Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/89 uku. 3
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wewe Huangalia Ubao wa Matangazo kwa Ukawaida?
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Kutambulisha Majumba ya Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Je! Wewe Unastahi Jumba la Ufalme Lenu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 1/89 uku. 3

Sanduku la Swali

● Ni habari gani inayopasa kuwekwa kwenye ubao wa habari wa kundi?

Ubao wa habari katika Jumba la Ufalme huandaa habari juu ya utendaji mbalimbali wa kundi. Hakuna habari inayopasa kuwekwa juu ya ubao wa habari bila kibali cha mwangalizi msimamizi.

Baadhi ya mambo yanayowekwa kwa ukawaida hutia ndani: Ratiba na migawo ya Mkutano wa Utumishi na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, orodha ya hotuba za watu wote ambazo zimeratibiwa, migawo ya mwenyekiti wa Mkutano wa Watu Wote na msomaji wa Mnara wa Mlinzi, mahali na wanaohudhuria Mafunzo ya Kitabu ya Kundi, julisho la ziara ya mwangalizi wa mzunguko inayofuata na habari inayohusiana, habari kuhusu kusanyiko au mkusanyiko unaokuja, na ratiba ya usafi wa Jumba la Ufalme. Nyakati fulani Sosaiti huagiza wazee kuweka barua fulani au habari nyingine. Ikiwa jambo lisilo la kawaida linatokea, baraza la wazee laweza kuamua kama ingefaa kuiweka kwenye ubao.

Ingawa tangazo fupi kuhusu ratiba ya arusi itakayofanyiwa katika Jumba la Ufalme laweza kufanywa wakati wa mmoja wa mikutano, tangazo rasmi halingewekwa juu ya ubao wa habari. Wala haingefaa kuweka matangazo kuhusu vikusanyiko ambavyo kihalisi ni vya asili ya kirafiki, kwa kuwa hivyo havihusiani na utendaji wa kundi.—Ona Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1984, ukurasa 12; Huduma ya Ufalme, Julai 1975, ukurasa 4, na Juni 1970, ukurasa 3.

Ubao wa habari wapasa kuwekwa ukiwa nadhifu na wenye kuvutia. Wapaswa kuwa mkubwa vya kutosha kuchukua habari zinazohitajiwa kabisa zilizotajwa hapa. Ratiba zilizomalizika na habari za ujumla ambazo kundi limepata kujua zapasa ziondolewe mara moja. Kundi zaidi ya moja linapokutana katika jumba lile lile, kila kundi lapasa liwe na ubao walo lenyewe wa habari, au sehemu ya ubao ulioonyeshwa waziwazi. Sisi tunapendekeza kwamba mwangalizi msimamizi, au mtu aliye chini ya mwelekezo wake, akague ubao pindi kwa pindi kuhakikisha kwamba habari zilizowekwa ni za wakati uliopo, zinafaa, na ni nadhifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki