Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/89 kur. 1-2
  • Vijana, Toeni Ushahidi kwa Matokeo Shuleni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana, Toeni Ushahidi kwa Matokeo Shuleni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI YA KUFANYA
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kitabu Kinachosaidia Watu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Endelea Kuyanena Mambo Uliyoyaona na Kuyasikia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Naweza Kuwahubiria Wanashule Wenzangu Vipi?
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 8/89 kur. 1-2

Vijana, Toeni Ushahidi kwa Matokeo Shuleni

1 Kumtumikia Yehova ukiwa kijana na mwenye kuthamini sana ahadi zake ni jambo zuri ajabu. (Mhu. 12:1) Nyinyi vijana mna fursa ya pekee kushiriki ukweli pamoja na wanadarasa wenzenu na walimu, eneo ambalo kwa ukawaida haliwezi kufikiwa na watu wazima. Je! nyinyi mko macho kuona njia nyingi ambazo kwazo mnaweza kutoa ushahidi kivivi hivi shuleni?

2 Kwa nini wengine wanaliona kuwa jambo gumu kushiriki ukweli pamoja na wengine shuleni? Je! inaweza kuwa kwamba wanahofu kile ambacho huenda wanadarasa wenzao wakawaza juu yao wakizungumza juu ya Mungu? (Linganisha Marko 8:38.) Labda ulipatwa na hofu ya aina hii ulipoanza kwenda nyumba kwa nyumba ukiwa na habari njema. Hata hivyo, ukithamini uhitaji ambao vijana wengine wanao kwa ajili ya ukweli, pia daraka lako mwenyewe ukiwa mwevanjeli, utatafuta fursa za kushiriki ujumbe wa Ufalme pamoja na wengine. (Mt. 9:36-38; Luka 12:8, 9) Ili uwe mwenye matokeo katika kuwatolea ushahidi kivivi hivi wale walio katika shule yenu unahitaji kujitayarisha mapema na kupanga mambo.

JINSI YA KUFANYA

3 Kijana mmoja alisoma kitabu chake cha Hadithi za Biblia kila siku shuleni wakati wa kipindi cha dakika 15 cha mapumziko. Mwanadarasa mwenzake alipouliza juu ya kitabu kile, alialikwa aketi chini wazungumze hadithi moja wakiwa pamoja. Baadaye, msichana huyo hakungojea aalikwe kujifunza bali alikuja akiwa na hamu nyingi ili wazungumze hadithi iliyofuata. Alishiriki na mama yake yale aliyokuwa akijifunza. Kama tokeo, mama yake alianza kujifunza Biblia na kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme pamoja na binti yake kijana.

4 Mbona usianze kuzungumza na wengine juu ya kitabu Hadithi za Biblia? Kwa kielelezo, unaweza kusema: “Kitabu hiki kinaonyesha jinsi Mungu anaweza kuwalinda watumishi wake waaminifu. [Fungua hadithi 79.] Yehova alimlinda Danieli katika tundu la simba. Je! unafikiri Mungu ataokoa watu wake kwa kukomesha maovu wakati ujao?” Baada ya kuruhusu jibu, unaweza kufungua hadithi 114 kuonyesha kwamba Yehova ataharibu uovu na kuokoa watu wake.

5 Unaweza kuweka kitabu Creation juu ya dawati yako ili wengine waweze kukiona. Au fursa inapotokea, unaweza kufungua picha iliyo kwenye ukurasa 83 kisha umwulize mwanadarasa mwenzako au mwalimu: “Je! unafikiri kwamba mababu wetu wa kale walikuwa na sura hii?” Baada ya kupata jibu, unaweza kuzungumzia habari iliyo kwenye ukurasa 89, mafungu 19 na 20. Huenda hamu ya wengine ikaamshwa wakionyeshwa vichwa vya sura vilivyoorodheshwa kwenye ukurasa 5. Ikitegemea itikio lao, unaweza kushiriki habari zaidi kutoka sehemu nyingine za kitabu Creation, au unaweza kuonyesha jinsi kitabu hicho kinavyoweza kusomwa kwa kusoma fungu kisha kuuliza swali lililo katika sehemu ya chini ya ukurasa.

6 Alipoingia kwenye shule ya sekondari, mhubiri mmoja tineja aliufanya uwe mradi wake kuanzisha funzo la Biblia. Mwanadarasa mwenzake alikuwa na matatizo fulani pamoja na wazazi wake naye akaongea na yule msichana Shahidi juu ya jambo hilo. Yule mhubiri kijana alimwonyesha makala inayofaa ya “Vijana Wanauliza . . . ” kutoka Amkeni! Yule mwanadarasa mwenzake alivutiwa na habari ile kisha akauliza maswali zaidi. Mhubiri kijana akamwangushia kitabu Kuishi Milele, akamweleza kwamba kingeweza kujibu maswali yake, na akaanzisha funzo la Biblia.

7 Ili tuwe shahidi wa Yehova, lazima tuzungumze juu yake. (Isa. 43:10-12) Je! wewe umefanya jitihada kwa weupe wa moyo kushiriki ukweli pamoja na wanadarasa wenzako na walimu katika shule yenu? Tayarisha vichwa vyenye kupendeza ili uzungumze nao juu yavyo. Fanya jitihada. Waulize wazazi wako au wengine wakusaidie. Sali kwa Yehova ili abariki jitihada zako, sawa na vile amebariki jitihada za wahubiri wengi vijana ambao ni wenye matokeo katika kutoa ushahidi kwa ajili ya Yehova shuleni.—Kol. 1:9, 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki