Kutambulisha Majumba ya Ufalme
1 Kila Jumba la Ufalme katika maeneo yaliyo wazi na yaliyo huru yapasa kutambulishwa waziwazi na ishara inayofaa inayosema: “Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova.” Ishara hiyo yapasa kuwa nadhifu, yenye kuvutia, na kutunzwa vizuri.
2 Mahali ambapo makundi yanayotumia lugha tofauti yanakutania kwenye Jumba la Ufalme lile lile, kwa kawaida ishara ya Jumba la Ufalme ingepasa kubandikwa katika kila lugha. Bila shaka hilo linafanya iwe rahisi zaidi kwa watu wanaosema lugha hizo watambue mahali petu pa ibada. Mabaraza ya wazee ya makundi hayo yanayohusika yangepaswa kufanya mipango ya kubandika ishara zinazofaa za Jumba la Ufalme katika lugha za makundi yanayotumia Jumba la Ufalme fulani.—Flp. 2:4.
3 Kuongezea hayo, inapofaa, nyakati za mikutano zapasa kubandikwa na kusahihishwa ziwe zile zinazotumika kwa wakati huo. Jumba la Ufalme linalotumiwa na kikundi kinachozungumza zaidi ya lugha moja lapasa kuwa na ishara ya lugha nyingi nyingi ikionyesha nyakati za mkutano wa kila kikundi cha lugha tofauti.