Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kumhubiria Mtu Anayezungumza Lugha Nyingine
Kwa Nini Ni Muhimu: Yehova anapendezwa na hali njema ya kiroho ya watu wa ‘kila taifa.’ (Mdo. 10:34, 35) Kwa hiyo, Yesu alisema kwamba habari njema zingehubiriwa “katika dunia yote inayokaliwa” na “kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14) Nabii Zekaria alitabiri kwamba watu “kutoka katika lugha zote za mataifa” wangeitikia habari njema. (Zek. 8:23) Kulingana na maono ya mtume Yohana, wale ambao wataokoka dhiki kubwa watatia ndani watu “kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha.” (Ufu. 7:9, 13, 14) Kwa hiyo, tunapokutana na mtu ambaye anazungumza lugha nyingine, tunapaswa kujitahidi kumhubiria.
Jaribu Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Katika Ibada yenu ya Familia inayofuata, fanyeni mazoezi ya jinsi ya kumhubiria mtu anayezungumza lugha nyingine.