Tumia Vizuri Vichapo Vyetu
1 Tengenezo lionekanalo la Yehova limetuandalia unamna-namna mwingi wa vichapo ili kutusaidia katika kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha. (Mt. 28:19, 20) Uthamini wetu kwa vichapo vya Sosaiti wapasa utusukume tuvitumie vizuri katika huduma yetu.
2 Katika kutekeleza huduma yetu, tunataka kusaidia wenye mfano wa kondoo waingie katika barabara iongozayo kwenye uzima. Fasihi yaweza kutusaidia kufanya hivyo. Tunapozungumza Maandiko na mtu mwenye kupendezwa, huenda tukaona kwamba habari fulani mahususi inamvutia. Tukiwa tunafahamiana vizuri na habari yenye thamani iliyomo katika vichapo tofauti-tofauti, tutaweza kupatanisha utoaji wetu na kumtolea kichapo ambacho chahusiana hususa na mapendezi ya mtu huyo tunayesema naye. Huenda hilo likataka kufanya ziara ya kurudia tukiwa na kichapo kinachofaa.
TOA KINACHOHITAJIWA
3 Kwa kufanyia eneo letu kazi kikamili, tutapata watu ambao wanapendezwa kwa moyo mweupe katika Biblia na ambao wangependa kujifunza zaidi juu yake. Chochote cha vichapo vyetu chaweza kuwasaidia wapate kuelewa Biblia. Lakini ikiwa tunaongea na mtu ambaye anakosa imani katika Biblia naye aamini kwamba inajipinganisha au haipatani na sayansi, ingefaa kutoa kitabu The Bible—God’s Word or Man’s? Kichapo hicho hukanusha kabisa uchambuzi wa mwanadamu juu ya Biblia na kutoa maelezo yaliyo wazi juu ya kwa nini Biblia yapasa kukubaliwa kuwa Neno la Mungu. Au ungeweza kutoa kile kitabu Mankind’s Search for God, ukitumia Sura ya 15 na 16.
4 Watu wengi wanakabiliwa na matatizo katika maisha yao wenyewe ya kinyumbani. Huenda wasiwe na maarifa hata kidogo juu ya shauri la Biblia au juu ya jinsi ya kulitumia. Ili kuwasaidia wayaweze matatizo ya maisha na kupata utatuzi wenye kutumika, twaweza kutoa kitabu Maisha ya Jamaa au pengine twaweza kuelekeza fikiria kwenye sura za 5 hadi 8 katika kitabu Furaha. Huenda sikuzote mabadiliko yasije kwa haraka, lakini twaweza kutaja kwamba shauri la Biblia huleta matokeo kweli kweli.
5 Tunapotembelea watu wenye watoto, fikiria kutoa vichapo vilivyotayarishwa hasa kwa kuwafikiria watoto. Labda ungeweza kutumia kichapo Young People Ask. Wahubiri wengi wamesaidia wazazi na vijana vilevile kwa kutoa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia au Kumsikiliza Mwalimu Mkuu.
6 Ni rahisi kubeba trakti, na zinaweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo tunapofanya kazi nyumba kwa nyumba na pia wakati tunapotoa ushuhuda wa vivi hivi. Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa? ni trakti inayofariji sana, ikiwa na habari yenye thamani. Je! wewe unabeba trakti kadhaa mbalimbali? Je! una maelezo yaliyotayarishwa ya kuzitolea utangulizi?
7 Tushirikipo habari njema na wengine, sisi tunataka kutumia vizuri misaada mingi ya kujifunza Biblia tunayoandaliwa na “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” (Mt. 24:45-47) Wingi huo wa chakula cha kiroho huonyesha ukarimu wa Yehova na hali yake ya kuhangaikia ainabinadamu yote.