumba kwa nyumba ya kawaida inatia nguvu tumaini letu katika ahadi za Mungu. Uwezo wetu wa kutumia Biblia kwa matokeo mazuri unazidishwa. Tunasaidiwa kushinda hofu ya wanadamu. Hisia-mwenzi yenye kiasi kikubwa inaweza kukuzwa tunapoangalia kwanza watu wanaoteseka kwa sababu ya kutomjua Yehova na wasioishi kupatana na viwango vyake vyenye uadilifu. Pia tunasaidiwa kukuza tunda la roho ya Mungu katika maisha yetu wenyewe.—Gal. 5:22, 23.

KUSHINDA VIZUIZI

5 Je! wewe unapata kwamba watu wengi hawapo nyumbani wakati unapozuru wakati wa mchana? Namna gani ubaridi wa kindani, hasa katika eneo linalofanyiwa kazi mara nyingi? Usiruhusu mambo haya yakuvunje moyo. Sali kwa Yehova, naye atakusaidia uendee eneo ukiwa na hali nzuri ya akilini. Utazame kila mlango kana kwamba unaweza kuwa na mtu ambaye ni aina ya kondoo nyuma yao. Kama Yesu alivyoagiza, acha mtu mmoja mmoja aonyeshe kama anastahili.—Mt. 10:11-14.

6 Hata katika eneo ambalo linafanyiwa kazi kwa ukawaida, huenda kukawa watu wengi ambao hawatolewi ushuhuda mara kwa mara kwa sababu hawapatikani nyumbani. Kuzuru nyakati mbalimbali ili kupata washiriki tofauti tofauti wa jamaa na kutunza maandishi ya nyumba kwa nyumba yaliyo sahihi kunafanya eneo lienezwe kwa ukamili zaidi.

7 Tangazo lililotangazwa rasmi na Mungu la habari njema nyumba kwa nyumba linakaribia mwisho walo kwa haraka. Tunataka kurudisha ripoti kwa Yehova na kusema kwa dhamiri nzuri: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.” (Eze. 9:11) Utendaji wa nyumba kwa nyumba kwa bidii utatuwezesha tufanye hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki