Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/91 kur. 1-4
  • Anzeni na Kumaliza Mikutano kwa Wakati

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Anzeni na Kumaliza Mikutano kwa Wakati
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Nufaika Kikamili na Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Mikutano ya Kuhimizana Ili Kupenda na Kufanya Kazi Nzuri
    Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Sanduku La Swali
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 4/91 kur. 1-4

Anzeni na Kumaliza Mikutano kwa Wakati

1 Mikutano yote ya kundi, kutia na mikutano ya utumishi wa shambani, yapasa kuanzwa na kumalizwa kwa wakati. Kwa nini? Kuanza kwa wakati kwaonyesha utaratibu na kuwafikiria wote wanaohudhuriao na kushiriki katika mikutano. (Mhu. 3:17b; 1 Kor. 14:33) Twaweza kuonyesha hangaikio letu kwa kushikamana na miongozo ifuatayo kuhakikisha kwamba mikutano inaanzwa na kumalizwa kwa wakati.

2 Sikuzote twapaswa kujitahidi kuwasili kwenye mikutano mapema vya kutosha ili kuzungumza na wengine, kushughulikia mambo ya lazima, na kushiriki katika wimbo na sala ya kufungua. Kwa kawaida, dakika tano zinaruhusiwa kwa ajili ya wimbo na sala. Wale wanaowakilisha kundi katika sala wapaswa kukumbuka kusudi la mikutano na kuonyesha jambo hilo katika sala zao za kufungua na kumalizia. Sala hizo hazihitaji kuwa ndefu.

3 Mkutano wa Watu Wote: Hotuba za watu wote zimewekewa muda wa dakika 45. Kupita wakati ulioruhusiwa kutaathiri Funzo la Mnara wa Mlinzi ambalo hufuata. Mikutano yote miwili, kutia na nyimbo na sala, yapasa imalizwe kwa saa mbili. Wasemaji wa hotuba za watu wote wapaswa wafuate wakati ulioonyeshwa katika muhtasari wa Sosaiti na wasiongeze mambo yasiyohusika, kama vile salamu. Ikiwa msemaji hafahamiani na mahali pa Jumba la Ufalme, apaswa kuuliza kutoka kwa kundi linalomkaribisha maelekezo na kiasi cha wakati kinaohusika katika kusafiri.

4 Funzo la “Mnara wa Mlinzi”: Saa moja inagawiwa Funzo la Mnara wa Mlinzi, pamoja na kusomwa kwa mafungu yote na maswali ya pitio ya kuzungumzwa. Maelezo mafupi na yenye kulenga maana ya utangulizi ya kiongozi yapaswa yaamshe kupendezwa na kuongoza kwenye somo. Maelezo na maoneleo yake wakati wa funzo yapasa kuwa machache. Kuigawia kila sehemu ya habari wakati wake kutasaidia kiongozi aepuke kutumia wakati mwingi mno katika sehemu ya kwanza ya somo na kupitia mbiombio sehemu ya mwisho.

5 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi: Huu ni mkutano wa dakika 45. Ingawa hotuba ya maagizo na mambo makuu kutoka usomaji wa Biblia hazikatizwi wakati unapokwisha, ni lazima ndugu wanaogawiwa sehemu hizi wasipitishe wakati walioruhusiwa. Ikiwa hilo halifanywi, shauri la faragha lapasa kutolewa. Pia, shauri na maelezo ya mwangalizi wa shule yapasa kufuata wakati uliogawiwa. Wakati waweza kuokolewa ikiwa wanafunzi wote wanakaa karibu na jukwaa na ikiwa kila mmoja amaliza hotuba yake mara moja wakati alioruhusiwa uishapo.—Ona Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1991.

6 Mkutano wa Utumishi: Huu ni mkutano wa dakika 45 pia. Pamoja na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na nyimbo na sala, programu yote isipite saa moja na dakika arobaini na tano. Ndugu walio na sehemu katika Mkutano wa Utumishi wapaswa washikamane na wakati uliogawiwa. Sehemu za kuzungumzwa kwa maswali na majibu zahitaji utangulizi mfupi tu. Hakuna haja ya kuongeza maelezo marefu ya utangulizi. Maonyesho yapasa yafanyiwe mazoezi vizuri, na washiriki wapaswa wawe tayari na katika mahali pao ili watumie vizuri wakati uliogawiwa sehemu hiyo.

7 Funzo la Kitabu la Kundi: Huu ni mkutano wa saa moja, kutia sala ya kufungua na kumalizia. Mafungu yote yapasa yasomwe. Ili kuhakikisha mkutano wamalizwa kwa wakati, kiongozi atagawia kila sehemu ya habari wakati ili kuepuka kupitia mbiombio sehemu ya mwisho ya somo au kumaliza mapema mno. Kiongozi ahitaji kuwa mwenye utambuzi kwa habari ya kiasi cha wakati kinachotumiwa katika kila fungu. Mambo makuu yapasa kueleweka wazi. Ustadi wa kufundisha wa kiongozi utamwezesha aliweze tatizo lolote kuhusiana na jambo hilo.—Tito 1:9.

8 Mikutano ya Utumishi wa Shambani: Hiyo haipasi kupita dakika 15, kutia na kufanya migawo ya eneo na kumalizia na sala. Wale wanaoenda nje katika utumishi wataka kuanza utendaji wao wa utumishi wa shambani upesi iwezekanavyo. Kiongozi ataanza mkutano kwa wakati, bila kukawia-kawia mpaka kikundi kikubwa kiwepo. Pia, mara migawo ya eneo ikiisha fanywa na mkutano kumalizwa kwa sala, kikundi chaweza kuondoka mara moja kwenda shambani. Hasa hilo ni la maana kwa mapainia ambao huenda wakawapo.

9 Sisi sote twaweza kunufaika kutokana na mikutano inayoanza na kumalizika kwa wakati. Hasa hilo lathaminiwa na wale walio na wenzi wasioamini ambao huwatarajia wawe nyumbani katika wakati fulani mahususi. Wakati wanapopangia usafiri kwenda na kutoka mikutanoni au wakati wanapotaarifu wakati watakaporudi nyumbani, wale wa kutoka familia zilizogawanyika wangefanya vema kukumbuka wakati wanaohitaji kabla na baada ya mikutano kwa ajili ya ushirika, kupata vichapo, na kadhalika. Pasipo shaka, kuanza na kumaliza mikutano kwa wakati huchangia kufanya mambo “kwa uzuri na kwa utaratibu.”—1 Kor. 14:40.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki