Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/92 uku. 1
  • Kubali Daraka la Ziara za Kurudia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kubali Daraka la Ziara za Kurudia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Takwa la Kufanya Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Je! Wewe Unafanya Ziara za Kurudia Zako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Je! Wewe Unahubiri Ukiwa na Kusudi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 1/92 uku. 1

Kubali Daraka la Ziara za Kurudia

1 Kuna hesabu fulani ya sababu zinazotusukuma tushiriki kikamili zaidi kwa kadiri tuwezavyo katika kufanya ziara za kurudia. Tunataka kutimiza kikamili kazi tuliyopewa kufanya, kama vile Paulo alivyofanya. (Mdo. 20:21, 24) Ikiwa tunarudia kikamili wale wanaopendezwa, tutadumisha dhamiri njema huku tukijaribu kutimiza huduma yetu kikamili.—2 Tim. 4:5.

2 Maarifa Hutufanya Tuchukue Daraka: Jambo la kwamba uhai umo hatarini lapasa kutusukuma kuwa wenye bidii kufanya ziara za kurudia. (Yn. 17:3) Maarifa yetu juu ya hukumu za Yehova na ukaribu wa Har–Magedoni yapasa yatuchochee si kuwaonya tu wabaya bali pia kusaidia wale ‘wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika duniani’ (Eze. 9:4) Wanahitaji kusaidiwa kuwa washirika pamoja na tengenezo lionekanalo la Yehova.

3 Watu wahitaji msaada ili kuelewa kweli kwa usahihi. (Mdo. 8:30, 31; 18:26) Hiyo ni sababu nyingine kwetu kukubali daraka letu kurudi na ‘kutilia maji’ mbegu za kweli zilizopandwa. Ni maendeleo gani ya kiroho ambayo sisi wenyewe tungalifanya kama isingalikuwa mtu fulani kurudi tena na tena kutusaidia kupata maarifa sahihi juu ya Yehova na makusudi Yake ya ajabu?—Mat. 7:12.

4 Onyesha Upendo na Bidii: Kufanya ziara za kurudia ni njia nzuri ya kuonyesha upendo wetu kwa watu. Ndugu mmoja kipofu anayetumika akiwa painia wa kawaida alisema: “Tangu ubatizo wangu, tamaa yangu imekuwa kuwaambia wengine yale niliyokuwa nimejifunza kutoka katika Biblia. Nilifurahi kwamba kizuizi changu hakikunizuia nisifanye hilo. . . . Nilijifunza pia kuweka akilini rekodi ya kila nyumba mtaani, na kwa njia hiyo, niliweza kufanya ziara za kurudia kwa watu waliopendezwa na funzo la Biblia.” Ndugu huyo kipofu aweza kwa kweli kuona kwa moyo wake, na hajizuii kufanya ziara za kurudia na kudhihirisha upendo wake wa Kikristo kwa wengine.

5 Tunapofanya ziara za kurudia, mara nyingi huwa tuna fursa za kutumia Biblia zetu sana na kutoa sababu za tumaini lililo ndani yetu. (1 Pet. 3:15) Hilo halisaidii mwenye nyumba tu bali pia huwasha bidii yetu wenyewe na uthamini wa ile kweli. Kufanya ziara za kurudia huleta shangwe isiyoweza kupatikana kwa njia nyingine yoyote. Na sifa ya shangwe hiyo haipaswi kupungua. Hiyo yaweza kufanywa upya mara kwa mara kwa kufanya ziara za kurudia kwa bidii.—Mit. 10:22.

6 Ni lazima tuchukue daraka letu la kufanya ziara za kurudia kwa uzito. Watu wa Yehova hawazuilii yaliyo mema kwa wengine, na hilo laweza kuonwa kutokana na utendaji wetu wa ulimwenguni pote katika mwaka wa utumishi wa 1991. (Mit. 3:27) Tulifanya ziara za kurudia 344,926,952 na tukaongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani 3,947,261. Kulikuwa na wanafunzi wapya 300,945 waliojiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa. Ongezeko hilo zuri ajabu halingalitokea kama hatungalikuwa na nia ya kukubali daraka la kufanya ziara za kurudia.—1 The. 2:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki