Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/92 uku. 12
  • Sitawisha Utangulizi Wenye Kuchochea

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sitawisha Utangulizi Wenye Kuchochea
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Matangulizi Yenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kufanyia Kazi Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Utoaji Mbalimbali Ulio Rahisi na Wenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 10/92 uku. 12

Sitawisha Utangulizi Wenye Kuchochea

1 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! pia ni yenye mafaa katika kupanda mbegu za kweli katika akili na mioyo ya wasomaji. Kwa hiyo, tunataka tusitawishe njia zenye matokeo za kuacha magazeti hayo nyumbani mwa watu wanaoweza kunufaika na vito vya kiroho vilivyomo.

2 Wenye nyumba wanaweza kuchochewaje ili wakubali na kusoma magazeti yetu? Mengi yanategemea jinsi tunavyoyatanguliza. Madokezo mazuri sana juu ya kutayarisha matangulizi yenye matokeo yanapatikana katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 9-15. Unapotumia utangulizi wowote tafadhali kumbuka yale ambayo yameonyeshwa katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 9, fungu la kwanza, jambo la (3) kwamba tunapaswa tufikirie desturi zozote ambazo mgeni anatazamiwa afuate kabla ya kusema sababu ya kuzuru kwetu.

3 Unapotoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, huenda ukajaribu kutumia dokezo la tatu chini ya kichwa “Matukio ya Sasa” kwenye ukurasa 12 wa kitabu Kutoa Sababu.

Baada ya kujijulisha, ungeweza kusema:

◼ “Ikiwa ungeweza kuchagua, ni tatizo jipi kati ya matatizo mengi yanayokabili ulimwengu sasa ambalo ungependa kuona likitatuliwa kwanza?” Sikiliza itikio la mwenye nyumba, na ukubali hangaikio lake. Kisha ungeweza kuendelea, ukisema jambo kama: “Fikiria yale ambayo Biblia hutoa kuwa utatuzi kwa matatizo kama hayo. [Soma Isaya 9:6, 7.] Kwa hiyo utatuzi halisi kwa matatizo yote ya ainabinadamu uko katika utawala wenye haki wa Mesiya, Yesu Kristo.” Kisha ufungue ukurasa 8 na uelekeze fikira kwenye mafungu matatu ya mwisho ya makala yenye kichwa “Mesiya—Tumaini la Kweli?”

4 Ikiwa unatumia Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, ungeweza kutumia utangulizi katika ukurasa 12 wa kitabu Kutoa Sababu chini ya “Udhalimu/Kuteseka.” Zaburi 72:12-14 laonyesha wazi hangaikio la Mungu na lapasa kuthibitika kuwa lenye matokeo sana katika shamba letu. Halafu ungeweza kuvuta uangalifu kwenye habari chini ya kichwa kidogo katika ukurasa 7 labda ukitumia Ufunuo 21:1-5 katika utoaji wako.

5 Ikiwa unatumia Amkeni! la Oktoba 8 kuhusu “Wewe Unaweza Kushinda Hisiamoyo Zisizofaa,” huenda ukajaribu utangulizi wa tatu chini ya kichwa “Maisha/Furaha” kwenye ukurasa 11 wa kitabu Kutoa Sababu. Baada ya kuunganisha Zaburi 1:1, 2, ungeweza kuvuta fikira kwenye jambo linalofaa katika toleo hili au katika mojawapo matoleo ya karibuni zaidi ya Amkeni! yanayopatikana.

6 Inaelekea utapata wenye nyumba wanaosema wana fasihi yao wenyewe ya kidini. Unaweza kueleza kwamba sisi pia tuna vichapo tunavyotumia wenyewe (kama vile Huduma ya Ufalme Yetu); hata hivyo, majarida yetu husomwa na mamilioni ya watu ambao si Mashahidi wa Yehova. Dumisha mtazamo unaofaa unapotoa uandikisho na ikiwa toleo hilo halikubaliwi, basi toa magazeti ya karibuni zaidi.

7 Paulo alisema kwenye 1 Wakorintho 3:6: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.” Ikiwa tunataka Yehova afanye mbegu za ile kweli zikue mioyoni mwa wanaopendezwa, tunapaswa tutoe uangalifu katika kupanda mbegu hizo kwa matokeo kwa kutumia matangulizi yenye kuchochea.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki