Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA APRILI 1
Dak. 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Zungumzia mambo makuu ya Ukumbusho, hesabu ya wapya waliokuwapo, na yale yanayoweza kufanywa juma hili kutia moyo hudhurio kwenye hotuba ya pekee, “Kuwapo kwa Mesiya na Utawala Wake,” katika Aprili 7. Pitia mipango ya utumishi wa shambani kwa juma hili. Pitia kifupi pamoja na kundi maagizo juu ya Jinsi ya Kushughulikia Maandikisho Ifaavyo (S-11).
Dak. 15: “Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme Katika Kundi.” Hotuba ikifuatwa na wonyesho uliotayarishwa vizuri, kiongozi wa funzo la kitabu akieleza wenzi wa ndoa jinsi ya kutumia Index kupata habari juu ya kwa nini na ni wakati gani kina dada wapaswa kuvaa vitambaa kichwani.
Dak. 18: Pitia Kichwa cha Mazungumzo. Zungumzia mambo tofauti-tofauti ya kuzungumziwa katika matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi. Watie akina ndugu moyo wafikirie kwa makini watu ambao wameonyesha kupendezwa kikweli na fasihi na ambao huenda wakaonea shangwe kupokea uandikisho. Mhubiri aliyejitayarisha vizuri atoe wonyesho wa Kichwa cha Mazungumzo. Katika kumalizia tafadhali onyesha jinsi ya kuhusianisha mazungumzo na makala inayofaa iliyoteuliwa kutoka toleo la karibuni la Mnara wa Mlinzi. Mhubiri huyo apaswa kuvuta fikira kwenye fungu mahususi au picha ambayo hufungamana vizuri na Kichwa cha Mazungumzo na ambayo itamfaa hasa mwenye nyumba huyo. Malizia sehemu hii kwa kutia wote moyo watumie Kichwa cha Mazungumzo.
Wimbo 60 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 8
Dak. 5: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Kutoa Habari Njema—Kwa Mafanikio Zaidi kwa Kusikiliza.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya habari. Wakati wa kuzungumzia fungu la 4, toa wonyesho wa jinsi mhubiri anavyokosa fursa ya kuwa na mazungumzo mazuri kwa kutokuwa chonjo kusikia maelezo ya mwenye nyumba juu ya jambo linalomhusu kibinafsi. Waulize wasikilizaji jinsi jambo hilo lingeshughulikiwa. Baada ya hapo, mhubiri uyo huyo arudie wonyesho, lakini wakati huu aonyeshe jinsi linavyopasa kufanywa ifaavyo kwa kusitawisha mazungumzo mazuri pamoja na mwenye nyumba.
Dak. 25: “Kuvuna kwa Kulingana na Kadiri ya Jitihada Yetu Binafsi.” Hotuba na mazungumzo yakitegemea makala ya nyongeza. Ishughulikiwe na mzee. Habari itumiwe ihusu kundi lenu. Mafungu na maandiko yaliyotajwa yaweza kusomwa kadiri wakati uruhusuvyo.
Wimbo 128 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Tia ndani maelezo ya uthamini wa Sosaiti kwa utegemezo wa kifedha kwa kazi ya ulimwenguni pote. Wapongeze ndugu kwa utegemezo wa ukarimu wa mahitaji ya kundi lenu.
Dak. 15: “Watie Moyo Wengine Wasome Mnara wa Mlinzi.” Hotuba yenye shauku ikifuatwa na maelezo mawili au matatu yaliyotayarishwa vizuri kutoka kwa wahubiri yakieleza kwa nini wanathamini Mnara wa Mlinzi na jinsi wamenufaika kwa kulisoma kwa ukawaida.
Dak. 20: “Anzeni na Kumaliza Mikutano kwa Wakati.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Someni mafungu yote.
Wimbo 8 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mipango ya usafi wa Jumba la Ufalme. Saidia akina ndugu wathamini uhitaji wa ushirikiano katika kuweka mahali pa ibada ya Yehova pakiwa safi.—Kupata habari zaidi ona makala “Je! Wewe Waheshimu Jumba la Ufalme Lenu?” kwenye ukurasa wa 7 wa toleo la Agosti 1989 la Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Tumia Vizuri Vichapo Vyetu.” Izungumzwe kwa maswali na majibu. Uwe na wonyesho mmoja kuonyesha jinsi ya kutumia trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani ili kuanza mazungumzo mlangoni.
Dak. 10: Kazi ya Wakaribishaji. Hoji ndugu asimamiaye wakaribishaji. Zungumzia wajibu wao mbalimbali na jinsi kundi liwezavyo kushirikiana na wakaribishaji. (Ona Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 63-4, na Huduma ya Ufalme Yetu, Desemba 1989, ukurasa 7.) Taja kwamba nyakati nyingine huenda wakaribishaji wakawajulisha wazazi uhitaji wa kuzuia masumbufu yanayosababishwa na watoto wao. Pia wakaribishaji huhakikisha mna starehe na utaratibu wakati wa mikutano yetu, huhesabu wanaohudhuria, husaidia wenye umri mkubwa na walemavu wapate viti, na kadhalika.
Dak. 10: Kutumia Trakti Katika Huduma. Waonyeshe akina ndugu trakti mbalimbali zinazopatikana, na uzungumzie njia mbalimbali ambazo katika hizo zaweza kutumiwa. Omba maelezo kutoka wasikilizaji juu ya jinsi wao hutumia trakti na labda wasimulie baadhi ya mambo yaliyoonwa ambayo wamepata. Katika Januari tulizungumzia jinsi trakti zaweza kutumiwa kuanza mafunzo. Waombe wasimulie matokeo ya njia hiyo. Ona pia kichwa cha Index “Trakti” ili kupata mambo zaidi yaliyoonwa kwa kuzitumia.
Wimbo 181 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA APRILI 29
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Usafi wa Kiadili Ndio Uzuri wa Vijana.” Hoji vijana kadhaa ukizungumzia habari katika Mnara wa Mlinzi, wa Novemba 1, 1989 kurasa 11-14. Huenda hata ukatumia maswali yaliyomo katika makala yakiwa msingi wa mazungumzo lakini haya yapasa yawe mahoji wala si funzo la Mnara wa Mlinzi
Dak. 15: Hubiri Nyumba kwa Nyumba. Hotuba yenye shauku na yenye kutia moyo ikitegemea Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 84-7. Itumiwe ihusu kundi lenu, ukivuta fikira kwenye mipango ya kundi kwa ajili ya kutoa ushuhuda kama kikundi nyumba kwa nyumba. Watie moyo wafanye angalau saa moja katika utumishi wa nyumba kwa nyumba Jumapili kabla ya kufanya ziara za kurudia na kuongoza mafunzo ya Biblia. Taja umaana wa kuzoeza wahubiri wapya wawe wenye mafanikio katika huduma ya nyumba kwa nyumba.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu au hotuba ikitegemea makala “Salini kwa Ajili ya Mtu na Mwenzake,” katika Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1990.
Wimbo 12 na sala ya kumalizia.