Mfikio Wenye Kutumika kwa Matayarisho ya Utumishi wa Shambani
1 Je! nyakati nyingine wewe husita kushiriki katika sehemu fulani ya utumishi wa shambani kwa sababu ya kutojua kile utakachosema? Ikiwa ndivyo, tuna hakika utathamini mfikio unaofuatiwa katika Huduma ya Ufalme Yetu.
2 Kuanzia na nakala hii, Huduma ya Ufalme Yetu itatoa unamna-namna mwingi zaidi wa madokezo ya kutoa ujumbe wa Ufalme, iwe ni katika nyumba kwa nyumba, ziara ya kurudia, au katika funzo la Biblia. Hayo yapasa kuchochea fikira zako juu ya maneno ambayo utapenda kutumia katika huduma. Unapojitayarisha kwa ajili ya huduma, chagua utoaji ambao unafaa eneo lenu. Halafu, amua kama utatumia maneno yaliyodokezwa katika makala au utabadili maneno ili kufaa hali za kwenu au utu wako mwenyewe. Utoaji wako huenda ukasikika kuwa maongeo ya kawaida ikiwa utasema kwa njia ya kawaida katika maneno yako mwenyewe. Je! ungependa kupanua huduma yako kwa njia fulani, labda kwa kushiriki katika sehemu fulani kwa mara ya kwanza? Madokezo yanayotolewa yakiwa na maelezo zaidi madogomadogo huenda yakawa ndio tu unayohitaji ili kuanza.
3 Ikiwa wewe huongoza mmoja wa mikutano ya utumishi wa shambani, unapaswa ufahamu vema habari iliyochapishwa katika Huduma ya Ufalme Yetu. Soma nakala yako kwa makini, na uvute fikira kwenye madokezo yanayoelekea zaidi kuwa yenye matokeo kwenu.
4 Sisi sote huonea shangwe mambo tunayofanya vema. Ni tumaini letu kwamba mfikio huu wenye kutumika utasaidia wahubiri wapya na wale wenye maarifa zaidi pia kuwa wenye matokeo na wenye shangwe katika huduma yao ya Ufalme.