Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/89 kur. 3-4
  • Je! Unatumia Kile Ulicho Nacho?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unatumia Kile Ulicho Nacho?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUTOA MAHITAJI YA KIROHO YA SASA
  • UWE MTENDAJI—SI MSIKIAJI MSAHAULIFU
  • KUFANYIA MAENDELEO HUDUMA YETU YA SHAMBANI
  • Jinsi ya Kufanya Utafiti
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme kwa Msaada wa Index
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • ‘Kutafuta Maneno Yapendezayo, Yaliyo Sahihi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Tumia Vizuri Vichapo Vyetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 8/89 kur. 3-4

Je! Unatumia Kile Ulicho Nacho?

1 Yesu Kristo aliwapa wanafunzi wake mwongozo juu ya mambo yanayohusiana na ibada ya kweli. Kuhusu mazungumzo ya Yesu pamoja na wawili wa wanafunzi wake, Luka anaripoti kwamba Yesu “akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.” (Luka 24:27, 32, 45) Hakika wanafunzi waliburudishwa sana na kuimarishwa na fundisho lake. Hata hivyo, baada ya wakati fulani Yesu alilazimika kuwaacha. Wangewezaje kuelewa Neno la Mungu lililoandikwa bila yeye kuwapo? Je! wangejua jinsi ya kulitumia katika maisha zao?

2 Yesu hakuwaacha wanafunzi wake katika hali ya kutojua la kufanya, akiwaacha wafanye uamuzi wao wenyewe usiokamilika. Upesi wakang’amua kwamba wakati wa kukaa kwake pamoja nao duniani, Yesu alikuwa ameandaa habari nyingi ambazo zingeweza kutumiwa kwa matokeo katika mambo mengi mbalimbali. Waliweza kutambua jambo la kufanya ‘walipoyakumbuka maneno yake.’ (Luka 24:8; Yoh. 14:26) Halafu, maneno mengi ya Yesu yalirekodiwa katika Neno la Mungu kwa manufaa yetu.

3 Kundi la Kikristo lilipoanza kufanya kazi, wale waliokuwa wakitoa uongozi waliwasaidia akina ndugu wakumbuke yale ambayo Yesu alikuwa amewafundisha mapema. Katika barua yake ya pili, Petro aliandika: “Naziamsha nia zenu safi kwa kuwakumbusha, mpate kuyakumbuka yale maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume wenu.” (2 Pet. 3:1, 2) Kwa hiyo, katika visa vingi, hata wakati mambo ya maana sana yalikuwa yakizungumzwa, lilikuwa tu jambo la kutumia yale ambayo yalikuwa yameandaliwa tayari.—Mdo. 15:12-21.

4 Agizo hilo halikupata kamwe kuwa lisilofaa, wala halikuja kuwa la kikale. Kwa muda wa miaka, Yehova aliwapa watu wake ufahamu ulio waziwazi wa penzi lake hatua kwa hatua. (Mit. 4:18) Marekebisho yaliyofanywa katika ufahamu yalifasiliwa vizuri na yakaandikwa waziwazi na tengenezo. Katika yote haya, kanuni za msingi zimebaki zile zile. Kwa kielelezo, hiyo ndiyo sababu Mahubiri ya Mlimani ya Yesu yanatumika leo kama yalivyotumika yalipotolewa miaka karibu 2,000 iliyopita. Hakuna haja ya kupata ufunuo mpya wa ukweli hali yale tunayohitaji tayari yameandaliwa.

KUTOA MAHITAJI YA KIROHO YA SASA

5 Tangu miaka ya 1870, kundi la Kikristo la ki-siku-hizi limesonga hatua kwa hatua kuelekea ufahamu ulio wazi zaidi wa Neno la Yehova. Kwa miaka iliyopita, maswali mbalimbali yamezuka yakitaka majibu yaliyo wazi. “Mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu” ametoa ‘chakula kama hicho kwa wakati unaofaa.’ (Mt. 24:45, NW) Moja kwa moja, maswali yamefanyiwa utafiti kwa ukamili kwa kufikiria ukweli wa Biblia, na mwelekezo hususa umeandaliwa kwa ajili ya watu wa Yehova. Habari yote hii imepitishwa kwetu kupitia vichapo vya tengenezo la kitheokrasi, hasa gazeti la Mnara wa Mlinzi.

6 Kwa kupitia yale ambayo yamechapishwa kwa miaka iliyopita, ni wazi kwamba vichapo vya Sosaiti tayari vimeandaa mwelekezo kwa karibu habari yoyote ya Biblia inayoweza kuingia akilini. Mafundisho yamechanganuliwa kwa ukamili. Kanuni zinazoongoza mwenendo wa Kikristo zimefasiriwa waziwazi. Na matakwa ya kutimiza kazi kubwa ya kuhubiri yameonyeshwa waziwazi. Kama tokeo, habari nyingi za Biblia zimekusanywa kwa manufaa ya wote. Kwa kielelezo, mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni ghala zenye maagizo. Ikiwa tulikuwa na mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kuanzia 1960 mpaka 1988, maana yake tungekuwa na ensaiklopedia yenye mabuku 58 iliyojaa maarifa ya Kimaandiko yenye muhimu na pia habari juu ya mambo mengine yasiyohesabika. Ile sehemu “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” imechunguza mamia ya maswali. Hatuwezi kutaja habari fulani ambayo haijazungumzwa kwa njia fulani katika kimojapo vichapo hivyo. Kwa hiyo, tunapohitaji mwongozo katika njia fulani hasa, ni jambo rahisi tu kukumbuka jambo tuliloelekezewa fikira wakati uliopita.

7 Hata hivyo, kutafuta habari hususa ambazo tunahitaji kwa wakati ule kunaweza kuwa kazi kubwa sana kama tungetegemea kumbukumbu letu wenyewe. Kwa furaha, tengenezo limeandaa Watch Tower Publications Index 1930-1985 ambayo tunaweza kutumia ili tupate habari hususa kwa dakika chache tu. Index inarejezea vichapo zaidi ya 200 vilivyotolewa katika kipindi cha miaka 56. Je! umejifunza kutumia Index kutafuta habari unazohitaji? Je! wewe unatumia kile ulicho nacho? Pia, kuna Index za pindi kwa pindi katika lugha mbalimbali, na vichapo fulani vina fahirisi yavyo vyenyewe.

UWE MTENDAJI—SI MSIKIAJI MSAHAULIFU

8 Tengenezo linatusaidia tufahamu penzi la Yehova, kupitia vichapo vyayo. Tunapaswa kuwa watendaji na kutumia yale tunayojifunza badala ya kuwa wasikiaji wasahaulifu. (Yak. 1:25) Jambo tunaloelekezewa fikira halipaswi kuonwa kuwa agizo la kuwekwa kando na kusahauliwa baada ya kulizungumzia mara moja. Badala yake, tunapaswa tusikilize tukiwa na maoni ya kulikumbuka kukiwa na uhitaji wakati ujao. Ili tufanye hivyo, “ni lazima kwetu tuyaangalie zaidi kuliko kawaida mambo yaliyosikiwa na sisi.”—Ebr. 2:1, NW.

9 Tunawezaje ‘kuangalia zaidi kuliko kawaida’? Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 1989, ukurasa 14, unaeleza hivi: (1) Tunahitaji kuthamini tengenezo la Yehova na kuonyesha kwa ushirikiano wetu na ukawaida katika hudhurio la mikutano. (2) Lazima tuwe na bidii-endelevu katika kujifunza kibinafsi Neno la Mungu na vichapo vinavyoandaliwa na jamii ya mtumwa. (3) Ni jambo la maana tuchukue wakati wa kutafakari jinsi mambo tunayojifunza yanavyoweza kutumiwa katika maisha zetu wenyewe na kutumiwa kusaidia wengine.

10 Vichapo vinaandaa agizo linaloendelea juu ya jinsi tunavyoweza kukabiliana na matatizo tunayopata katika kulea jamaa zetu, kujiweka safi kiadili, na kushughulika na wengine. Tunaitikiaje agizo hilo? Je! unaliona kwa uthamini, ukiangalia kwa umakini mambo yanayokuhusu kibinafsi? Au je! unaliona kama jambo la kuwekwa kando, lenye upendezi wenye kupita. Uthamini unapaswa utusukume tufikirie habari hiyo na kutafakari juu yayo tukiwa na maoni ya kuikumbuka baadaye na kuitumia kikamili.—Isa. 48:17.

11 Tunahitaji kufanya zaidi ya kusoma tu yale ambayo yameandaliwa. Hilo linaweza kuwa jambo la vivi hivi tu au la kijuu-juu tu. Kujifunza kunamaanisha kuweka akili katika habari fulani kwa utaratibu ili tujifunze kwa ajili ya matumizi ya wakati ujao, jambo fulani liwe lenye kufikiriwa tukiwa na maoni ya kutenda. Hii inamaanisha kwamba tunapoanza kujifunza habari hiyo kwa kweli hali yetu ya akilini inaamua jinsi itakavyoingizwa sana katika akili zetu na kutumiwa katika maisha yetu ya kila siku. Tunapojifunza, tunapaswa tuendelee kuuliza: Hii inanihusuje mimi? Ninaweza kuitumiaje ili kuzidi kufanya maendeleo yangu ya kiroho? Ni mabadiliko gani ninayohitaji kufanya? Naweza kuitumiaje kusaidia wengine? Ningeweza kuielezaje kwa wengine?

KUFANYIA MAENDELEO HUDUMA YETU YA SHAMBANI

12 Kwa ukawaida Huduma ya Ufalme Yetu huchanganua mahitaji na maelekeo tunayopata katika huduma ya shambani, ikionyesha njia ambazo zitatusaidia kupata matokeo zaidi. Kwa kuwa inachapishwa kila mwezi, je! wewe una mbetuko wa kuona agizo layo kuwa linatumika au linalofaa mpaka tu wakati toleo jingine linapotokea? Sikuzote mmojapo miradi ya msingi katika huduma ni kufikia mioyo ya watu tukiwa na ujumbe wa Ufalme. Upendezi wa kibinadamu, hisia za kimoyoni, na mitazamo zimekuwa zile zile katika muda wa miaka iliyopita. Njia nyingi za namna-namna zinaweza kutumiwa kwa matokeo kuamsha upendezi. Huduma ya Ufalme Yetu inatuweka macho juu ya njia ambazo wengine wanatumia kwa mafanikio. Ingawa njia mbalimbali zimetokezwa kwa kipindi fulani, njia za msingi zinabaki zile zile. Madokezo yanayotolewa sasa huenda yalitolewa wakati uliopita, na huenda yakatumiwa tena wakati ujao.

13 Uandalizi mwingine wenye kutokeza umekuwa kitabu Reasoning. Ukurasa 8 unaeleza kwamba “matumizi ya kitabu hiki yanapasa yakusaidie wewe ukuze uwezo wa kusababu kutoka kwa Maandiko na kuyatumia kwa matokeo katika kuwasaidia wengine.” Wahubiri wengi wamesimulia maono yenye kupendeza sana yakionyesha jinsi kitabu hiki kimetumiwa ili kupata matokeo yenye kuridhisha. Habari yacho ni yenye kufaa kutumika katika karibu kila hali inayokabiliwa katika huduma yetu. Lingekuwa jambo lenye manufaa sana kupitia sehemu zilizochaguliwa kabla ya kushiriki utumishi wa shambani kila juma. Sikuzote tunapaswa tubebe nakala moja katika mkoba wetu wa vitabu. Pia imependekezwa kwamba tukitie miongoni mwa vichapo tunavyoleta kwenye mikutano kwa ukawaida. Kwa kuwa nacho tayari na kujua yaliyomo, tunajitahidi kweli kweli kuwa ‘tumekamilishwa tupate kutenda kila tendo jema.’—2 Tim. 3:17.

14 Tunaonyesha uthamini kwa kile ambacho Yehova ameandaa kwa kukitumia vizuri katika huduma yetu. Chakula cha kiroho kinachohitajiwa sana pamoja na mwongozo kwa ajili ya huduma yetu kimefanywa kipatikane kwa wingi. Tunahitaji ‘kutafakari hayo; tukae katika hayo.’ (1 Tim. 4:15) Hii itatusaidia tukumbuke yale tunayohitaji kwa wakati unaofaa. Tunapohitaji msaada ili tukumbuke, tuna vichapo ambavyo vimekusudiwa kuamsha kumbukumbu letu. Badala ya kutazamia kitu fulani kipya sikuzote, tunapaswa kushukuru kwa vile tulivyo navyo na kuvitumia kwa ukamili. Katika kufanya hivyo, tunajionyesha wenyewe kuwa watu waliokomaa “ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.”—Ebr. 5:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki