Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Novemba uku. 8
  • Kushirikiana Kuhubiri Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushirikiana Kuhubiri Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Mwenye Nyumba Anapozungumza Lugha ya Kigeni
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kumhubiria Mtu Anayezungumza Lugha Nyingine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Tumepangwa Ili Kuwahubiria Watu Wote
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
mwb18 Novemba uku. 8

MAISHA YA MKRISTO

Kushirikiana Kuhubiri Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali

Wenzi wa ndoa wakiwa katika huduma ya shambani wamekutana na mwanamume na kijana wake wanaozungumza lugha tofauti na yao

Mara nyingi watu huitikia kwa utayari zaidi wanaposikia ujumbe wa Ufalme katika lugha yao ya asili. Huenda hiyo ndiyo sababu katika Pentekoste ya 33 W.K., Yehova alipanga mambo ili “Wayahudi waliomwogopa Mungu kutoka kila taifa lililo chini ya mbingu” wasikie habari njema katika “lugha [yao] ya asili,” ingawa inaelekea walizungumza lugha nyingine kama vile Kiebrania au Kigiriki. (Mdo 2:5, 8) Katika maeneo yenye lugha mbalimbali leo, makutaniko yanayoongoza mikutano katika lugha mbalimbali yanaweza kuwa yakihubiri kwenye eneo lilelile. Wahubiri katika makutaniko hayo wanawezaje kushirikiana ili kumtolea kila mtu ushahidi huku wakiepuka kuwaudhi wenye nyumba kwa kuhubiri mara nyingi katika eneo moja au kurudia kuhubiri katika eneo lililohubiriwa siku chache zilizopita?

  • Simu

    Zungumzeni (Met 15:22): Waangalizi wa utumishi wanapaswa kuzungumza na kukubaliana kuhusu mfumo utakaowaridhisha wote wa kueneza habari njema. Ikiwa eneo lao ni dogo, makutaniko yanayohubiri katika lugha nyingine huenda wakataka msihubiri kwenye nyumba zilizo katika eneo la lugha yao. Lakini ikiwa hawawezi kumaliza eneo lao kwa ukawaida kwa sababu ya ukubwa, huenda wakawaomba mhubiri nyumba zote, kisha muwaeleze mnapopata mtu anayependezwa. (od 93 ¶37) Au huenda wakaomba kutaniko lenu liwasaidie kuwapata watu wanaozungumza lugha ya kutaniko lao ili anwani zao ziongezwe kwenye eneo lao. (km 7/12 5, sanduku) Kumbuka kwamba katika visa fulani, watu katika nyumba moja wanaweza kuwa wanazungumza lugha zaidi ya moja. Mipango ya kushughulikia eneo inapaswa kufuata sheria za kulinda taarifa zinazotumiwa.

  • Nyumba katika eneo

    Mshirikiane (Efe 4:16): Fuata kwa uangalifu mwongozo wowote unaopata kutoka kwa mwangalizi wako wa utumishi. Je, unaongoza funzo la Biblia na mtu anayependelea lugha tofauti na ile ya kutaniko lenu? Huenda anaweza kufanya maendeleo haraka zaidi ukimpa mtu wa kutaniko au kikundi jirani kinachozungumza lugha yake.

  • Lugha mbalimbali

    Jitayarishe (Met 15:28; 16:1): Ikiwa mwenye nyumba katika eneo lenu anazungumza lugha nyingine, jitahidi kumtangazia habari njema. Unaweza kujitayarisha kwa kufikiria lugha ambazo huenda ukakutana nazo na kupakua mapema Biblia na video za lugha hizo kwenye kifaa chako. Unaweza pia kutumia programu ya JW Lugha kujifunza salamu katika baadhi ya lugha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki