Habari za Kitheokrasi
◆ Australia iliripoti kilele kipya cha wahubiri 54,306 katika Machi, kilele chao cha tatu mfululizo.
◆ Bolivia ilikuwa na vilele vitano katika wahubiri wakati wa miezi saba ya kwanza katika mwaka huu wa utumishi. Kilele kipya kilifikiwa katika Machi, kukiwa na wahubiri 8,031 wakiripoti. Wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa saa 14.4 hudumani. Hudhurio la Ukumbusho lilikuwa 33,377, zaidi ya mara nne jumla ya hesabu ya wahuburi.
◆ Jamhuri ya Dominika ilikuwa na ongezeko la asilimia 13 katika Machi ikiwa na kilele kipya cha wahubiri 13,238. Hudhurio la Ukumbusho lilikuwa 52,340.
◆ Baada ya miaka tisa ya vizuizi, kwa mara nyingine tena Nikaragua ilianza kutenda ikiwa tawi katika Mei 1, 1991. Wamisionari watano ambao hapo kwanza walikuwa wamepewa migawo Nikaragua waliweza kurudi kuendelea na utumishi wao wa misionari huko.
◆ Ufilipino ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 108,456 katika Machi, kilele chao cha tatu mfululizo.
◆ Jumba la Ufalme la Njoro liliwekwa wakfu katika Mei 4 wakiwapo 279 kwa ajili ya programu ya kuwekwa wakfu.