Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/90 kur. 11-12
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Mwenye Nyumba Anapozungumza Lugha ya Kigeni
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kushirikiana Kuhubiri Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 10/90 kur. 11-12

Sanduku la Swali

● Ni mambo gani yanayopasa kukumbukwa wakati makundi yanayotumia lugha mbili au tatu tofauti yanafanyia kazi eneo lile lile moja?

Toleo la Aprili 1984 la Huduma ya Ufalme Yetu, chini ya “Kutangaza Habari Njema,” lilitaarifu hivi: “Wahubiri wa kila kundi wanapaswa kukaza jitihada zao kwenye watu wa lugha yao hasa.” Iko hivyo kwa sababu migawo ya eneo la kundi katika sehemu yenye lugha nyingi hutolewa kulingana na lugha. Makundi yenye kufanyia kazi eneo lenye lugha nyingi huenda yakaliona kuwa jambo lenye kusaidia kufanya orodha ya nyumba na majumba yenye vyumba vingi ambamo wahubiri wao hawapaswi kuzuru. Ni daraka la waangalizi wa utumishi wa makundi yanayohusika kufanyiza mfumo wenye kukubalika kwao wote kwa ajili ya kufanyia eneo kazi kikamili na kuelekeza wenye kupendezwa kwenye kundi linalofaa. Hilo lapasa kufanywa ili wenye nyumba wasisumbuliwe isivyo lazima na wahubiri wa makundi ya lugha tofauti, labda wakati wa asubuhi au alasiri ile ile. Sisi hatutaki ‘kuzuia habari njema ya Kristo.’—1 Kor. 9:12.

Wakati marekebisho yanapohitaji kufanywa kwa sababu ya watu kuhama, pelekeni kwa haraka majina na anwani za watu wenye kupendezwa kwa kundi linalofaa. Hilo litasaidia kuweka maandishi ya eneo yakiwa na habari za karibuni zaidi. Upendo, kuhangaikiana, uelewevu, utumizi mzuri wa akili, na ushirikiano ni mambo ya lazima.—Flp. 4:5.

Wanaposhiriki huduma wahubiri wanatiwa moyo wachukue fasihi katika lugha tofauti-tofauti. Hata hivyo, wakati wa kuangusha fasihi na kufuatia kupendezwa kokote tafadhali hakikisheni kuelekeza mwenye nyumba anayependezwa kwenye mikutano ya kundi inayofanywa kwa lugha ambayo mwenye nyumba anaelewa vizuri zaidi au kupendelea.

Kwa wazi nyakati fulani kutakuwako kupishana kwa jitihada zetu. Lakini kama ilivyotaarifiwa katika makala hiyo inayorejezewa juu, “ni jambo zuri kuweka kwanza akilini kwamba tunapohubiri, kusudi letu ni kufanya wanafunzi—kufundisha ukweli. (Mt. 28:19, 20) Kufundisha kwapaswa kufanywa katika lugha ambayo watu huelewa vizuri zaidi. (1 Kor. 14:9)” Kwa kukazia huduma yetu juu ya watu wanaoelewa vizuri zaidi au wanaopendelea lugha ya kundi tunalohudhuria, mema mengi yaweza kutimizwa katika kusaidia wengi zaidi wapate wokovu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki