Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/88 kur. 1-2
  • Je! Wewe Unahubiri Ukiwa na Kusudi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unahubiri Ukiwa na Kusudi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUFANYA ZIARA ZENYE KUSUDI
  • RATIBU ZIARA
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kubali Daraka la Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Je! Wewe Unafanya Ziara za Kurudia Zako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Jipe Ujasiri wa Kufanya Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 10/88 kur. 1-2

Je! Wewe Unahubiri Ukiwa na Kusudi?

1 Yehova ni Mungu mwenye kusudi, na kazi zake zina kusudi. Ndivyo inavyopaswa kuwa kwa habari yetu, hasa kuhusiana na huduma yetu. Yesu aliwapa utume wanafunzi wake wahubiri habari njema kwa kusudi la kutoa ushuhuda. (Mt. 24:14) Tunapochangia utimizo wa utume huo, tunapaswa pia tuwe wenye juhudi kufuatia kupendezwa kote kunakoonyeshwa. Hilo linaithibatiwa na maneno zaidi ya Yesu yanayopatikana kwenye Mathayo 28:19, 20.

2 Ripoti za utumishi wa shambani zinaonyesha kwamba ziara za kurudia hazifanywi kwa wote ambao wanakubali fasihi. Huenda wengine wakajizuia, wakidhani kwamba ni wahubiri ambao wana ustadi na wenye utu wa kirafiki tu ndio wanaostahili kufanya ziara za kurudia. Hata hivyo, si jambo gumu kama ambavyo huenda wahubiri hawa wakawa wamewaza. Lakini tunahitaji kufanya ziara zetu za kurudia ziwe zenye kusudi.

KUFANYA ZIARA ZENYE KUSUDI

3 Unapopata mtu anayependezwa, ni jambo zuri kuweka msingi wa ziara ya kurudia mara moja. Jinsi gani? Wengine wameliona kuwa jambo lenye matokeo kumwacha mwenye nyumba na swali ambalo linaweza kujibiwa katika ziara inayofuata. Wengine wameweza kuangusha fasihi na kukazia jambo hususa ambalo litazungumziwa watakaporudi. Hakikisha unaandika jina la mwenye nyumba, habari iliyozungumziwa, itikio lake, na fasihi yoyote iliyoangushwa. Halafu, kabla ya kufanya ziara ya kurudia, rudia habari hiyo na ufikirie kwa sala yale utakayosema.

4 Wakati wa mwezi wa Oktoba tuna fursa nzuri ya kutoa uandikishaji wa Amkeni! na Mnara wa Mlinzi kwenye ziara za kurudia. Ingawa ni kweli kwamba maandikisho yanapatikana katika huduma yetu ya nyumba kwa nyumba, wahubiri wengi wamekuwa na mafanikio sana ya kupata maandikisho kwenye ziara za kurudia. Wengine ambao walipokea magazeti yetu tulipozuru mara ya kwanza huenda wakawa waliahidi kwamba wangeandikisha au walionyesha kwamba huenda wakaandikisha. Halafu kuna watu ambao tuna vikaratasi vya Uandikishaji Unaokaribia Kwisha, watu mmoja mmoja tunaopelekea magazeti kwa ukawaida, au watu ambao tumejifunza nao wakati uliopita. Kuwa na uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kunaweza kusaidia kujazia uhitaji wao wa kiroho.—Mt. 5:3.

5 Ikiwa unarudia mahali ambapo ulitumia Kichwa cha Mazungumzo cha sasa, unaweza kusema: “Nilipozungumza na wewe, tulizungumzia uhitaji wa aina ya binadamu kwa mambo ya kiroho na jinsi uhitaji huo unavyoweza kutimizwa kupitia funzo la Neno la Mungu. Angalia manufaa zinazowajia wale wanaojifunza Neno la Mungu. [Soma Yohana 17:3 na utoe maelezo.] Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni vifaa bora vya kusaidia kutimiza uhitaji wetu wa kiroho.” Halafu unaweza kuonyesha jambo hususa katika gazeti unaloonyesha na ueleze toleo la uandikishaji. Pia kumbuka kwamba, kusudi letu la kurudia ni kuanzisha mafunzo ya Biblia, kwa hivyo wanaweza kuelezewa pia mpango wa kujifunza.

RATIBU ZIARA

6 Wengine hawafanyi ziara za kurudia kwa sababu hawaratibu wakati halisi kwa ajili yazo. Ziara za kurudia zinaweza kufanywa jionijioni, miisho-juma, mara tu baada ya kumaliza ziara za nyumba kwa nyumba, au nyakati nyinginezo zinazofaa. Mbona usiweke mradi wa kibinafsi wa kufanya angalau ziara moja ya kurudia mara moja kwa juma? Tafuta msaada wa wale ambao wana ujuzi zaidi katika upande huu wa utumishi wa shambani. Uwe huru kuuliza kiongozi wako wa funzo la kitabu akupe madokezo kuhusiana na jambo hili. Pia, unaweza kutaka kupata ujuzi kwa kwenda pamoja na painia au mhubiri anayefanya vema katika kazi hii.

7 Mtume Paulo alitaja vyote viwili kupanda na kutia maji kuhusiana na huduma ya Kikristo. (1 Kor. 3:6, 7) Kwa hiyo tuna daraka la kuwarudia watu mmoja mmoja tukiwa na kusudi la kuanza funzo la Biblia. Hakika shangwe yetu itaongezeka ikiwa sisi tunahubiri tukiwa na kusudi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki