Nufaika Kabisa na Mikutano ya Utumishi
1 Usemi wa kuhisi moyoni wa kila mtumishi wa Mungu wapaswa kuwa: “Ee BWANA [Yehova, NW], unifundishe njia yako; nitakwenda katika kweli yako; moyo wangu ufurahi kulicha jina lako.” (Zab. 86:11) Mkutano wa Utumishi huandaa maagizo hususa kutusaidia kutimiza kazi ya Yehova ya kuhubiri habari njema za Ufalme wake. Je! wewe hunufaika kikweli na Mkutano wa Utumishi kwa kufyonza shauri linalotolewa?
MANUFAA ZA MATAYARISHO MAZURI
2 Ili kunufaika kwa kadiri kubwa zaidi na maagizo yanayoandaliwa kwenye Mkutano wa Utumishi, kujitayarisha kimbele kunatakwa. Kwa nini? Kujitayarisha kikamili hutayarisha akili na moyo zipokee maagizo. Kwa kujifunza habari mbele ya wakati, kuitafakari, na kuchanganua maandiko yaliyotumiwa, utakuwa katika hali nzuri zaidi kufyonza na kukumbuka kile chakula cha kiroho kinachotolewa. Ushiriki wako mwenyewe katika kutoa maelezo, kushiriki katika mawonyesho, au kutoa hotuba kutakuwa kwenye kujaa maana zaidi. Moyo wako utajawa na utosheki kwa sababu wewe ulichanga kilicho bora.—Kut. 23:19a; Mit. 16:23.
3 Wakati wa kutayarisha, inasaidia kila mshiriki wa jamaa akiwa na nakala ya kichapo kinachotumiwa. Tayarisho ni la maana hasa kwa wale waliogawiwa sehemu katika programu ya Mkutano wa Utumishi. Migawo yapasa itolewe mapema vya kutosha kuruhusu wakati wa kutosha ili wanaoshiriki wajitayarishe.
MANUFAA KUTOKANA NA USHIRIKI NA UTUMIZI
4 Je! wewe umeona kwamba kushiriki katika mikutano huchangia sana uifurahie? Kama Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1973, ulivyoeleza kwenye ukurusa 18: “Furaha ya kweli inakuja wakati mtu anapoonyesha imani yake mwenyewe katika Yehova kati ya ndugu zake za Kikristo. Si shauri la kujiona kulazimishwa kutoa melezo kisha kuacha na sehemu inayobaki ya mkutano kuwaachia wengine. . . . Ni upendo wetu kwa Yehova unaojaa ndani yetu na kufurika hata tunataka kumhimidi Yehova na kuonyesha upendo wetu kwake.”
5 Sisi tuna mgawo kutoka kwa Yehova kuhubiri habari njema. Kwa upendo yeye ameandaa maagizo mengi kupitia Mkutano wa Utumishi ili kwamba kila mmoja wa sisi awe katika hali ya kutoa ushuhuda wa Ufalme ulio bora iwezekanavyo. Akiwa Mkufunzi Mkuu, Yehova anatazamia matokeo kutoka yale maagizo anayotolea watu wake. (Ona Kumbukumbu 17:10.) Kuzoea na kutumia yale unayojifunza kutakunufaisha wewe, nawe utaweza kusema, “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”—Eze. 9:11.
6 Pia wewe utakuwa na shangwe ya kujiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza. (1 Tim. 4:16) Hakuna shaka juu yalo, manufaa za kiroho kutokana na Mkutano wa Utumishi ni nyingi. Wewe na jamaa yako na mwe mmepiga moyo konde kujifaidi kabisa kutokana nayo!