Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
Juma Linaloanza Desemba 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: Je! Utumishi wa Upainia Ni kwa Ajili Yangu? Katika Afrika Mashariki asilimia 9 hivi ya wahubiri wote ni mapainia wa kawaida. Toa tarakimu za kwenu kwa ulinganisho. Je! wengi zaidi kati yetu, kutia na vijana wanaokaribia kumaliza shule, waweza kupata wakati kufanya utumishi wa wakati wote? Wahoji mapainia wa kawaida watatu, afadhali wawe kijana mmoja, mke wa nyumbani, na mtu aliyestaafu. (Ikiwa mapainia wa kawaida hawapatikani, mapainia wasaidizi au wahubiri ambao wamepainia waweza kutumiwa.) Fikiria hali ya fedha. Ni kazi za aina gani za nusu wakati zinazopatikana katika eneo lenu? Kila mtu hulipiaje gharama za kila siku? Ni mabadiliko gani wamefanya kuhusu tabia za kutumia fedha? Fikiria ratiba inayowawezesha kutimiza saa. Je! kuna wowote wenye matatizo ya kiafya? Wao hukabilianaje? Ni matatizo gani mengine ambayo wamekabili na kufanikiwa? Mahoji yapasa kuwa chanya na yenye kutia moyo. Uliza wasikilizaji kwa uchangamfu kufikiria hali za kibinafsi ili kuamua ikiwa wengi zaidi waweza kufanya utumishi wa wakati wote.
Dak. 20: “Wajulishe Wote Kwamba Usalama Ulimwenguni Pote U Karibu.” Baada ya maelezo mafupi ya utangulizi, kwa kadiri wakati uruhusuvyo fikiria kila kiunganisho na wahubiri waliojitayarisha vizuri watoe wonyesho wa utumizi wacho. Ikiwa inatumika, ingekuwa vema kijana atoe wonyesho wa Kiunganisho Na. 2. Kiunganisho Na. 3 charuhusu mhubiri aache katika akili ya mwenye nyumba angalau wazo moja la Kimaandiko lenye kupendeza. Pia, toa wonyesho wa kiunganisho kimoja kutoka kwa Kichwa cha Mazungumzo, “Biblia—Mwongozo Ufanyao Kazi kwa Siku Yetu” kipatikanacho katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1991 kwa kutumia picha iliyo katika ukurasa 172, 173 wa kitabu Usalama Ulimwenguni Pote. Eleza juu ya matarajio ya wakati ujao kwa wale wanaokubali Biblia kuwa mwongozo wao wa leo. Au waweza kuonyesha kiunganisho kwa kitabu kimoja kati ya vitabu vya zamani vilivyochapishwa kabla ya 1983 ambavyo kundi linavyo akiba. Watie moyo akina ndugu kwa uchangamfu kutumia moja la matangulizi yaliyodokezwa katika ukurasa 4 na kimoja cha viunganisho hivyo.
Wimbo 30 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 6
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Tia ndani ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji.
Dak. 17: Hati ya Kitiba na Kadi ya Utambulisho. Mwandishi aone kwamba kadi zimegawanywa na azungumzie mafungu 1, 2, 4-7, 9 na 10 ya barua ya Sosaiti ya Januari 1, 1991, kuhusu jambo hili. Sababu pamoja na wasikilizaji kwa nini maagizo hayo yapasa kufuatwa kwa uangalifu ili kadi zituhami kwa mafanikio zaidi iwezekanavyo. Wazee waweza kufanya kama walivyofanya mwaka jana. Msikawie kujaza kadi na kuhakikisha kwamba zimetiwa sahihi ifaavyo.
Dak. 20: Jinsi Mzazi Aliye Peke Yake Anavyoweza Kusaidia Watoto Wake. Utangulizi mfupi ukifuatwa na wonyesho wa mama mwenye watoto wawili wanaojitayarisha kwa utumishi wa shambani. Kuna familia nyingi zaidi zenye mzazi mmoja katika tengenezo leo kuliko wakati mwingine wowote. Njia ambayo mama na nyanya ya Timotheo walitia kweli ndani yake huandaa mfano mwema wa kufuatwa na wazazi wote. (2 Tim. 1:5; 3:14, 15) Wonyesho: Mama, binti tineja, na binti mchanga zaidi wamekaa kwenye meza jikoni, baada ya kumaliza chakula cha jioni. Mama asema kwamba kabla ya kuosha vyombo watapitia tena utoaji wao wa utumishi na kwamba yeye atakuwa mwenye nyumba. Binti mchanga zaidi achagua utangulizi kutoka ukurasa 4 wa Huduma ya Ufalme Yetu na kuutoa kwa mama yake. Mama ampongeza kwa uchangamfu kwa utoaji uliofanywa vema na kumuuliza asome andiko lililodokezwa na Sosaiti. Binti mchanga zaidi upesi afungua Isaya 9:6, 7 na kulisoma. Ndipo mama amuuliza binti mkubwa jinsi atakavyotoa kitabu. Binti achagua kiunganisho kutoka ukurasa 1 wa Huduma ya Ufalme Yetu na kukitoa kwa mama yake. Mama ampongeza halafu atia moyo wasichana wote wawili kujizoeza utangulizi pamoja na kiunganisho ili kutoa kitabu katika utumishi wa shambani. Mabinti waambiwa kwamba wajizoeze muda zaidi kidogo halafu waoshe vyombo. Mzee amalizia sehemu kwa kutia moyo familia zote katika kundi kuandaa msaada wenye upendo kwa watoto wao.
Wimbo 183 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Mfikio Wenye Kutumika kwa Matayarisho ya Utumishi wa Shambani.” Zungumza makala pamoja na wasikilizaji, halafu uwaulize wahubiri watatu au wanne waliogawiwa kutoa maelezo hususa juu ya njia ambazo kwazo mfikio huu waweza kuwafaidi. Kwa mfano, wanaweza kueleza juu ya unamna-namna wa utolewaji, njia ambazo habari yaweza kutumika katika eneo la kwenu, ubadilikano, au kwamba mfikio huu huruhusu wahubiri kuchagua habari wanayohisi wamestareheka zaidi kuitoa. Tia moyo wahubiri walete nakala zao za Huduma ya Ufalme Yetu katika mikutano ya utumishi wa shambani.
Dak. 20: “Matangulizi ya Kuwafanya Wenye Nyumba Wasikilize.” Kwa ufupi fikiria jinsi eneo lenu lilivyo. Ni mambo gani yaliyo ya maana kwa wenye nyumba? Kazia utangulizi na utoaji uelekeao kuwa wenye mafanikio kwenu. Mhubiri aliyejitayarisha vizuri aonyeshe utoaji huo na atoe kitabu Usalama Ulimwenguni Pote. Mhubiri apaswa kufanya utoaji kama ulivyoonyeshwa katika makala. Halafu kijana wa umri wa kwenda shule aweza kuonyesha utoaji uo huo na kumalizia kwa kutoa magazeti kwa aliyependezwa. Watie moyo wote wajaribu njia hii katika utumishi wa shambani.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 20
Dak. 15: Mzee ashughulikie matangazo ya kwenu, Habari za Kitheokrasi, na kufikiria mahitaji ya kwenu. Kwa kadiri wakati uruhusuvyo, zungumzia mambo mbalimbali ya kusemwa kutokana na magazeti ya karibuni. Chagua moja litakalopatana vema na mmoja wa matangulizi yaliyodokezwa na kiunganisho katika nakala hii Huduma ya Ufalme Yetu. Halafu mhubiri aliyejiandaa vizuri afanye utoaji akitumia utangulizi na kiunganisho, akitoa magazeti kwa mtu aliyependezwa. Eleza kwamba kwa kuhusisha watu katika mazungumzo na kutumia utoaji mbalimbali uliodokezwa, sio vigumu kutambua watu wanaopendezwa.
Dak. 18: “Kubali Daraka la Ziara za Kurudia.” Maswali na majibu. Watie moyo wote kwa uchangamfu kushiriki kikamili katika kufanya ziara za kurudia.
Dak. 12: Mazungumzo ya “Utoaji-Mimba” kutoka kitabu Kutoa Sababu, kurasa 395-7. Baada ya utangulizi mfupi kwa kichwa hicho, kuonyesha jinsi jambo hilo lilivyo katika habari leo na linavyohangaisha sana mamilioni ya watu, fanya kikao cha dada akiongoza funzo la Biblia. Mwanafunzi huyo mpya wa Biblia amwarifu dada kuhusu hangaiko lake kuu la kuwa mjamzito. Aeleza jinsi alivyo na wasiwasi, kwa sababu hali ya kifedha ya familia si nzuri. Watu wake wa ukoo wa kilimwengu wanamhimiza atoe mimba upesi. Dada adokeza watumie kitabu Kutoa Sababu na wachunguze Maandiko waone jinsi Yehova huuona uhai wa mtoto asiyezaliwa na kama huuona utoaji-mimba kuwa sawa. Kwanza wafikiria fasiri ya utoaji-mimba. Halafu wanazungumzia maswali, maandiko, na maelezo mengine katika kurasa 395-7. Dada huyo apaswa amsaidie mwanafunzi afikiri na kuthamini utakatifu wa uhai.
Wimbo 164 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 27
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wahubiri kufanya mipango sasa kufanya upainia msaidizi katika Machi na Aprili. Tia moyo familia, pamoja na wahubiri wachanga watakaokuwa likizoni Machi na Aprili, waone ni mipango gani wanaweza kufanya ili kuwa na ushirika zaidi katika utendaji wa utumishi wa shambani. Unaweza kutumia mawazo fulani kutoka makala “Umepangia Nini Machi na Aprili?” kutoka Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1991 ili kuwatia moyo akina ndugu waanze kujitayarisha sasa kwa kipindi cha Ukumbusho.
Dak. 15: “Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Katika Kaseti.” Ishughulikiwe kwa maswali na majibu. Kazia kwamba Sosaiti haitakubali daraka kwa kaseti zisizofikia wenyewe.
Dak. 15: “Kukopesha Wakristo Wenzetu Pesa.” Hotuba ikitolewa na mzee juu ya makala kutoka Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1991, kurasa 25-8.
Wimbo 147 na sala ya kumalizia.