Kutangaza Habari Njema—Kwa Vichapo vya Zamani
1 Kufanya uamuzi wa kuabudu Mungu ni muhimu. Kunamaanisha uhai. Hivyo, kupata maarifa sahihi na hekima ya kuyatumia ni mradi unaostahiki.—Mit. 23:23; Yn. 17:3.
2 Ili kupata maarifa na kukua katika hekima, lazima sisi tujifunze kwa bidii-edelevu Neno la Mungu. Katika njia hiyo sisi tunafahamiana na amri zake, sheria, vikumbusha, na shauri. Pia sisi tunahitaji kutafakari juu ya historia ya shughuli za Yehova pamoja na watu wake. Yehova anatoa kwa ukarimu maarifa na hekima kwa wale ambao humtafuta yeye kwa moyo mweupe. Kwa muda wa miaka iliyopita, kupitia tengenezo lake, yeye ameandaa vichapo tele ambavyo huzungumzia nyanja nyingi za maarifa ya Biblia. Hivyo vyaweza kuwa manufaa kubwa kwa wengi ambao hawajamjua Yehova.
THAMANI YA VICHAPO VYA ZAMANI
3 Wakati wa Januari na Februari, chochote cha vichapo vya kurasa 192 kilichotangazwa kwa kupigwa chapa kabla ya 1980 chaweza kutumiwa. Mna habari nyingi sana katika vichapo hivi. Vinaweza kuwa vya thamani halisi ya kiroho kwa watu. (Ona Mathayo 5:14-16.) Kwa hiyo wakati wa hii miezi miwili, acheni sisi tujitahidi kuangusha vichapo vyote vya zamani ambavyo huenda kundi letu likawa navyo akibani.
4 Umaana wa kuweka vichapo hivi mikononi mwa watu unaweza kuonwa kwa kufikiria ono la mtu mmoja ambaye alipokea nakala zawadi ya kimoja cha vitabu vya zamani kutoka kwa mke wake, aliyekuwa Shahidi. Kufikia wakati huo, yeye hakuwa ameonyesha kupendezwa katika Biblia. Kwa mshangao wa mkeye, yeye alisoma kitabu chote katika jioni moja. Hilo liliimarisha sana imani yake katika Biblia kuwa Neno la Mungu hivi kwamba alihudhuria mkutano wa kundi uliofuata na akaomba funzo la Biblia. Katika muda wa miezi mitatu, yeye alikuwa akienda nje katika huduma ya shambani na sasa amebatizwa.
UWE NA MWELEKEO CHANYA
5 Usikadirie kidogo nguvu za Neno la Mungu. Kwa kuwa vichapo hivi vya zamani hukazia kweli za Biblia, vitoe kwa mwelekeo chanya. Bila shaka, utataka kuhakikisha kwamba vichapo vya zamani unavyovitoa viko katika hali nzuri. Ikiwa vitabu vimeharibika au kurasa vikageuka vikawa rangi manjano, havipasi kutolewa nyumba kwa nyumba, kwa kuwa kufanya hivyo kungeweza kupunguzia ujumbe thamani.
6 Ikiwa kundi lenu halina vitabu vyovyote vya kurasa 192 vilivyokusudiwa vitumie katika kampeni hii, basi mwaweza kuonyesha chochote cha vichapo vya kurasa 192 kwa mchango wa kawaida. Kama dokezo wakati wa kutumia vile vichapo vya karibuni zaidi ungeweza, baada ya kuzungumzia Ufunuo 21:4 pamoja na mwenye nyumba, kusoma fungu 3 kwenye ukurasa 184 katika kitabu Furaha au uvute fikira kwenye kisanduku kwenye ukurasa 25 katika kitabu “Ufalme Wako Uje” kama njia ya kuunganisha na toleo.
7 Sisi sote na tufurahie huduma yenye mazao kwa kushiriki maarifa kutoka kwa Neno la Mungu kwa vichapo hivi vya zamani! Hilo linaweza kutokeza masilani ya milele kwa wale tunaotolea ushuhuda.