Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/91 uku. 1
  • Kufahamu Umaana wa Matukio ya Wakati Huu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufahamu Umaana wa Matukio ya Wakati Huu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia Matukio ya Karibuni Katika Huduma Yako
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Kichwa cha Mazungumzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Tumia Matukio ya Sasa Kuamsha Upendezi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kutumia Magazeti Yetu Nyumba kwa Nyumba
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 10/91 uku. 1

Kufahamu Umaana wa Matukio ya Wakati Huu

1 “Mambo ya ulimwengu huu yanapita.” (1 Kor. 7:31) Hilo laonyeshwa na matukio ya wakati huu yenye kwenda kasi. Pamoja na yote yanayotukia ndani ya tengenezo la Yehova, hayo yamaanisha nini kwako wewe binafsi?—Lk. 21:28.

2 Utimizo wa unabii wa Biblia katika karne hii ya 20 huthibitisha kwamba mfumo wote mwovu wa mambo u katika siku zao za mwisho. (Mt. 24:3-14; Lk. 21:7-11) Yesu alisema kwamba “kizazi hiki hakitapita hata hayo yote yatimie.” (Lk. 21:32) Je! wewe unafahamu jambo hilo lamaanisha nini kwa watu katika eneo ambao bado hawajachukua msimamo wao upande wa Yehova? Ikiwa wafahamu, jambo hilo lina matokeo gani katika huduma yako ya shambani?—Lk. 21:34-36.

3 Saidia Wengine Maadamu Kuna Wakati: Yesu alihimiza wanafunzi wake watumie hali zenye kufaa wajulishe habari njema. (Yn. 9:4) Mtume Paulo alirudia onyo ilo hilo la upole alipohimiza ndugu katika Kolosai ‘waenende kwa hekima mbele yao walio nje, wakiukomboa wakati.’—Kol. 4:5.

4 Wengine wametii onyo la upole la mtume wakomboe wakati nao wamekuwa mapainia wa kawaida. Vijana wengi wamechukua utumishi wa painia wa kawaida wakati wangali shuleni nao wamekuwa na mafanikio mazuri kwa kufanya hivyo. Vijana shuleni waweza kukomboa wakati wawasaidie wanadarasa wenzao wafahamu umaana wa yale yanayotukia leo na tumaini jangavu kwa wakati ujao chini ya Ufalme wa Mungu.—Mhu. 12:1.

5 Twaweza kutumia vizuri wakati wetu katika huduma ya shambani wakati wa Oktoba kwa kutoa gazeti la Amkeni! katika kila fursa. Kichapo hiki kinatoa ufahamu wa ndani wa maana halisi ya matukio ya wakati huu. Kitoe kwa watu wenye kuhangaika uwapatao unapofanya kazi nyumba kwa nyumba. Chukua hatua ya kwanza ukitoe kwa wanashule wenzako au watu katika mahali unapofanya kazi. Kazia habari zinazoweza kupendeza kipekee watu unaojua. Kwa mfano, Amkeni! la Oktoba 8, 1991 (Kiingereza), lina makala juu ya watoto kutendwa vibaya. Watu wengi wanahangaikia jambo hilo.

6 Kichwa cha Mazungumzo cha wakati huu chaweza kutumiwaje? Wengi wamekuwa na mafanikio mazuri kwa kutumia utoaji uliodokezwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1991. Au, kwa ajili ya unamna-namna, baada ya kujijulisha ungeweza kusema: “Watu wanaopendezwa kufanyia maendeleo maisha yao huenda wakaonyesha jambo hilo kwa kufuata dini hususa. Lakini wengi wafanyao hivyo bado hawana furaha. Ni kwa nini iko hivyo? Kwa sababu kama vile Yesu Kristo mwenyewe alivyoonyesha hapa kwenye Mathayo 7:13, 14 si dini zote hukubalika kwa Mungu.” Ndipo ungeweza kusoma andiko hilo na kuendelea na Kichwa cha Mazungumzo cha wakati huu. Ili katika kumalizia utoe andikisho la Amkeni! ungeweza kusema hivi: “Kwa hiyo Mashahidi wa Yehova hutia moyo elimu ya Biblia ili kusaidia watu watambue wazi dini inayokubalika kwa Mungu. Kwa mfano, angalia habari inayozungumzwa katika gazeti letu la karibuni la Amkeni!” Kisha tafadhali ukazie makala hususa, ukurasa na fungu, unalohisi litampendeza mwenye nyumba.

7 Hakuna shaka kwamba hizi ni nyakati zenye kusisimua kuwa tukimtumikia Yehova. Uhakika huo na utusukume tutumie vizuri fursa mwezi huu tusaidie watu wenye mioyo myeupe waone umaana halisi wa matukio ya wakati huu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki