Sura ya 3
Ufalme Unachomaanisha kwa Dunia Yetu
1, 2. Kuja kwa Ufalme kunaonyeshaje kwamba Mungu anajali dunia na watu wayo?
SALA ya kielelezo ya Yesu inaendelea kusema “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Mungu anapendezwa sana na dunia yetu na wote wanaoishi sasa na ambao wamepata kuishi hapa. Ndiyo sababu Ufalme unakuja, “kuharibu wale wanaoiharibu dunia,” kuandaa nafasi ya kufufua wafu, kumwondoa yule adui kifo na kufanya dunia yetu iwe makao ya wanadamu yenye furaha na amani —Ufunuo 11:15, 18, NW. 21:1, 3, 4.
2 Basi, jinsi imetupasa kusali maneno hayo kwa hamu nyingi, “Ufalme wako uje”! Huo ni ufalme wa Mu ngu ulio mikononi mwa Mwanaye, Bwana Yesu Kristo. Kupitia huo mapenzi ya Yehova, ambaye mwenyewe ndiye “Mfalme wa umilele,” yatatimizwa kweli kweli katika dunia hii. Ebu fikiria hiyo itakachomaanisha kwa watu wa mataifa yote:
YULE “MWANA-MFALME WA AMANI” ATAWALA
3, 4. (a) Umoja wa Mataifa umeshindwa ijapokuwa umejichukulia maneno gani ya unabii, na kwa sababu gani? (b) Ni njia gani peke inayoweza kuandaa amani yenye kuendelea, na kupitia nini?
3 Akiutazamia utawala wa Ufalme wa Kristo, nabii wa Mungu anamsimulia kuwa “Mwana-Mfalme wa Amani,” na kuongeza, “Kwa wingi wa utawala wa mwana-mfalme na kwa amani hakutakuwa na mwisho.” Nabii uyo huyo anatuhakikishia “Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.” Ijapokuwa maneno hayo ya mwisho yameandikwa kwenye ukuta wa uwanja mkubwa ng’ambo ya barabara ya kutoka Umoja wa Mataifa (U.M.), si shirika hilo la kimataifa lenye kupatwa na ugomvi mwingi linaloutimiza unabii huo. Maana U.M. umeshindwa kabisa kabisa kuwa chombo cha kuimarishia amani na usalama kati ya mataifa.—Isaya 2:4, UV; 9:6, 7, NW.
4 Amani ya kweli na yenye kuendelea inataka kila mtu atendewe haki, na uadilifu ufuatwe kweli kweli. Ufalme wa yule “Mwana-Mfalme wa Amani” pekee ndio waweza kuhakikisha hilo; ‘utaimarishwa ndi na kutegemezwa kwa njia ya uadilifu.’ Ndiyo, ufalme huo ni njia ya Mungu ya kuandaa “duniani amani miongoni mwa watu wenye nia njema.”—Isaya 9:7; 32:17; Luka 2:14, NW.
5. Katika kuimarisha amani ya kweli, ni mambo gani yenye kustaajabisha ambayo Ufalme unatimiza?
5 Ufalme huo utafanya hivyo namna gani? Kwa njia yenye kutokeza, itakuwa kupitia kule ‘kuja’ kwa ufalme wa Mungu ukiwa mikononi mwa “Mwana-Mfalme wa Amani” wake dhidi ya mataifa ya ulimwengu yenye kupigana. Zaburi 46:8, 9 inatukaribisha hivi: “Njoni myatazame matendo ya [Yehova], jinsi alivyofanya ukiwa katika [dunia]. Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari [ya vita].” Ufalme huo utapiga marufuku silaha zote za ujeuri. Isitoshe, hautaruhusu majambazi na wenye kulala wanawake kinguvu waotee watu katika barabara za mjini, maana chini ya ufalme wa Mungu “wapole wenyewe wataimiliki dunia, na watapata kweli kweli mteremo wao ulio bora sana kwa wingi wa amani.”—Zaburi 37:9-11, NW.
MFANO WA KIUNABII
6. Ni utimizo gani wa kiajabu wa unabii wa Biblia uliotokea katik karne ya sita K.W.K.?
6 Unabii mwingi wa Biblia unahusu ule utumwa Waisraeli wa kale. Baada ya kutumikia Babuloni muda wa miaka 70, baki lenye uaminifu la Waisraeli lilirudia nchi yao mwaka wa 537 K.W.K. Miaka yote hi yo, nchi ilikuwa imekaa ukiwa, ikiwa jangwa. Lakini sasa, kwa baraka ya Yehova juu ya watu wake, kukawa na mgeuzo wenye kustaajabisha. Unabii uliokuwa umeandikwa miaka mingi zamani ukatimizwa kiajabu:
“Nyika na mahali palipo ukiwa patafurahi; jangwa litashangilia na kuchanua maua kama waridi. Litachanua maua mengi, na kufurahi, naam, kwa shangwe na kuimba; litapewa uzuri wa Lebanoni, utukufu wa Karmeli na Sharoni; watauona utukufu wa [Yehova], ukuu wa Mungu wetu.”—Isaya 35:1, 2 ona pia Isaya 65:18-25; Mika 4:4.
7. Basi, tunaweza kutazamia nini kwa dunia yetu ufalme wa Mung ‘utakapokuja’?
7 Kama historia inavyoshuhudia, unabii wote huo ulitimizwa kiajabu juu ya watu wa Mungu waliorudishwa wakati wa karne iliyofuata kufunguliwa kwa Babuloni. Na ufalme wa Mungu ‘utakapokuja’ kubariki watoto wote wa Mungu hapa duniani, je! utakosa kurudisha hali za kiparadiso kwenye dunia yetu? Jibu ni Hapana kabisa! Ufalme huo utahakikisha kweli kweli kwamba limetimizwa kikamili lile agizo la awali ambalo Mungu aliwapa wanadamu ‘waitiishe dunia,’ waifanye yote iwe kama paradiso ya Edeni.—Mwanzi 1:28; 2:8-14; Isaya 45:18.
PARADISO YA DUNIANI POTE
8. Chini ya Ufalme huo, hali ya chakula na mafuta ya kutumia itakuwaje, na ni kwa sababu ya kufuata sheria gani?
8 Ufalme wa Mungu ‘utakapokuja,’ upungufu wa chakula na infuleshoni utatoweka, maana “kutakuwako wingi wa nafaka juu ya dunia; juu ya kilele cha milima kutakuwako mfuriko.” Baba yetu mwenye upendo ‘atafanya tena chakula kitokee katika dunia, na divai inayoufanya moyo wa mwanadamu anayekufa ushangilie, kuufanya uso ung’ae kwa mafuta, na mkate unaoutegemeza moyo wenyewe wa mwanadamu anayekufa.’ (Zaburi 72:16; 104:14, 15, NW) Hakutakuwa na matatizo ya ugavi wa chakula kati ya mataifa, hakutakuwako kupimiwa vitu, hakutakuwako milolongo ya kupata mafuta. Wanabiashara wenye pupa ya kujipatia faida watakuwa wamekwenda zao. Wanadamu wote wataitii ile amri ya kifalme, “Mpende jirani yako kama nafsi yako,” wagawiane vitu kulingana na uhitaji.—Yakobo 2:8.
9. Tuna uhakikisho gani kwamba hakuna kitakachoumiza wanadamu wakati huo?
9 Tena, tunaweza kutazamia kwamba Ufalme huo utazuia misukosuko ya nguvu za asili, kama vile matetemeko ya ardhi na tufani. Yesu alionyesha jinsi hilo lingeweza kufanywa alipotuliza “dhoruba kuu ya upepo.” Kwa njia hiyo, wanafunzi wake wakafahamu kwamba “hata upepo na bahari humtii.” (Marko 4: 37-41) Katika milki yote ya kidunia ya ufalme wa Mungu, hakutakuwa na kitu kinachoumiza au kuleta uharibifu.—Linganisha Isaya 11:6-9.
10. Miujiza mingi ya Yesu ilionyesha nini juu ya Ufalme huo?
10 Hospitali kubwa-kubwa hazitahitajiwa tena ili kutunzia humo wagonjwa wa mwili na akili. Ugonjwa wa moyo, kansa na magonjwa yenye kulemaza yatakomeshwa, maana Mganga Mkuu, Yesu Kristo, atatumia ubora wa dhabihu yake ya ukombozi ili “kuwaponya mataifa.” Miujiza mingi ya kuponesha wagonjwa na kufufua wafu aliyofanya Yesu alipokuwa hapa duniani ni kiishara tu cha yale atakayotimiza kupitia utawala wa Ufalme wake wenye nguvu. Hata hali ya kufa ambayo wanadamu walirithi itaondolewa, maana tunahakikishiwa kwamba “hakutakuwako tena na kifo.”—Ufunuo 21:4, HNWW; 22:1, 2; Mathayo 11:2-5; Marko 10:45; Warumi 5:18, 19.
11. Wakati wa utawala wa Ufalme wa Yesu, ni jambo gani litakalokamilisha furaha?
11 Nayo ni furaha gani!—makaburi hayatakuwapo ili yaharibu uzuri wa nchi, maana hata hayo yatakuwa yamekuwa matupu. “Malimbuko” ya ufufuo huo, yaani, wanafunzi washikamanifu wa Yesu 144,000, wataungana naye katika zile mbingu wawe washiriki wake katika ufalme wake. Pia ile ahadi ya ajabu ya Yesu itatimizwa ya kwamba wafu wale wengine walio “makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka . . . kwa ufufuo.” Hao watakuwa na nafasi yenye kupendeza ya kuletwa kwenye ukamilifu wa kibinadamu wawe raia za Ufalme hapa duniani.—Yohana 5:28, 29; Ufunuo 14:1-5; 20:4-6, 11, 12.
12. (a) Sababu gani imekupasa utake kuishi milele katika paradiso? (b) Kulingana na Yohana 17:3, ni lazima tufanye nini ili tuje kuwa humo?
12 Unataka kuwa mmoja wa wale watakaoishi waone dunia hii ikisafishwa uovu wote na kugeuzwa kuwa paradiso ya raha? Wataka kuwapo ukaribishe wafu watakaokuwa wakifufuliwa? Ungependa kuishi milele katika dunia itakayofanywa kuwa yenye utukufu—ambamo hakuna atakayedhoofishwa na uzee wala kuchoshwa na mapendezi yatakayofuatana na kila siku ya kuishi? Unaweza, ikiwa utafuata matakwa ya Mungu ya kupatia uzima. Yesu alisema kwa urahisi hivi, akisali kwa Baba yake: “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” (Yohana 17:3) Litakuwa pendeleo kama nini kuishi milele katika paradiso, wakati “dunia itajazwa maarifa ya utukufu wa [Yehova], kama maji yaifunikavyo bahari”!—Habakuki 2:14.
“MKATE WETU KWA SIKU HII”
13. Sababu gani tunaweza kusali tukiwa na hakika ya kupata “mkate wetu kwa siku hii”?
13 Walakini, sisi leo tunahangaikia sana mahitaji ya sasa. Kwa wengi wetu, kuchuma fedha na kuruzuku jamaa zetu kumekuwa tatizo kubwa. Hivyo hatuhitaji kusali tu Baba atakase jina lake kuu na kufanya mapenzi yake yatimizwe duniani kupitia kuja kwa ufalme wake; tunahitaji kusali ili Mungu atupatie mahitaji ya kila siku pia, atupatie “mkate wetu kwa siku hii.” Tunaweza kufanya hilo tukiwa na hakika kabisa kwamba, tukijitahidi kuzifuata kanuni za uadilifu za Mungu na kuziweka kwanza maishani mwetu zile faida za ufalme wake, Mungu atatimiza sehemu yake ya kuwa Mwandalizi Mkuu. Iko tu kama Yesu anavyoendelea kutuambia: “Msiwe na wasiwasi kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’ Kwa maana hivyo vyote ndivyo vitu ambavyo yale mataifa yanafuatia kwa bidii sana. Kwa maana Baba yenu wa kimbingu anajua mwahitaji vitu vyote hivyo. Endeleeni, basi, kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, na vitu vingine vyote hivyo vitaongezwa kwenu ninyi.”—Mathayo 6:11, 31-33, NW.
“UTUSAMEHE DENI ZETU”
14, 15. (a) Tunaposali maneno ya Mathayo 6:12, imetupasa tuwe tayari kutendaje? (b) Katika hilo, ni mifano gani ya ajabu tunayoweza kuiga?
14 Katika kujenga uhusiano wa karibu sana na Baba yetu, tunahitaji tuukubali kwa unyenyekevu udeni wetu kwake, na kukiri makosa yetu tunayofanyia Mungu na wanadamu wenzetu. Inafaa, basi, kusali hivi kwa Mungu: “Utusamehe deni zetu, kama vile sisi pia tumesamehe wadeni wetu.”—Mathayo 6:12, NW.
15 Ilikuwa ni fadhili ya ajabu, tusiyoistahili kabisa, Mungu kumtuma Mwanaye, Yesu, ulimwenguni, ili apate “kutoa nafsi yake ukombozi badala ya wengi” wetu sisi wanadamu. Hiyo inaweka msingi wa kusamehe dhambi zetu. (Mathayo 20:28, NW) Lo! ni kubwa kama nini rehema ya Mungu aliyowaonyesha hivyo wanadamu wenye dhambi! Jinsi tulivyo na sababu yenye kulazimisha, basi, tusamehe udhaifu wa wanadamu wenzetu! Imetupasa kuwa tayari kufanya hata zaidi ya hivyo: kusamehe hata dhambi nzito tunazotendwa. Kwa njia hiyo tunaweza kuonyesha wengine ile sifa ya upendo mwingi sana ambayo Yesu alisema ingekuwa alama ya kutambulisha Wakristo wa kweli.—Yohana 13:35; Wakolosai 3:13; 1 Petro 1:22.
“UTUKOMBOE KUTOKA KWA YULE MWOVU”
16, 17. (a) Tutayafahamuje maneno haya, “Usitulete katika kishawishi”? (b) Tunaweza kutendaje kupatana na sala ya ‘kukombolewa kutoka kwa yule mwovu’?
16 Hatimaye, Yesu anatuagiza tusali kwa Mungu hivi: “Usitulete katika kishawishi, bali utukomboe kutoka kwa yule mwovu.” (Mathayo 6:13, NW) Tusidhani kwamba Mungu anaweka vishawishi katika njia yetu, vituangushe. Badala yake, yule mwovu mwenye kumwasi Mungu, yaani, Shetani, ndiye anayetaka kutuondoa kwa Mungu.
17 Walakini, Baba anatutayarisha tuweze “kuzipinga hila za Shetani,” ndiyo, tushindane mweleka kwa kumshinda yeye na yale majeshi ya roho waovu ambayo anaongoza. Ili ‘tusiletwe katika kishawishi,’ Mungu anatuandalia suti kamili ya silaha za kiroho, tunayoweza kuvaa. Mtume Paulo anaisimulia katika Waefeso 6:10-18. Tunaposimama imara katika kutumia kifaa hicho alichotoa Mungu, na kuendelea kusali, yule Baba atahakikisha kwamba ‘hatuletwi katika kishawishi,’ bali ‘tunakombolewa kutoka kwa yule mwovu.’—1 Petro 5:6-9.
18. Kwa muhtasari, ni mambo gani yaliyo katika Sala ya Kielelezo?
18 Jina maarufu la Yehova na litakaswe upesi kupitia ‘kuja kwa ufalme wake.’ Mapenzi yake na yatimizwe katika dunia kwa kuondoa ubaya wote na kwa kuifanya iwe paradiso kote kote kwa sifa yake. Kwa kadiri mfumo mbovu uliopo utakavyoendelea kuwapo, Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo na atuandalie mahitaji ya maisha, atusaidie kudumisha uhusiano mwema pamoja na wengine na kutukomboa kutoka nguvu za Shetani. Hayo ndiyo mambo ambayo Yesu alitufundisha tusali. Sala yake ya kielelezo ina yote hayo.
[Sanduku katika ukurasa wa 25]
YATAKAYOFANYWA NA UFALME WA MUNGU
• Kutegemeza enzi kuu ya Yehova, kukomesha utawala wa Shetani.
• Kuondoa dini ya uongo na watawala waonezi duniani.
• Kuleta milki ya Kristo akiwa “Mwana-Mfalme wa Amani.
• Kufanya dunia yote ichanue maua iwe paradiso yenye utukufu.
• Kuondoa ukosefu wote wa nyumba, chakula na mafuta.
• Kuimarisha jamii yenye kutegemea upendo wa jirani.
• Kuongoza kani za asili, kuzuia misiba.
• Kuondoa mikazo, wasiwasi, maumivu, uchungu, uzee.
• Kumharibu adui kifo, magonjwa na huzuni yote.
• Kufufua mabilioni ya wafu, waishi milele duniani.