Kutumia kwa Hekima Vyombo vya Muhimu
1 Unapotoa ushahidi kutoka nyumba hadi nyumba lengo lako lapasa liwe kumhusisha kila mwenye nyumba katika mazungumzo ya Kimaandiko, yenye kujenga kwa kutumia Biblia na vyombo vinginevyo vya muhimu. (Linganisha 2 Wakorintho 6:1; 2 Timotheo 2:15.) Watu katika eneo lako wanahangaikia nini siku hizi? Je! wana wasiwasi juu ya hali ya kiuchumi na kushuka kwa hali ya maisha ya familia? Maneno machache ya utangulizi juu ya kimojapo vichwa hivyo yaweza kuongoza kwenye mazungumzo mazuri ya Biblia.
2 Ungeweza kusema hivi:
◼ “Katika nyakati hizi zenye ugumu, watu wengi huliona kuwa jambo gumu kulipia gharama. Je! wafikiri matatizo yetu ya kifedha yatapata kusuluhishwa katika njia itakayo kuwa ya haki kwa wote? [Sikiliza jibu.] Mimi binafsi niliona wazo hili kuwa lenye kutia moyo sana . . . ”
3 Halafu ungeweza kusoma Zaburi 72:12-14 na kumaliza mazungumzo vizuri kwa kuchagua andiko la kuongezea kutoka kwa yale yalioko kwenye kurasa 328-9 za kitabu Kutoa Sababu. Au baada ya kusoma andiko, ungeweza kurejezea fungu moja katika trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Wahubiri wengi—kutia na wachanga—wanaanzisha kwa mafanikio mafunzo ya Biblia katika mojayapo trakti kwa kusoma fungu na kisha kumwomba mwenye nyumba maoni yake juu ya yaliyosomwa.
4 Katika jumuiya nyingine huenda ukapendelea kutumia mfikio huu:
◼ “Watu wengi wangependa kuona watu wakirudi kwenye thamani za familia za zamani. Je! wafikiri kila mtu mmoja mmoja ana haki ya kuamua thamani hizo, au kwapasa kuwe kiwango kimoja kwa kila mtu? [Ruhusu itikio.] Wengi hukubali kwamba ikiwa shauri la Biblia lenye hekima lingefuatwa, kungekuwako maendeleo yenye kutokeza katika hali ya maisha ya familia.”
5 Ndipo waweza ama kutaja na kuzungumzia taarifa ya mtume kwenye Wakolosai 3:12-14 ama kujaribu kuanzisha funzo la Biblia nyumbani kwenye ziara ya kwanza kwa kutumia habari chini ya kichwa kidogo “Ni Njia Ipi ya Kufaulu?” katika trakti Furahia Maisha ya Familia.
6 Ikiwa mwenye nyumba aonyesha kupendezwa, mwonyeshe thamani ya kimojapo vitabu vya Sosaiti vilivyojalidiwa vyenye kurasa 192 ambavyo mnatoa mwezi huu. Ikiwa toleo hilo halikubaliwi, tumia kwa hekima vyombo vyinginevyo vya muhimu kwa kushiriki jambo lifaalo katika trakti, gazeti, au broshua.
7 Ikiwa unaweza kuanzisha funzo kwenye ziara ya kwanza, fanya mipango hususa ya kuendeleza mazungumzo kwenye tarehe ya baadaye. Waweza kuwekea msingi ziara yako ifuatayo kwa kumwambia mwenye nyumba kwamba unaporudi ungependa kushiriki jibu la swali hili linaloulizwa kwa kawaida: “Kwa nini Mungu huruhusu uovu?” Makala iliyopo chini itadokeza jinsi habari hiyo inavyoweza kukuzwa kwenye ziara ya kurudia.