Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/89 uku. 11
  • Wasaidie Wachanga Wanufaike Kutokana na Mkusanyiko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wachanga Wanufaike Kutokana na Mkusanyiko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI WAZAZI WANAVYOWEZA KUSAIDIA
  • TOA UANGALIFU KWA NIDHAMU NA SURA YA NJE
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1990
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Nufaika Kabisa Kwa “Ufundishaji wa Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1993
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Unakaribishwa Kwenye “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1989!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1996
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 10/89 uku. 11

Wasaidie Wachanga Wanufaike Kutokana na Mkusanyiko

1 Mwaliko wa kuhudhuria “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya unatolewa kwa kila mwabudu wa Yehova. Matayarisho ya mkusanyiko yamekwisha kufanywa, kwa kufikiria hesabu kubwa ya wachanga walio katikati yetu. Ndiyo, vijana, hata “watoto,” wanatazamiwa kuhudhuria.—Kum. 31:12.

2 Wazazi wapaswa kuwafundisha watoto wao kwamba mkusanyiko ni kwa ajili yao pia. Maendeleo mazuri ya kiroho yanaweza kupatikana ikiwa watoto wanafahamu kwamba kuwapo kwao na kusikiliza kwao programu ya mkusanyiko ni sehemu ya ibada yao. Inakubalika kwamba, si rahisi sikuzote wachanga wabaki wakiwa wameketi, wakiwa kimya, na wasikivu wakati wa vipindi. Pia, habari fulani inayotolewa huenda ikawa ngumu kwao kuelewa. Kwa hiyo ni jambo la muhimu wazazi waelekeze fikira daima na kujitahidi, ndiyo, wafanye kazi kwa bidii.

3 Ni jambo lenye kutia moyo kuona kupendezwa kikweli katika manufaa za kiroho kunakodhihirishwa na watoto wachanga na matineja wanaohudhuria mkusanyiko. Ijapokuwa idili fulani huenda sanasana ikatokana na fursa ya kusafiri, msisimuko wa umati, kula nje, na kadhalika, hata watoto wachanga sana wanaweza kusaidiwa wathamini mkusanyiko wenyewe na kupata manufaa za kiroho kwa sababu hiyo.

JINSI WAZAZI WANAVYOWEZA KUSAIDIA

4 Watoto wanapaswa kuelekeza akili zao kwenye mambo ya kiroho kwa kutazamia mkusanyiko. Kabla ya kuhudhuria mkusanyiko, mbona usiketi chini pamoja na watoto wako na kupitia habari iliyomo katika kitabu Insight chini ya kichwa “Ujitoaji Kimungu” (Godly Devotion)? Bila shaka itasaidia wote katika jamaa wanufaike kutokana na programu ya mkusanyiko.

5 Wazazi wengi wamepata matokeo mazuri sana kwa kuwaandaa watoto wao kwa kuwapa Biblia yao wenyewe, kitabu cha wimbo, na fasihi nyingine. Kuingiza akilini maoni yanayofaa ya Biblia na fasihi kutasaidia kudhibiti mwelekeo wa kucheza na vitabu kwa kuchora au kuandika ndani yavyo. Watie moyo watoto waandike mambo makuu, kisha yapitie pamoja na jamaa nzima wakati wa jioni. Pia, lingekuwa jambo zuri zaidi kutoleta vitu vya kuchezea, vitabu vya kuchora picha, na vitu vingine vya kuchezea kwenye mkusanyiko.

TOA UANGALIFU KWA NIDHAMU NA SURA YA NJE

6 Wazazi fulani wameruhusu watoto wao wawe wenye kusumbua wakati wa programu. Hata wakati wa sala, watoto fulani hucheza na kukengeusha fikira za wengine. Jiulize mwenyewe, ‘Watoto wangu wanafanya nini wakati wa sala? Je! wanapaswa kuruhusiwa kuacha viti vyao wakati wa programu?’ Wazazi wanaohangaika wanaliona kuwa jambo la hekima kuketi karibu na wachanga wao. Hili linawawezesha kutoa usimamizi unaofaa ili wasikengeushe fikira za wengine. Hata wakati wazazi wana madaraka yanayohusiana na mkusanyiko, wanapaswa kufanya kila jitihada kuketi na watoto wao wakati wa vipindi. Watoto wanahitaji pia usimamizi wa wazazi wao wenyewe wakati wa tafrija wanapokuwa mbali na mahali pa mkusanyiko.

7 Wachanga wetu wanavaliaje kwa ajili ya mikusanyiko? Ikiwa wanavalia kwa uzembe tu au wanavaa viatu vya kuchezea, je! hilo litawasaidia kufahamu uzito wa pindi hiyo? Kwa upande mwingine, watoto wanaovaa ifaavyo kwa ajili ya mikutano ya Kikristo wanaonyesha heshima na uzito kwa pindi hiyo. Hilo linaletea jina la Yehova sifa na heshima.

8 Kufikiria mambo kwa uzito kunaweza kutiwa moyo kwa kufanya mipango ili watoto wafanye kazi fulani baada ya vipindi. Kama ilivyotajwa katika nyongeza, watoto walio chini ya umri wa 16 wanaweza kufanya kazi pamoja na mzazi mmoja au mtu mwingine mzima mwenye daraka chini ya mwelekezo wa Idara ya Utumishi wa Kujitolea. Wachanga wengi wanaona huu kuwa upande wenye kunufaisha wa mkusanyiko.

9 Labda kwa kufikiria madokezo haya, wazazi na vilevile wengine wanaweza kuwa chonjo wawasaidie wachanga wapate manufaa kubwa zaidi kutokana na mkusanyiko.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki