Wimbo 183
Mahali pa Vijana Katika Mpango wa Mungu
1. Kunayo nafasi ndani ya mupango.
Mungu aita vijana, wazee.
Itikio lao linavutia we,
Wauhubiripo Ufalme wake.
Una matokeo ushuhuda wao,
Wako maridadi tena tayari!
Wanathaminiwa sana na Yehova;
Wanapendeza hata na wazee.
2. Itakuwa siku ya furaha sana
Kwa vijana wajuao Yehova!
Wana akiba ya wakati ujao
—Uzima wa milele Paradiso!
Sasa tunayo mikazo mingi sana
Ya mufumo utakaotoweka.
Lazima tupige vita tuushinde;
Sharti tushikamane na Ufalme.
3. Watapata rafiki walio wema.
Mbona wawe rafiki za ’limwengu?
Na wajishughulishe na yajengayo,
Kwenye kurasa za Neno la Mungu.
Wakati wa shida acheni vijana,
Watafute wale wawapendao.
Mungu ndiye Rafiki yao mukubwa;
Mwenye ufahamu hata rehema.
4. Tu washiriki wa kundi la Kikristo,
Humo Yesu atupa haja zetu.
Basi na tushikamane tu na yeye;
Na kuyatii mashauri yake.
Na tusifanane nao ulimwengu;
Mungu asafishe akili zetu.
Vijana na wazee tuaminike,
Tumusifu tukapate uzima.