Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/90 kur. 1-2
  • Endelea Kufundisha Bila Kuacha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kufundisha Bila Kuacha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FIKIA KILA MMOJA
  • PANUA HUDUMA YAKO
  • Sifu Yah kwa Njia ya Kupata Maandikisho
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Iweni na “Juhudi Katika Matendo Mema” Mwezi wa Aprili!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutoa Maandikisho kwa Ujasiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 10/90 kur. 1-2

Endelea Kufundisha Bila Kuacha

1 Biblia haituachi na shaka juu ya aina ya eneo ambalo mitume na wanafunzi wa Yesu wa mapema walikuwa nalo. Muda mfupi baada ya kifo cha Yesu, wenye mamlaka waliwaonya “wasiseme kabisa wala kufundisha” juu ya Yesu. (Mdo. 4:18) Kwa nini? Sababu moja ilikuwa lile fanikio lenye kushangaza walilokuwa wakipata. Maelfu walikuwa wakiwa waamini, kama vile Matendo 4:4 huripoti: “Wengi katika hao waliosikia lile neno waliamini; na hesabu ya watu waume ikawa kama elfu tano.”

2 Kwa sababu sisi pia twaendelea kufundisha bila kuacha, mamia ya maelfu, ndiyo, mamilioni wanakuwa waamini katika siku zetu. Wakati wa Oktoba tuna pendeleo la kutolea watu Amkeni! na Mnara wa Mlinzi kwa mpango wa uandikishaji. Hakuna shaka kwamba Amkeni! limetimiza sehemu muhimu katika kufanya watu waone uhitaji wao wa kiroho. Jambo hilo limeongoza wengi kwenye furaha, walipojifunza kufanya mapenzi ya Yehova.—Linganisha Mathayo 5:3.

FIKIA KILA MMOJA

3 Kwa kuwa sehemu kubwa ya eneo letu haienezwi kwa ukawaida, Oktoba utakuwa mwezi mzuri kufikia sehemu za eneo la kundi zisizofanyiwa kazi mara nyingi kwa toleo la uandikishaji. Hata katika eneo linalofanyiwa kazi kwa ukawaida jaribuni kujitahidi kipekee kunena na mwanamume mwenye nyumba mnapotoa ushahidi wa jioni au wa mwisho-juma. Kwa kutunza rekodi za nyumba kwa nyumba nzuri, twaweza kutafuta washiriki wengine wa familia, kama vile nyanya, mpwa au binamu ambaye huenda shuleni, au dada-mkwe ambaye hufanya kazi wakati wa juma. Jitihada hiyo ya ziada iliyofanywa ya kunena na kila mshiriki wa familia huenda ikathawabishwa sana.

4 Kuna njia nyingi nzuri za kupata maandikisho wakati wa mwezi. Moja ingekuwa kuwaalika wanafunzi wetu wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa waandikishe. Labda mmoja wa wanafunzi wa Biblia tayari ameandikisha mojapo magazeti. Kwa nini usidokeze apokee yote mawili? Familia zaweza kutiwa moyo zipate uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi kwa ajili ya kila mshiriki ili waweze kujitayarishia Funzo la Mnara wa Mlinzi. Dokezo jingine lingekuwa kusitawisha mpango wa kuwapelekea watu magazeti kwa ukawaida na kisha uwatolee uandikishaji wale wanaoonyesha upendezi zaidi ya ule wa kawaida. Twapaswa pia kujitolea tujifunze Biblia na wale wanaoonyesha kupendezwa halisi.

PANUA HUDUMA YAKO

5 Bado hujachelewa mno kujiandikisha kwa utumishi wa painia-msaidizi kwa mwezi wa Oktoba. Mkiwa familia, je! mnapanga kushiriki kazi ya painia wakati pindi cha likizo ya shule na sikukuu za kilimwengu za Desemba? Sasa ndio wakati wa kuanza kufikiria jinsi mwaweza kuifanya kwa mafanikio. Ikiwa familia yote nzima haiwezi kuwa mapainia wasaidizi, je! mwaweza kufanya kazi pamoja ili mmoja au wawili waweze kufanya hivyo? Ikiwa sivyo, ingewezekana angalau kutumia wakati zaidi katika huduma katika kutoa magazeti Amkeni! na Mnara wa Mlinzi?

6 Sisi twathamini zile manufaa na baraka za kiroho ambazo tumepokea kupita kurasa za Amkeni! na Mnara wa Mlinzi. Twajua kwamba watu mmoja mmoja wenye mioyo ya ufuatiaji haki katika eneo letu watanufaika sana kwa kusoma magazeti hayo kwa ukawaida. Wakati wa mwezi wa Oktoba, acheni sisi tuendelee na ufundishaji wetu kwa vifaa hivi vizuri ambavyo Yehova amefanya vipatikane kwetu. Kwa kufanya hivyo, sisi tutavuna baraka za Yehova na kujithibitisha wenyewe kuwa baraka kwa wengine.—Gal. 6:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki