Wajulishe Wote Kwamba Usalama Ulimwenguni Pote U Karibu
1 Karibuni, “Mwana-Mfalme wa amani” ataleta amani na usalama wa kweli duniani pote. Imani yetu katika ahadi hiyo ya Biblia yapasa itusukume kuishiriki na wengine. (Isa. 9:6, 7, NW; Mik. 4:3, 4) Katika miezi ya Januari na Februari, tutatoa kitabu chochote cha kurasa 192 kilichochapishwa katika 1983 au mapema zaidi. Makundi ambayo hayana akiba ya vitabu hivyo yaweza kutoa kitabu Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani.”
2 Katika ukurasa wa 4 wa toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu, tumetoa hesabu fulani ya matangulizi ambayo huenda mkataka kutumia katika huduma wakati wa Januari. Viunganisho vitatu ambavyo vyaweza kusaidia kuelekeza fikira za wenye nyumba kwenye kitabu Usalama Ulimwenguni Pote vimedokezwa katika mafungu yafuatayo.
3 Kiunganisho Na. 1: Baada ya utangulizi wako, fungua ukurasa 13 na useme: “Isaya 9:6, 7 imenukuliwa neno kwa neno kutoka kwenye Biblia katika fungu hili la kwanza. Niruhusu nikusomee.” Halafu uliza: “‘Mwana-Mfalme wa amani’ ni nani?” Ruhusu jibu, halafu uendelee hivi: “Kitabu hiki kinamtambulisha wazi ‘Mwana-Mfalme wa amani’ na kinaeleza jinsi atakavyoleta amani ulimwenguni pote kwenye dunia katika wakati wetu. Je! unapendezwa kukisoma, na ungependa kujifunza zaidi kuhusu ulimwengu mpya ulioahidiwa?”
4 Kiunganisho Na. 2: Baada ya kusoma Isaya 9:6, 7, fungua ukurasa 4 na umwulize mwenye nyumba: “Ni hali zipi zenye amani unazoona kwenye picha hii?” Ruhusu jibu, halafu uendelee kwa kusema: “Kuna amani kati ya watu na amani kati ya wanyama. Amani na usalama halisi kama ilivyoonyeshwa kwenye ukurasa huu na kama ilivyotabiriwa katika Biblia lazima iwe imefanyizwa na Mungu, si na wanadamu. Wakubali hivyo?” Ruhusu jibu, halafu usome fungu la 4 katika ukurasa 5 na ueleze kwamba kitabu hiki kinajibu maswali mengi kuhusu Ufalme na amani duniani. Ikiwa mwenye nyumba anapendezwa kikweli na ujumbe wa Ufalme na ataka kukisoma kitabu hicho, mtolee kitabu hicho.
5 Kiunganisho Na. 3: Katika maeneo ambako watu wanaelekea kukatisha mazungumzo na hawakuruhusu umalize utoaji wako, huenda ukatumia mfikio huu: “Je! ninaweza kukuuliza swali?” Ikiwa mwenye nyumba akubali, endelea hivi: “Yesu alisema katika Mathayo 28:19, 20 kwamba wafuasi wake wangefanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote. Swali ni: Je! ingebidi ulimwengu wote uongoke kabla ya yeye kutawala akiwa ‘Mwana-Mfalme wa amani’? Maoni yako ni nini?” Ruhusu jibu, halafu useme: “Jibu la Biblia kwa swali hilo linapatikana hapa katika ukurasa 21.” Halafu soma fungu la 2 katika ukurasa 21, na uonyeshe jinsi maandiko yaliyonukuliwa katika kitabu hiki yanavyojibu swali hilo na mengi zaidi kuhusu usalama ulimwenguni pote na “Mwana-Mfalme wa amani.”
6 Huenda ulichagua utangulizi unaopenda kutoka ukurasa 4 wa Huduma ya Ufalme Yetu. Baada ya kupitia tena viunganisho katika makala hii, huenda ukapata kimoja hususa ambacho utafurahia kutumia. Chukua wakati kufanyia mazoezi utangulizi na kiunganisho chako kabla ya kwenda katika utumishi wa shambani. Matayarisho yako na usadikisho wako binafsi kwamba amani na usalama wa kweli utakuja kwa njia ya “Mwana-Mfalme wa amani” na Ufalme wake utaongezea kwenye usadikisho wako na uchangamshi katika kutoa kitabu Usalama Ulimwenguni Pote.